Dovutwa amshambulia Dk. Slaa

Jamani na mimi namshutumu sana Dk Slaa!!! kwa kuwachochea hata wasina warembo kama wale watoto wa Wassira kuichukia CCM....!! Namchukia sana...

0744 010101 Mpesa yangu
 
Hiyo ndio staili kutokea hapa mjini kwa wanasiasa wenye vyama vyao wasio na hoja. Nape Nnauye alipotaka kugombea uenyekiti UVCCM aliibuka na Lowasa kaauza nyumba ya uvccm.
Inaelekea bila kumtaja Dr Slaa single haiuzi,mambo ya nitokeje!

Mimi wala nilikuwa sijui "mdudu" unaoitwa Dovutwa,nilidhani ni kifupisho cha taasisi or something nilipoiona heading.Sasa kamtaja Slaa tumemjuwa wale tusiokuwa tukimfahamu.
 
Hujui shughuli anayofanya? 2010 aliwithdraw jina lake kupigiwa kura akasema kura zake apewe JK. Hujajua bado shughuli aifanyayo?
Yaani hapo jibu liko wazi, shughuli yake kaajiriwa Lumumba, yupo kwenye payroll ya Nape!!
 
bazazi sana huyu, badala atoe suluhisho la matatizo yanayolikabili taifa, ikiwemo kuhimiza wananchi kudumisha Amani akasema tukimchagua atajenga kiwanda cha silaha! mpumbavu kweli huyu JUHA! Halafu kale kazee kasajili cha vyama kanabakia kutishia kufuta chama cha upinzani, badala waanze kwa kufuta hiki ki - NGO cha CCM ambacho by any means hakina tija yeyote ya kuwepo, na hakina mantiki yeyote katika ustawi wa jamii ya mwana wa nchi ya Tanzania.
Dovutwa kuna siku utakula maneno yako machafu. PERIOD!
 
Tuheshimu maoni yake. Kinachonishangaza ni jinsi ambavyo vyama vya upinzani havitaki kuchukua hii nchi. Chama tawala kinafanya kila njia ili wasiungane ili waendelee kupeta. Vyama 2 au 3 vingeungana chama tawala kingepata changamoto. Unganeni jamani kama kweli mnataka mabadiliko! Hata sisi wananchi wa kawaida tutawaoneni nyie viongozi kwamba mna upeo wa kutosha.
 


“Kauli ya Dk. Slaa inashangaza na imevitia doa vyama vya upinzani, hii inaonyesha kumbe Dk Slaa anaogopa na hataki CCM ianguke mwaka 2015, swali la kujiuliza huyu bwana anamfanyia kazi nani? Nilitarajia Dk Slaa angefurahia CCM kuanguka ili Chadema iingie Ikulu, lakini yeye anasikitika CCM inakufa.

“


MODS TULETEENI HUYU JAMAA HAPA JAMVINI KWA MAHOJIANO ZAIDI. KAULI YAKE INATOA MASWALI MENGI SANA KULIKO MAJIBU
1) Je yeye na chama chake yumo kwenye hivyo vyama vya upinzani vilivyotiwa doa na DR.SLAA?
2) Mbona yeye aliagiza kura zake 2010 apewe kikwete? kama alikuwa na nia ya kuiondoa CCM madarakani hilo sio doa?
3) ofisi ya chama chake cha upinzani ziko wapi?
4) kina wanachama wangapi?
5)Mbona kila mara amekuwa akiibuka na kauli tata dhidi ya CHADEMA na sio CCM?
mods nasisitiza mleteni aje ajibu haya maswali hapa!!!!
 
Jamaa huyu nae amejadiliwa leo atulie sasa alicho taka tayari tumekifanya!
 
Huyu tapeli anayetumiwa na CCM kuvuruga upinzani ana nini cha mno zaidi ya kufikiri kwa tumbo na kuliendekeza? Elimu wala udhu hana zaidi ya kujirahisi na kutumiwa kupata riziki yake hata kwa makombo ya mafisadi. Huyu hana tofauti na akina Mrema, Lipumba, Maalim Seif, Kaboro, Mbatia, Cheyo na nyemelezi wengine waliojazana kwenye vyama vya siasa wakivuruga upinzani kwa malipo machafu ya CCM.
 
