Yaani umechukia mzee mpaka kifaransa kinapanda chenyewe!Nikiwa kama mpigania haki za mamilioni ya wanyonge tanzania ninalaani kitendo cha serikali ya magufuri kuwawajibisha wanyonge na maskini kisha kuwaacha ama kuwaonya matajiri na vigogo wa chama na serikali.
Serikali ilitoa siku 7 kwa hoteli ya flomi iliyopo morogoro iliyojengwa kwenye pipe line ya bomba la mafuta TAZAMA ibomolewe lakini leo ni siku ya 30 haijabomolewa,
Nyumba ya mbunge mstaafu wa ccm mchungaji mama rwakatale iliyocholwa X juzi ili ibomolewe leo hii imetolewa sababu kuwa nyumba hiyo haiwezi kubomolewa kwa kuwa ina makosa madogo tu
lakini kuna hotel na nyumba za kifahari kibao ambazo zilipaswa kubomolewa lakini zimeachwa na zingine zitabomolewa fence na gate tu.
lakini sio hivyo tu matajili waliokwepa kodi mabilioni ya kodi bandalini wanapewa muda wakalipe kodi kwa kuombwa bila kuchukuliwa hatua lakini maskini waliokwepa kodi za elfu 70 mpaka laki wanapelekwa kisutu na kufungiwa biashara zao this is the exploitation of government ni serikali gani ya kibaguzi hii?
haiwezekani maskini wanaokula chakula kwa kubahatisha wakabomolewa makazi yao halafu matajili wakapewa muda hakika huyu magufuri sitaondoka hapa duniani bila kumbuluza mahakamani siwezi kuona sheria zinafanya kazi kwa maskini matajiri zinawaacha nchi hii ni yetu sote kwa nini tubaguane?
tunataka kuona nyumba ya rwakatale inabomolewa tunataka kuona mahotel yanabomolewa Je ne peux pas supporter de voir la folie est effectuée par le gouvernement.
By Mdude Chadema (Facebook)
Maelezo mengi ya nini.. kama nyumba za walala hoi zinabomolewa na za matajiri zibomolewe.. kwa kasi ile ileMtayaona mengi tu ya namna hii.... Magufuli ni binadamu tu km mimi na wewe.... amelelewa na mzazi km mzazi wako, amesoma shule ulizosoma wewe, km ulienda UD basi ulikuwa unishana na ye zile coridors za chuoni pale, naye yawezekana alishagomaga km wewe ulivyogoma, alishashika chaki akifundisha kemia na hesabu km waalimu wako waliokufundisha, akainigi chama kile ukipendacho au ukichiacho km wewe, amehonga kidogo wale wananchi wake kule chato kwa kanga, kofia na t shirt km wabunge wengine wa CCM, na mengine mengi tu yanayofanana na hayo.... hata akiwa waziri wa ujenzi kuna barabara zilizojengwa chini ya kiwango leo zina potholes km zingine pia..l
Tofauti ni kuwa leo yeye ni RAIS.... chini yake kuna watendaji amewaweka ambao ni binadamu km wewe pia, wana ndugu, jamaa na marafiki na wengine ni hao wenye nyumba na hoteli hizo unazolalamikia... nao wataenda kuzungumza na baadhi na kusikitika kuwa wanabomoloewa km hao masikini, tofauti ni kuwa wao watasikilizwa na hakuna atakayesikiliza kilio cha masikini, kwanza ni km zinaenda na maji km machozi ya samaki vile....
So kuna mambo utayashangaa mpaka siku unakufa ila ujue haki inatendekaga Mbinguni tu... pale ambapo huwezi honga wala kujitetea tetea... huku chini ya juu no fairness... lijue hilo hutakufa kwa presha bure!!!!