December 11, 2019
Dar-Es-Salaam, Tanzania
Mada : Sera pacha ya Maendeleo ya Watu na Maendeleo ya Vitu
Dr. Azaveli Lwaitama akizungumza na wazee wa CHADEMA ameainisha jinsi sera pacha ya Demokrasia na Maendeleo inavyoshika kasi ushawishi miongoni mwa watu-huru.
Sera hii pacha ina kwenda sawasawa na maono ya CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO ( CHADEMA) ambayo tangu kuasisiwa kwake mwaka 1992 imesisitiza maendeleo ya vitu yaendane na maendeleo shirikishi ya watu kupitia demokrasia.
Ambapo wananchi mmoja mmoja na kama vikundi hukubaliana kupitia ushawishi wa kidemokrasia maendeleo pacha ya vitu na maendeleo ya watu yanapatikana sawia.
Source: DARMPYA TV
Sera hii ya maendeleo na demokrasia ni tofauti na mtizamo wa chama kongwe ambacho awamu hii ya 5 imeamua kutosa mwananchi yaani watu wasipate maendeleo na wala hawatakiwi kuhoji vipi mnatuacha na kushikilia maendeleo ya vitu.
Chama kongwe CCM sasa kinaamini katika kuminya demokrasia, mawazo huru na ushirikishwaji watu ktk maamuzi ya mustakabali wa maisha yao.
Hapa ndipo penye tofauti kubwa kuelekea 2020 ambapo CHADEMA ina ushawishi mkubwa wa watu huru kupitia demokrasia kujiamulia maendeleo ya vitu sambamba na maendeleo ya watu.
Huku CCM wao wameamua kuwapa kikundi kidogo kusingizia maendeleo ya vitu yataletwa kwa kuwanyima watu uhuru wao wa kidemokrasia huku wakiwanyima maendeleo ya watu kitu kinachopelekea umasikini na ugumu wa maisha kushika kasi nchini Tanzania.
Dar-Es-Salaam, Tanzania
Mada : Sera pacha ya Maendeleo ya Watu na Maendeleo ya Vitu
Dr. Azaveli Lwaitama akizungumza na wazee wa CHADEMA ameainisha jinsi sera pacha ya Demokrasia na Maendeleo inavyoshika kasi ushawishi miongoni mwa watu-huru.
Sera hii pacha ina kwenda sawasawa na maono ya CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO ( CHADEMA) ambayo tangu kuasisiwa kwake mwaka 1992 imesisitiza maendeleo ya vitu yaendane na maendeleo shirikishi ya watu kupitia demokrasia.
Ambapo wananchi mmoja mmoja na kama vikundi hukubaliana kupitia ushawishi wa kidemokrasia maendeleo pacha ya vitu na maendeleo ya watu yanapatikana sawia.
Source: DARMPYA TV
Sera hii ya maendeleo na demokrasia ni tofauti na mtizamo wa chama kongwe ambacho awamu hii ya 5 imeamua kutosa mwananchi yaani watu wasipate maendeleo na wala hawatakiwi kuhoji vipi mnatuacha na kushikilia maendeleo ya vitu.
Chama kongwe CCM sasa kinaamini katika kuminya demokrasia, mawazo huru na ushirikishwaji watu ktk maamuzi ya mustakabali wa maisha yao.
Hapa ndipo penye tofauti kubwa kuelekea 2020 ambapo CHADEMA ina ushawishi mkubwa wa watu huru kupitia demokrasia kujiamulia maendeleo ya vitu sambamba na maendeleo ya watu.
Huku CCM wao wameamua kuwapa kikundi kidogo kusingizia maendeleo ya vitu yataletwa kwa kuwanyima watu uhuru wao wa kidemokrasia huku wakiwanyima maendeleo ya watu kitu kinachopelekea umasikini na ugumu wa maisha kushika kasi nchini Tanzania.