engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,150
- 1,437
Dr.Mwakyembe-Sitolipiza kisasi ni moja ya vichwa vya habari nilivyovisikia leo ktk magazeti ya Tanzania
je kuna ukweli wowote juu ya habari ama ripoti ya Mwana JF aliyoitoa hapa,juu ya afya ya Dr MWAKYEMBE?
Mwakyembe: Namwachia Mungu
NAIBU Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, ameshindwa kueleza moja kwa moja kama amelishwa sumu, badala yake amemwachia Mungu juu ya wabaya wake waliotenda kitendo hicho.
Dk. Mwakyembe alisema hayo nyumbani kwake jijini Dar es Salaam jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya afya yake tangu arejee kutoka nchini India alikokwenda kwa matibabu.
Oktoba mwaka huu, Mwakyembe alikimbizwa nchini India kwa matibabu zaidi baada ya hali yake ya afya kuzidi kuzorota, huku tetesi kizitolewa kwamba amelishwa sumu na watu wasiojulikana.
Hata hivyo, jana Dk. Mwakyembe alisita kuweka wazi ukweli wa suala la kulishwa sumu na badala yake alisema yeye si mtu wa kisasi kwa waliomtendea hayo, hivyo akasema anashukuru amerudi salama akiwa na afya njema.
"Siwezi kueleza moja kwa moja kwamba nimelishwa sumu, ninachoweza kusema nilikuwa na hali mbaya sana wakati napelekwa India kwa matibabu na nimerudi salama nikiwa na afya njema, namwachia Mungu alipe kisasi, mimi si wa kulipa," alisema kwa kifupi.
Dk. Mwakyembe ambaye alivalia kofia nyeusi ya pama kichwa huku akiwa na gloves mikononi pamoja na T-shirt ya mikono mirefu, vilivyoweza kuficha ngozi yake isionekane kabisa, alisema anafahamu siri ya ugonjwa wake na kamwe hayuko tayari kuieleza.
Kwa mujibu wa maelezo yake, uchunguzi wa ugonjwa uliokuwa ukimsumbua hadi kupelekwa nchini India, tayari umetumwa Wizara ya Afya, hivyo ni jukumu la wizara kuweka taarifa hadharani.
na Datus Boniface,Tanzania daima
je kuna ukweli wowote juu ya habari ama ripoti ya Mwana JF aliyoitoa hapa,juu ya afya ya Dr MWAKYEMBE?
Mwakyembe: Namwachia Mungu
NAIBU Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, ameshindwa kueleza moja kwa moja kama amelishwa sumu, badala yake amemwachia Mungu juu ya wabaya wake waliotenda kitendo hicho.
Dk. Mwakyembe alisema hayo nyumbani kwake jijini Dar es Salaam jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya afya yake tangu arejee kutoka nchini India alikokwenda kwa matibabu.
Oktoba mwaka huu, Mwakyembe alikimbizwa nchini India kwa matibabu zaidi baada ya hali yake ya afya kuzidi kuzorota, huku tetesi kizitolewa kwamba amelishwa sumu na watu wasiojulikana.
Hata hivyo, jana Dk. Mwakyembe alisita kuweka wazi ukweli wa suala la kulishwa sumu na badala yake alisema yeye si mtu wa kisasi kwa waliomtendea hayo, hivyo akasema anashukuru amerudi salama akiwa na afya njema.
"Siwezi kueleza moja kwa moja kwamba nimelishwa sumu, ninachoweza kusema nilikuwa na hali mbaya sana wakati napelekwa India kwa matibabu na nimerudi salama nikiwa na afya njema, namwachia Mungu alipe kisasi, mimi si wa kulipa," alisema kwa kifupi.
Dk. Mwakyembe ambaye alivalia kofia nyeusi ya pama kichwa huku akiwa na gloves mikononi pamoja na T-shirt ya mikono mirefu, vilivyoweza kuficha ngozi yake isionekane kabisa, alisema anafahamu siri ya ugonjwa wake na kamwe hayuko tayari kuieleza.
Kwa mujibu wa maelezo yake, uchunguzi wa ugonjwa uliokuwa ukimsumbua hadi kupelekwa nchini India, tayari umetumwa Wizara ya Afya, hivyo ni jukumu la wizara kuweka taarifa hadharani.
na Datus Boniface,Tanzania daima