Dr. Mengi atangaza zawadi ya ml.10

Dr. Mengi atangaza zawadi ya ml.10

hivi yule aliyeliaga bungeni alichukua hatua gani? na leo kama nimesikia BBC dira ya dunia kuwa albino wameandamana kuna mshtakiwa kasema anatumwa na viongozi. sasa wanamtaka awataje hao viongozi. du


Kuna mtu humuhumu amehusisha hiyo project na mambo ya uchaguzi unaokuja, inaonekana anaufahamu wa channels zilivyo, ofcourse lisemwalo siku zote lipo, lazima kuna wanaojua isipokuwa serikali haipo serious kuwashughulikia hao wanaotajwatajwa (politicians)
 
Mnafiki tu,watumishi wake wanaishi kwa shida nyingi mshahara mdogo,tukija kusikia mtumishi wake nae kaelekea huko kwa sababu ya shida sitashangaa, ni kampuni zake zinazoongoza kwa mishahara midogo,
Tatizo lenu mnaishi katika mfumo wa kibepari lakini bado mnafikiri kijamaa.kama mfanyakazi anaona anacho lipwa hakilingani na huduma anayo toa aache kazi.hakuna anae lazimishwa kukaa pale.
 
tatizo lenu mnaishi katika mfumo wa kibepari lakini bado mnafikiri kijamaa.kama mfanyakazi anaona anacho lipwa hakilingani na huduma anayo toa aache kazi.hakuna anae lazimishwa kukaa pale.

tena maulidi kitenge kaonesha mfano,karejesha mshahara wa mwezi mmoja kaacha kazi,
 
ha haa...asaidie watu aliowaajiri..unyonyaji na majungu vs undugu .... basic rights ni ndoto ukiwa chini yake. ila kwa ishu flani flani ndio kwanza kuita media na kuseek sympathy...damb
Acha chuki za kipuuzi, hiki alichokifanya ni kitendo cha kupongezwa! Kama ana mapungufu yake mengine hayafuti jambo jema analolifanya.
 
Umuofia kwenu watanzania wenzangu!
Mimi sijui mtz. mwenye dhamiri njema awezaje kumlaumu MENGI? Hivi kafanya kosa gani kutoa zawadi hiyo kuwezesha watuhumiwa kukamatwa? Hivi hawa wanaomsakama mengi wanatumwa na nani? Kwa kosa gani? Nani mjasiriamali anayejituma km huyu? Watz. acheni wivu wa kikike (Msekwa, 2002)
 
Mengi amesema atakayesaidia kukamatwa kwa waliomkata mkono Albino wa Tabora atamzawadia sh.10,000,000. Lakini pamoja na hayo, wengine wa mauaji ya hapo awali wamewahi kukamatwa na baadae kuachiwa licha ya kuwepo ushahidi wa kuthibitisha hilo.

mkono Tu 10mil Ni noma..
 
ha haa...asaidie watu aliowaajiri..unyonyaji na majungu vs undugu .... basic rights ni ndoto ukiwa chini yake. ila kwa ishu flani flani ndio kwanza kuita media na kuseek sympathy...damb
Matajiri (sijui watano) waliotajwa na jarida la Forbes hapa Tanzania huwezi kumsikia hata mmoja anahangaika na mambo ya haki za binadamu, rushwa au mambo ya kijamii mbali na kuendeleza philosophy ya utumwa na utwana. Ni Mengi pekee ambaye angala (kwa miaka mingi sasa) anaonekana.

Sasa kaahidi hiyo million kumi na waswasi uliopo ni pale mshukiwa akipatikana atapelekwa polisi/mahakama gani!? Maana hao waliokwishajulikana sote tunajua kinachoendelea hadi sasa.

