Dr. Magufuli "a man with no vision"

Dr. Magufuli "a man with no vision"

DATAZ

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2012
Posts
4,712
Reaction score
11,982
Maneno ya Mwalimu Nyerere (RIP) kwamba
"Watanzania wanataka mabadiliko",
yanathibitika sana kipindi hiki cha uchaguzi huu pengine kuliko uchaguzi mwingine mwingine wowote uliowahi kufanyika katika Nchi yetu.

Kwa maoni yangu mabadiliko ya kwanza huanzia kwa msimamizi anaetarajiwa kubeba mabadiliko hayo ambae ni Mgombea wa uraisi.

Raisi mtarajiwa ni lazima awe na maono, awe na vision na mission, awe independent thinker and dependable leader, hizi ni baadhi.

Lakini kwa Magufuli sizioni sifa hizi.

KWANINI;
Mheshimiwa huyu hadi leo hana vision yake yeye kama yeye ambayo tungeisikia na kui-vision katika kauli mbiu yake, (Ilani ya chama ni baadae).

Sana utamsikia,
"sitaawangusha ndugu zangu" NA "alimselema, alimselema.....".

Sifahamu hao "ndugu zangu" ni kina nani na hatawaangusha kwa lipi, na hiyo alimselema inatupeleka wapi?

Lakini pili, Magufuli hakuwahi kuwa chaguo la Kikwete katika Uraisi. Chaguo la Kikwete alikuwa ni Bernard Membe (Mdogo wake). Magufuli ilikuwa ni "BASI TU, HAKUNA NAMNA" Kwa maana hiyo na kwa kitendo cha Magufuli kutokuwa na campaign team na strategies na kumtegemea sana Kikwete kumtembeza kwenye kwenye hafla mbalimbali ili kumnadi, hakuashirii future nzuri kwa safari yake.

Ikumbukwe kuwa sio tu CCM imechokwa bali Hata Kikwete kachokwa vile vile.

Sasa huyu aliyechokwa ndiyo amnadi mbadala wake halafu utarajie ushindi wa kishindo!
Labda kwa "bao la mkono".

In short, Magufuli hakujiandaa kwa hili "Zali la Mentali".

He has to be quick in re-adjusting himself accordingly.
 
msimchokoze magufuri katulia mtoto wa watu hana makuu ukitaka kujua ana vision n mission kawaulize idara alizo simamia
 
mabadiliko hayawezi kutoka ccm ata wakiweka malaika
 
Well said mkuu,hata mm mwanzo nilizani ni mpiga drums wa TOT,anaishia kupiga ngoma hana Sera anaongozwa kila kitu na kkwete
 
hajui kuzifafanua sera za kijamaa wala kibepari,tangu awe mwana ccm sijawahi kumsikia akiongelea chochote kuhusu TANU,ASP,inawezekana hajui hata mapinduzi ya zanzibar yalitokeaje,hajui karume alifariki lini, hajawahi kushiriki mdahalo wowote wa kijamii iwe ndani au nje ya nchi ili watu wajue msimamo wake kijamii,kisiasa na kiuchumi,amekazana kusema hatatuangusha utafikiri yeye ni mcheza mieleka
 
msimchokoze magufuri katulia mtoto wa watu hana makuu ukitaka kujua ana vision n mission kawaulize idara alizo simamia

Halafu jamaa muongeaji kuliko mamvi kilakitu pesa watakuja kuwekwa kitimoto iwe aibu
 
Magufuli hawezi kuleta/kuweka foundation ya mabadiliko yanayohitajika sasa hivi tanzania, ukianza na katiba mpya na refo za sekta mbali mbali, maana hana vision(picha yake) kichwani atafanya nini..!? Na hii kuanza kucheka cheka na kupiga ngoma inamuharibia kabisa.. Lowasa yeye anavision hasa kuleta uwajibikaji kwenye serekali na taasisi na kupambana na umaskini(ambao anasema anauchukia)..
 
