everybody
JF-Expert Member
- Oct 30, 2010
- 337
- 103
Kuna kitu kimoja naona kinakosekana katika huu mjadala wa DOWANS. Kamati ya Mwakyembe ilishasema kuwa mkataba na DOWANS ni feki. Sasa hii kamati ya nishati inavyokutana kujadili jinsi ya kuirudisha na kuipa mkataba mpya DOWANS mbona haiongelei kabisa matokeo ya kamati ya Mwakyembe? Nafikiri kama kuna uamuzi wa kuipa mkataba mpya inabidi bunge na CCM wakubaliane kwamba utafiti uliofanywa na kina Mwakyembe haukutoa matokeo yenye ukweli. La sivyo, kujadiliana na DOWANS ni sawa na kujadiliana na mwizi aliyekuibia ili umpe mali zako akuchungie.
Kwa kifupi naona kama bunge, CCM na kamati ya nishati wanajichanganya na mwisho wa siku wananchi tutakosa imani na kamati zinazoundwa na bunge kwa sababu matokeo yake yatakuwa hayana umuhimu na ni upotevu wa hela bure. Kama wanataka kuiwasha hiyo mitambo labda wachukue wazo la Mnyika la kuitaifisha, na watuhakikishie wananchi kwamba hakuna hela itakayolipwa kwa DOWANS kutokana na kuwashwa kwa mitambo hiyo. Otherwise watueleze wazi kuwa uchambuzi/utafiti uliofanywa na kamati ya Mwakyembe haukuwa makini.
Naona kuna umuhimu wa kamati ya Mwakyembe kuhusishwa katika kila mjadala au hatua inayochukuliwa kuhusiana na DOWANS.
Ni mtazamo tu.
Kwa kifupi naona kama bunge, CCM na kamati ya nishati wanajichanganya na mwisho wa siku wananchi tutakosa imani na kamati zinazoundwa na bunge kwa sababu matokeo yake yatakuwa hayana umuhimu na ni upotevu wa hela bure. Kama wanataka kuiwasha hiyo mitambo labda wachukue wazo la Mnyika la kuitaifisha, na watuhakikishie wananchi kwamba hakuna hela itakayolipwa kwa DOWANS kutokana na kuwashwa kwa mitambo hiyo. Otherwise watueleze wazi kuwa uchambuzi/utafiti uliofanywa na kamati ya Mwakyembe haukuwa makini.
Naona kuna umuhimu wa kamati ya Mwakyembe kuhusishwa katika kila mjadala au hatua inayochukuliwa kuhusiana na DOWANS.
Ni mtazamo tu.