Kwa haika wangelijitokeza watu wengine kuungana na Mengi tungelipunguza mateso haya ya binadamu pamoja na aibu tunayoipata kata taifa kwa maana ni Tanzania tu duniani kote inayoua binadamu kupata utajiri!

 
serikali ndiyo ya kulaumiwa kuhusu hili
 
Tatizo lenu mnaishi katika mfumo wa kibepari lakini bado mnafikiri kijamaa.kama mfanyakazi anaona anacho lipwa hakilingani na huduma anayo toa aache kazi.hakuna anae lazimishwa kukaa pale.

Kwa hiyo anatumia mfumo wa ubepari kufanya unyonyaji? Kama bosi hana fair play kwenye salarly payment ni kazi bure kujipendekeza kwa jumuiya,unaiba huku unatenda wema huku
 
Umuofia kwenu watanzania wenzangu!
Mimi sijui mtz. mwenye dhamiri njema awezaje kumlaumu MENGI? Hivi kafanya kosa gani kutoa zawadi hiyo kuwezesha watuhumiwa kukamatwa? Hivi hawa wanaomsakama mengi wanatumwa na nani? Kwa kosa gani? Nani mjasiriamali anayejituma km huyu? Watz. acheni wivu wa kikike (Msekwa, 2002)
Yaani anayemshutumu mengi atakuwa ni mmoja wa WAUaji wa albino kwa sababu wameona ni mpiganaji mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Mengi amesema atakayesaidia kukamatwa kwa waliomkata mkono Albino wa Tabora atamzawadia sh.10,000,000. Lakini pamoja na hayo, wengine wa mauaji ya hapo awali wamewahi kukamatwa na baadae kuachiwa licha ya kuwepo ushahidi wa kuthibitisha hilo.
Hao waliowatuma kukata mikono ya albino ni vigogo wa serikalini wanaotafuta madaraka.., sasa unategemea nini hapo.., BIG UP MENGI kwa kutupa matumaini...!
 
Tatizo lenu mnaishi katika mfumo wa kibepari lakini bado mnafikiri kijamaa.kama mfanyakazi anaona anacho lipwa hakilingani na huduma anayo toa aache kazi.hakuna anae lazimishwa kukaa pale.
Ni kweli kabisa Jerusalem kwa sababu mtu kama unaona mshahara ni mdogo ya nini uendelee kung'ang'ania kufanya kazi? Mimi nimewahi kufanya kazi kwenye kampuni moja kwa mda wa miaka miwili na ushee lakini mshahara ulikuwa hauridhishi ila tukatumia msemo wa mvumilivu hula mbivu lakini ilifikia hatua ya uzalendo kunishinda na kuacha kazi na kurudi nyumbani kufanya mambo yangu. Anayesema Mshahara ni mdogo kwa wafanyakazi wa MENGI hawajui walisemalo maana hakuna anayefungwa kwa kamba kuwa lazima afanye kazi hata kama malipo hayaridhishi.
 
Last edited by a moderator:
Hadi ukiona raia mmoja anatoa donge nono kukamatwa kwa watuumiwa basi ujue walinda usalama tulio nao wameshidwa kutekeleza majukumu yao. Inasikitisha sana vyombo vyetu vya usalama na serikali kwa ujumla kushidwa kufanya kazi yake ipasavyo kwenye kulinda amani na kulinda wananchi wake.
 
Mnafiki tu,watumishi wake wanaishi kwa shida nyingi mshahara mdogo,tukija kusikia mtumishi wake nae kaelekea huko kwa sababu ya shida sitashangaa, ni kampuni zake zinazoongoza kwa mishahara midogo,

Wabongo bwana,kwani selikali inalipa mishahara mikubwa? No free lunch jiongeze
 
kwa kweli hata mimi nimemsikia jana usiku nimefarijika sana kitendo alichokifanya ni cha kizalendo hata mimi ningekuwa na uwezo kama wa Mengi ningefanya hivyo. mungu abariki sana Bw. R. Mengi binaadamu tuwe na moyo wa huruma.
 