Magufuli hawezi kuleta/kuweka foundation ya mabadiliko yanayohitajika sasa hivi tanzania, ukianza na katiba mpya na refo za sekta mbali mbali, maana hana vision(picha yake) kichwani atafanya nini..!? Na hii kuanza kucheka cheka na kupiga ngoma inamuharibia kabisa.. Lowasa yeye anavision hasa kuleta uwajibikaji kwenye serekali na taasisi na kupambana na umaskini(ambao anasema anauchukia)..
Mgombea anazingatia ilani ya chama kazi yake ni kuisimamia siyo porojo kama ya lowasa.
 
ivi nyie mnaoongelea vision, mmejuaje magufuli hana vision!!
mnamsemea kama nani.?
nchi haiwez kuongozwa na vision ya mtu mmoja ata siku moja. nchi itaendeshwa na vision ya Ilani!
Ilani inasaidia sana kiongozi asiiweke nchi rehani au kufanya anachotaka yeyetu bila kupima impact kwenye jamii ya Tanzania.
je kiongoz akipata matatizo ya kisaikologia au akili, unafkili ataongoza tu nchi anavotaka!?
hilo haliwezekani.
hii nchi si ya raisi, kwamba ahamue anachotaka yeye,! raisi ni kiongozi tu na inabidi afate ilani ya kundi kubwa kuliko yote lililomchagua katika nafasi io ya uraisi. na ilo kundi ni chama cha siasa kitakachoshinda nafasi io.
 
Natamani Kuwe Na Presidential Debates...Hz Figisufigisu Sijui Hana Vision Ztajulikana Tu...By The Way 4days Remainng Kufikia Ile Siku Ya Hawa Tunaosema Mara Wengne Wagongjwa,hawana Vision Watueleze Waliyo Nayo Na Chama Chao....
 
Maneno ya Mwalimu Nyerere (RIP) kwamba
"Watanzania wanataka mabadiliko",
yanathibitika sana kipindi hiki cha uchaguzi huu pengine kuliko uchaguzi mwingine mwingine wowote uliowahi kufanyika katika Nchi yetu.

Kwa maoni yangu mabadiliko ya kwanza huanzia kwa msimamizi anaetarajiwa kubeba mabadiliko hayo ambae ni Mgombea wa uraisi.

Raisi mtarajiwa ni lazima awe na maono, awe na vision na mission, awe independent thinker and dependable leader, hizi ni baadhi.

Lakini kwa Magufuli sizioni sifa hizi.

KWANINI;
Mheshimiwa huyu hadi leo hana vision yake yeye kama yeye ambayo tungeisikia na kui-vision katika kauli mbiu yake, (Ilani ya chama ni baadae).

Sana utamsikia,
"sitaawangusha ndugu zangu" NA "alimselema, alimselema.....".

Sifahamu hao "ndugu zangu" ni kina nani na hatawaangusha kwa lipi, na hiyo alimselema inatupeleka wapi?

Lakini pili, Magufuli hakuwahi kuwa chaguo la Kikwete katika Uraisi. Chaguo la Kikwete alikuwa ni Bernard Membe (Mdogo wake). Magufuli ilikuwa ni "BASI TU, HAKUNA NAMNA" Kwa maana hiyo na kwa kitendo cha Magufuli kutokuwa na campaign team na strategies na kumtegemea sana Kikwete kumtembeza kwenye kwenye hafla mbalimbali ili kumnadi, hakuashirii future nzuri kwa safari yake.

Ikumbukwe kuwa sio tu CCM imechokwa bali Hata Kikwete kachokwa vile vile.

Sasa huyu aliyechokwa ndiyo amnadi mbadala wake halafu utarajie ushindi wa kishindo!
Labda kwa "bao la mkono".

In short, Magufuli hakujiandaa kwa hili "Zali la Mentali".

He has to be quick in re-adjusting himself accordingly.

Unachoongea sizani kama.umetumia ubongo ama ni maneno ya team fisadi ndio yamekujaa na ya Tapeli Mbowe anaeudanganya umma kwa kuita mtu fisadi ila leo anamuita shujaa na wewe unakubali kwa kushangilia kwa vifijo na unaandamana MAGUFULI NDIO KIONGOZI PEKEE ALIEBAKI NA ATAKAEIKOMBOA TANZANIA
 
Back
Top Bottom