Dovutwa amshambulia Dk. Slaa

Hivi yulle kiongozi wa chama cha upinzani aliyesema kura zake za urais uchaguzi 2010 apewe Kikwete ,alikuwa nani vile nimesahau .naomba umnikumbushe

Kumbe na wewe unamkumbuka mkuu, nilidhani umma umemsahau huyu mfia tumbo. Labda baada ya kuona Nape kamsahau kwenye payroll ya Lumumbalizing ndio anajifanya kukumbuka kuwa kuna upinzani Tanzania.

Yuko na mwenzake anaitwa Hashim Rungwe yeye ni mwenyekiti wa chama gani sijui (kati ya hivi vyama vya njaa) na yeye alijitahidi sana kuingia kwenye Payroll ya magamba sasa sijui walitolewa nje ndio wanatapatapa.

Kama wanaume kweli wajitokeze JF tuna maswali ya kuwauliza
 
Hivi huyu Davutwa anajitangaza kupitia Dr. Slaa... Ni mwanamke au dume huyu...?? Hiki chama kipo ..??

... Yaani aibuu tupu...
 
Akaombe kazi ya ulinzi ana faa kufungua geti.Anadhani akimsema walau dr atafahamika na kusikika
 

Oh nooo, this busy head of mine. Hata sikumtambua maana nilikuwa bize najiandaa na safari. Ndie yeye alikuja amevaa kiajabuajabu kama mnubi?

Kuna watu wana matatizo na hawajijui. Mkuu wewe una link na hawa watu, siku moja tuletee hapa jamvini tumpatie maswali mawili matatu ili tujiunge na chama chake.
 
Dovutwa kapata mahali pa kutokea.

Mhh! ama kweli CDM "moto mkali". Waliosemwa na Dr Slaa hawasemi ila wapambe kama DoVutwa anakuwa mkali kuliko MAGAMBA. Huku ni Kujifanya "MKATOLIKI" Kuliko Pope, au ni "Mwislamu" kumshinda Mufti??
 

mkuu aweda, hii ni strategy ya ccm kujibu hoja zinazotolewa na cdm kwa kutumia vyama dhaifu km hiki cha dovutwa na mkewe cuf(refer mkutano wao arusha juzi). dovutwa na kunukuu articles za katiba wapi na wapi! km ulivyosema katengenezewa ili nao atoke.
 
Hivi yulle kiongozi wa chama cha upinzani aliyesema kura zake za urais uchaguzi 2010 apewe Kikwete ,alikuwa nani vile nimesahau .naomba umnikumbushe
Ndiyo huyo huyo Dovutwa, baada ya yeye kuenguliwa kugombea urais kutokana na kujaza vibaya fomu yake, aliwasihi wapiga kura wake, wampigie Kikwete!! Kama Tendwa angekuwa serious na kazi yake, hiko ndiyo chama kilipaswa kufutwa na siyo Chadema, ambayo imeingia mioyoni mwa mamilioni ya wa-TZ, na ambayo ndiyo tegemeo pekee la wa-TZ kwa sasa. Hiko chama cha Dovutwa ni kama ka-NGO fulani ka Dovutwa, kwa sababu yeye ndiye everything, mweka hazina, mwenyekiti na pia Katibu. Sasa haieleweki katika mazingira gani chama hicho kinaachwa kuwepo! Nadhani ni kwa matakwa ya magamba, kupitia kwa kibaraka wao Tendwa. Hata hivyo kama magamba wanamlipa huyo jamaa ili aiponde CDM, wakitegemea CDM, itadhoofika, wanajidanganya. Wa-TZ sasa wana uelewa mkubwa wa kuchambua, mchele ni upi na pumba ni zipi!!!
 
Inaonekana singo ya chadema ndo inayouza kwa sasa!! Anayefuata naye aje tumsikilize.................
 
Huyu jamaa alinikuna sana kipindi kile cha uchaguzi alipodai eti akichagulia kua Raisi atajenga Kiwanda cha Silaha!
mwishoni akasema kura zake apewe kikwete si ndio huyu?
 
Kweli kabisa huyu ndiye aliye mpigia jk campaign

 
Dovutwa pole kwa kukerwa, nakushauri safari nyingine usiwe mwepesi wa ku-comment maana comment yako inaweka wazi utupu wa kichwa chako.
Kumbuka Dr, slaa hauzwi na makosa ya CCM tu bali anauzwa zaidi na mitazamo yake kwa nchi kiujumra, Maamuzi yake sahihi, Siasa zake na mengine yanayofanana na hayo ndio yanayompandisha bei
Pia kauli yake isingebadilisha uchaguzi uliokwisha wala maamuzi yaliyopitishwa na vikao vya CCM

Dovutwa nakushukuru kwani umenifumbua macho kwamba kumbe Dr. Slaa ndio kila kitu kwenye siasa za bongo, kila kukicha mnaumia Dr. Slaa kasemaje.

Kwa kukusaidia tu, kumbuka kwamba kutangaza weakness za mpinzani wako ni credits kwa wapigakura wako at the same time ni kuendeleza elimu ya demokrasia ambayo wewe na CCM wenzako meshindwa
 
Ameshapona kipindupindu??

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
ivi huyu dovutwa katokea wapi tena......... hafanyi kampeni kutangaza chama chake yeye anadandia hoja za watu.........kweli hivi ndio vile ccm b.......... yeye atoe hoja yake na sio kujipatia umaarufu kupitia hoja ya slaa.........ebooo!!!
 
Dovutwa ana mapepo! Mpango wake wa kujenga kiwanda cha silaha Temeke umefikia wapi?
 
mbona anafanana na wale wakimbiza mwenge wa JAKAYA?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…