Dovutwa hajielewei bado japokuwa na utu uzima wake.

Jinga kabisa hili lipinzani gan?
 
Hayo ni mawazo yake, he has a point, so aheshimiwe. WanaJF lets play mature! tusibeze hoja ya mtu....bali tujibu hoja point by point. just like I said we need to be serious thinkers ili tukipeleke chama mbele. sio kumponda mtu kwa kuwa tu humtaki bila hoja.... hoja iue hoja..basi. tafadhali tujibu hoja ya Dovutwa.... tusisemetu katumwa...that simple?
 
''Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Dovutwa alisema Dk. Slaa hakupaswa kutoa angalizo hilo, kwani kufanya hivyo kunaonyesha wazi kuwa kiongozi huyo si mpinzani wa kweli na pia lengo lake ni kutaka CCM iendelee kubaki madarakani''...........Nani mpinzani wa kweli kati yake na Dr.Slaa?Nani anayehitaji CCM iendelee kubaki madarakana kati ya dovutwa na DR.SLAA?Mwaka 2010 nani aliyejitoa na kutaka kura zake ziende CCM ingawa hakuwa na watu wa kumpigia kura?Jambo la muhimu aache kudakia hoja na asiuwaze Udiwani,Ubunge wala Uraisi level lake ni Uwenyekiti wa mtaa mwaka 2014.
 


"Dk. Slaa hana dhamira ya dhati ya kutaka CCM iondoke madarakani, kama yeye anaona kurudishwa NEC kwa akina Lowassa na Chenge ndiyo kifo cha CCM hakupaswa kusema hayo.

"Alipaswa kunyamaza ili waweze kuishughulikia CCM na mwisho wa siku Chadema ishinde uchaguzi iingie Ikulu, lakini kwa maneno hayo ni sawa na kuifungua macho CCM, hivi wakisimamisha mtu strong (anayekubalika) Chadema itapitia mlango gani kuingia Ikulu?.

Nilitarajia Dk Slaa angefurahia CCM kuanguka ili Chadema iingie Ikulu, lakini yeye anasikitika CCM inakufa.




Huyu Dovutwa akili yake ya kisiasa fupi sana, hastahili hata kuitwa mwanasiasa. Yeye anafikiri ushindi wa Chadema maana yake CCM ife? Sasa CCM ikifa na Chadema wakashinda unataka nani aje awe mpinzani wa Chadema ili kutoa changamoto za uwajibikaji kwa Chadema, hicho chama chako cha UPFD kisicho na sura wala mwili?

Watu wengine mna-bore sana mnaongea kama mmetoka kunywa tap tap iliyolala. Hivi unaweza kufikiria Obama kusema hadharani anakitakia chama cha Republicans kife ili Democrats washinde? Huu unaoongea hapa ni upunguwani wa kisiasa ambao hauvumiliki.

Kwa taarifa yako Slaa kaonyesha kuwa mzalendo wa kweli kwa kutaka CCM waamke. Utamu wa ushindi wa Yanga au Simba ni kuwa na mpinzani wa jadi mkali sio debwe debwe.
 
Wahenga walisema MTI WENYE MATUNDA HAUISHI KUTUPIWA MAWE NA MWAMBA WENYE MADINI NDIO HUCHORONGWA. SIO SIRI DR. SLAA NI KIONGOZI ANAYETAKIWA KULIONGOZA TAIFA HILI KWA MIAKA KUMI IJAYO.
 
Hujui shughuli anayofanya? 2010 aliwithdraw jina lake kupigiwa kura akasema kura zake apewe JK. Hujajua bado shughuli aifanyayo?

Hebu nijuzeni makomredi wenzangu. Hivi Tovutwa ndiye mnyama gani vile?. Hivi nchi hii tumefikia kiwango cha kuwa na chama kinachoongozwa na mbayuwayu kama huyu na eti akapata wanachama wa kuwezecha chama kisajiliwe?. Mara nyingi nachanganyikiwa na uelewa wetu Wabongo.
 
Davutwa ! malayaa Mujarabu wa Siasa ! hahahaaah , Mtu ambae hata mamake Mzazi hajui chama anachoongoza . . . .

Takataka huyu , tupa kule

tuvyama twingine bwana! sasa huyu nae kawaza wapi atokee kaona hapo ndio mahali muafaka.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom