Ndallo
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 7,619
- 4,292
Waziri wa ujenzi, Dr John Pombe Magufuli leo anatarajiwa kuwaweka kitimoto baadhi ya watendaji wake walioidhinisha nyumba 59 zilipiwe fidia ili kupisha upanuzi wa barabara mbalimbali za katikati ya jiji la Dar es Salaam wakati nyumba hizo hazipo. Hatua hiyo inakuja baada ya Dr. Magufuli kubaini kuwepo kwa nyumba hewa zilizopendekezwa kuwa zinapaswa kulipiwa fidia. Waziri huyo amesema mhandisi yeyote atakaye kuwa amehusika na malipo hayo hewa atafukuzwa kazi na kufungwa kwakua atakua amevunja sheria. Hii imetulia.