DOUBLE IMPACT(Lowassa na Sumaye) yaivuruga kabisa CCM

DOUBLE IMPACT(Lowassa na Sumaye) yaivuruga kabisa CCM

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
12,151
Reaction score
44,071
UKAWA wameanza kampeni za urais rasmi huku Mawaziri wakuu wawili wa zamani walihama CCM na kujiunga na UKAWA, Edward Lowassa na Fredrick Sumaye wakipiga kampeni kwa pamoja katika jiji la Dar siku ya jana na kuendelea hivyo hivyo katika mkoa wa Iringa kwa siku ya Leo.
Mtindo huo wa kampeni uliopewa jina la "Double Impact" umepelekea kuvuruga kabisa kampeni za CCM na kujikuta wakiacha kunadi sera zao na kubakia kukachifu na kumwaga matusi ya nguoni.

Kwa mfano, siku ya leo katika kampeni za mgombea urais wa CCM huko mkoani Njombe, ilibidi apandishwe jukwaani Amon Mpanjo (Kada wa CCM, mwenye ulemavu wa macho) ili kutumika katika kujibu hoja za Sumaye na Lowassa walizozitoa jana Jangwani. Baadhi ya viongozi wa CCM wa mkoa wamekosoa tabia ya baadhi ya makada wa CCM kudandia majukwaa na kuropoka kwani inaharibu mwelekeo mzima wa hotuba ya mgombea wao wa urais, wabunge na madiwani kwa kuwa unafanya wasahau kunadi sera na ilani ya uchaguzi ya CCM mwaka huu.

Inadaiwa kuwa CCM wako mbioni kufanya kikao cha dharula ili kufanya mabadiliko katika timu ya kampeni ya Magufuli ikiwemo kuongeza baadhi ya makada wenye ushawishi zaidi. Kuna taarifa zinasema Benjamini Mkapa na Pinda wameombwa kuongozana na Magufuli katika baadhi ya mikoa ili kuongeza nguvu.
 
Wamechanganyikiwa.

Lodilofa ataharibu kabisa kwani amekashfu watanzania majuzi.

Lowassa Rais hakuna namna tena
 
Hakika hotuba ya Jana ya Sumaye ilikuwa bora sana Kwangu binafsi Jana ndio nimeona uwezo wa Sumaye
 
Na bado, huo ni moto wa mabua lakini utaunguza nyumba.
 
Labda kwao wanapotoka lakini huo ulaghai unamuda wake. Timu ilishaundwa sasa watu wanashambulia
 
Hakika hotuba ya Jana ya Sumaye ilikuwa bora sana Kwangu binafsi Jana ndio nimeona uwezo wa Sumaye

Hata Mimi mkuu. Sikuamini kabisa kama jamaa Ni jembe namna hii. Mungu awape uzima mrefu na afya njema wakati huu wa Campaign
 
Lowasa baada ya kusoma bango lililoandukwa "mashekhe wa zanzibar vp mheshimiwaaa" Lowassa alijibu tutalishughulikia tukiingia.... sasa huyo mponchi anasema Lowassa kasema atawatoa!!
 
hakuna kulala mpaka kieleweke..... nnimeipenda hiyo double impact
 
Watanzania mnafanywa mazuzu alafu mnachukulia poa.EPA ilipgwa wakati wa utawala wa Sumaye,Uuzwajı wa nyumba za serikali na mashirika ya umma kwa hasara ni utawala wa Sumaye,ESCROW/IPTL dili ilifanyika wakati wa Sumaye.Rada,Kiwira ni Sumaye.Leo mnashanglia hilo jambazi??
 
Back
Top Bottom