Le Grand Alexei
Senior Member
- Nov 9, 2011
- 116
- 83
Nimekuwa nikifuatilia nyendo na harakati za wabunge wawili vijana wa CCM kwa muda sasa tangu waingie kwenye Ubunge. Nimekuja kugundua kuwa wote hawa wanafanya vizuri sana kama wabunge, kwa kusimamia maslahi ya Taifa na ya Chama chao, mpaka hivi siku za karibuni kufuatia msimamo wao kwenye posho walikaribia kufukuzwa uanachama wa CCM na kwa maana hiyo kuvuliwa Ubunge.
Kwa maoni yako hivi ni nani yuko juu zaidi ya mwenzake kwa misimamo? Hivi kuna fununu kwamba January Makamba yuko kwa ENL na Dr, Hamisi Kigwangalla yuko kwa Membe, je ni kweli?
Na pia ni kweli wanaandaliwa kuja kushika madaraka makubwa endapo makundi yao hayo yatashinda na kuingia Ikulu? Na pengine ndiyo maana wamekuwa wakishambuliana sana kwenye mitandao ya kijamii? January Makamba alikuwa Clouds FM kwenye Jahazi akielezea kuhusu Hoja yake ya nyumba, na Kigwangalla naye akasikika wiki hiyo hiyo Clouds FM kwenye Power Breakfast akiongelea Hoja yake Binafsi ya Kuhusu Ajira kwa Vijana.
Wadau mtujuze kuna lolote hapa kati ya hawa vijana chipukizi na machachari kutoka CCM???
Kwa maoni yako hivi ni nani yuko juu zaidi ya mwenzake kwa misimamo? Hivi kuna fununu kwamba January Makamba yuko kwa ENL na Dr, Hamisi Kigwangalla yuko kwa Membe, je ni kweli?
Na pia ni kweli wanaandaliwa kuja kushika madaraka makubwa endapo makundi yao hayo yatashinda na kuingia Ikulu? Na pengine ndiyo maana wamekuwa wakishambuliana sana kwenye mitandao ya kijamii? January Makamba alikuwa Clouds FM kwenye Jahazi akielezea kuhusu Hoja yake ya nyumba, na Kigwangalla naye akasikika wiki hiyo hiyo Clouds FM kwenye Power Breakfast akiongelea Hoja yake Binafsi ya Kuhusu Ajira kwa Vijana.
Wadau mtujuze kuna lolote hapa kati ya hawa vijana chipukizi na machachari kutoka CCM???