Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Mgombea urais kupitia Chama cha NLD, Doyo Hassan Doyo ameahidi kuwa endapo wananchi watampa ridhaa ya kuongoza Taifa, atapitia upya mikataba ya uwekezaji katika sekta ya madini nchini ili kuhakikisha kila Mtanzania ananufaika na uwepo wa rasilimali za madini.
Amesema mchakato huo utafanyika ndani ya miaka mitano ya uendeshaji wa nchi kwani ni mchakato unaohusisha masuala ya sheria, ukilenga kuondoa changamoto ya ajira kwa kutanua fursa ambazo hazipo kwa ajili ya watu kupata cha kufanya.
Doyo ametoa ahadi hiyo leo Oktoba 13, 2025 katika Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga kwenye mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya kituo cha mabasi CDT.
Amesema mchakato huo utafanyika ndani ya miaka mitano ya uendeshaji wa nchi kwani ni mchakato unaohusisha masuala ya sheria, ukilenga kuondoa changamoto ya ajira kwa kutanua fursa ambazo hazipo kwa ajili ya watu kupata cha kufanya.
Doyo ametoa ahadi hiyo leo Oktoba 13, 2025 katika Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga kwenye mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya kituo cha mabasi CDT.