Kwa hiyo anatumia mfumo wa ubepari kufanya unyonyaji? Kama bosi hana fair play kwenye salarly payment ni kazi bure kujipendekeza kwa jumuiya,unaiba huku unatenda wema huku

ndio ubepari ulivyo namna yao ya kujitangaza ndivyo ilivyo!! lakini pia mtu hulazimishwi kufanyakazi kwa mtu au kampuni isiyo kulipa vizuri ukilinganisha huduma yako! seikalini kima cha chini ni 310000 kwa Mengi kima cha chini ni 400000!! yule kaondoka kwa mambo yake mengine.
 
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk.
Reginald Mengi, ameliomba Jeshi la
Polisi mkoani Tabora kuhakikisha
linawakamata na kuwafikisha
mahakamani wote waliohusika na
kukatwa kiwiko cha mkono mlemavu
wa ngozi (albino), Suzan Mungi (35)
na kutangaza dau la Sh. milioni 10
taslimu kwa mwananchi yeyote
atakayetoa taarifa zitakazosaidia
kukamatwa kwa watu hao.
Pia ameahidi kubeba jukumu la
kuwasomesha watoto wawili wa
Suzan, ambaye mumewe, Mapambo
Mashili, aliuawa kikatili kwa kupigwa
na kitu chenye ncha kali kifuani na
kichwani wakati akijaribu kumnusuru
mkewe (Suzan) asikatwe mkono wake
na watu hao katika tukio hilo.
Katika tukio hilo, watoto hao wawili
wameripotiwa pia kujeruhiwa na
kulazwa hospitali.
Dk. Mengi alisema hayo alipokutana
na viongozi wa Chama cha Albino
Tanzania (TAS), ofisini kwake, jijini
Dar es Salaam jana.
Alisema amefikia uamuzi huo
kutokana na kuguswa na uchungu wa
madhara yaliyowasibu albino na
wengine, ambao wamekuwa ama
wakikatwa viungo vya miili yao au
kuuawa kabisa kwa sababu ya
ulemavu wao.
“Ingekuwaje wewe ni mwanaume na
Suzan ni mkeo, au ni mtoto wao, au
mdogo wako au ni mtu wako wa
karibu? Ungejisikiaje? Niwaachie
Watanzania jibu la hilo swali.
Tunachukua hatua gani kuwalinda
watu hawa. Mtu hachagui, hakuzaliwa
wala hakuomba kuwa mlemavu.
Mungu hafanyi makosa katika kazi
yake,” alisema Dk. Mengi.
Aliongeza: “Uongozi wa Jeshi la
Polisi uchukue hatua za haraka hata
ikibidi nyumba kwa nyumba
wachukue hatua ili liwe fundisho kwa
wengine na tuonyeshe kuwa
tunawajali hawa wenzetu. Kama kuna
mganga amehusika achukuliwe hatua.
Kama kuna mtu anatafuta madaraka
achukuliewe hatua kali. Naliomba
Jeshi la Polisi Tabora wahusika
washikwe, wafikishwe mahakamani ili
anayehusika aonje machungu.
Aliyetumwa kukata mkono, mganga na
kila aliyehusika wote
washughulikiwe.”
Alisema yeye hana madaraka ya
kuchukua, hivyo atatoa mchango
wake kwa kumpa kiasi hicho cha
fedha mwananchi yeyote atakayetoa
taarifa zitakazosaidia kukamatwa kwa
wahusika na uhalifu huo, ikiwa ni
pamoja na kuwasomesha watoto hao.
Naye Katibu Mkuu wa TAS, Ziada
Nsemo, alimshukuru Dk. Mengi
akisema ni mtu wa kwanza nchini
kuguswa moyoni na kujitokeza
hadharani kukemea vitendo vya
ukatili vinavyofanywa dhidi ya albino.



CHANZO: NIPASHE
 
Mengi unamengi ya kuwasaidia hawa ndugu zetu,Mungu akuzidishie upendo huo..
 
Back
Top Bottom