Don't travel with wrong patners, it's too expensive

Don't travel with wrong patners, it's too expensive

Wakati nasoma hii story kuna melody nilikua naisikiliza nimejikuta nimemsikitikia huyo kaka

Umejitahidi kusimulia maana nilikua utadhani naangalia movie,nimependa your advise pia.

Back to topic mapenzi ya chuo mengi yao ni kusaidiana kukua tu hakuna la maan

Hii story ni cut & paste ya kilichonitokea, ukiondoa minor edits za UDsm na Mlimani City na kwingineko. Tofauti ni settings tu. Masomo na malavidavi havichangamani kabisa. Nawashukuru sana marafiki zangu walionisaidia ushauri nasaha mpaka nikamaliza bila kukamatwa masomo, na sasa nadunda mzigo.
 
duu pole zake,nishaona pia kwa marafiki zangu kadhaa, nilichojifunza kutokana na matukio ya namna hii ni kuwa gals always ukishaanza process znazoonesha kuwa uko serious na yeye mfano kumtambulisha om basi anaanza kuibua makuu,cjui ndo wanakua wanamaliziamalizia kula ujana! Kuna mwingine naye alikua na beib wake mpk kwao kamtambulisha ila wakakosana kdg tu m.mke katafuta mchepuko akaishia kupata mimba kumbuka jamaa alikua anampenda mpk ashawah kunywa sum wakati wa magomvi yao. Wakaja kusameana lkn dem tayar alikua na kiumbe cha mtu tumbon na jamaaa hakuambia ukizingatia walikua wanasoma vyuo tofauti..kwa upande wngu my gal mpk kuja kutambulishwa wakti tbs imehusikaa sana otherwise..cjui
 
Honey inabidi unifunge alarm ukiniita tu nikurupuke kuja maana naona napitwa tu, wewe huoni saivi ndo nakurupuka mwenzio
Mmmh unakosaje utamu sasa, na we usilale sana bhana
Haya nenda kwenye ule Uzi wa mtu ambae Araki mwenyemimba yake apeweushirikiano humu
 
Nilijifunza kutoka kwa m1 wa marafiki zangu wa karibu, i would like to share the lesson.
Akiwa 4th yr (finalist) pale CoET, huyu jamaa alikua very smart darasani, he knew playing the cards both hearts, spades and diamonds were on his hands. Tangu awali jamaa alikua anafanya vzr, siri kubwa ya mafanikio yake ni kutochanganya mapenzi na masomo.
Now that he knew time ain't his friend, jamaa aliamua atafute mpnz ambaye ndiye angeweza kuwa mwenza wa maisha yake. Basi huyu jamaa akapata binti wa 1st year pale UDBS, yule dada alikua mrembo wa sura+umbo, mwenye mvuto, mpole sana, mkarimu,heshima sifa zote zake. Tofauti na mabinti wengine hakuwa na papara, vituko, she was 1 of a kind. Hata sisi marafiki wa jamaa tulikua tunatamani kupata kifaa kilichokamilika kama kile....

Basi, semester ya kwanza ikaisha, kukawa na likizo ya mwezi m1. Mapenzi yameshika hatamu, yamewakolea vilivyo. Kwakua binti kwao ni Mwanza na jamaa kwao ni Geita, basi huyu jamaa alitumia ukaribu huo kujuana na familia ya binti, nae binti alipata kutambulishwa ukweni. Wazazi wa jamaa walifurahi sana kijana wao kupata mke mwema.
Chuo kikafunguliwa, penzi lilizidi kuchanua.

Lkn cha kushangaza yule dada akaanza kubadilika, nidhamu ikaanza kushuka taratibu, akaanza kuvaa nguo zisizo na maadili. Akawa na marafiki ambao kwakweli hawakua wa type yake kama tunavyomfahamu. Mapenzi yao yakaanza kupungua kwa kasi, jamaa alijitahidi sana kusecure their intimacy, na kweli alifanikiwa. Yule dada akarudi tena kwenye hali yake ya kawaida. Lkn kuhusu lifestyle na aina ya marafiki jamaa hakuconsider sana.

Basi penzi lao likawa la kusua sua na mashaka sana. Siku 1 nikiwa na marafiki zangu wengine, mida kama ya saa5 usiku, tukiwa Daruso tunacheki UEFA, tulimwona yule binti yupo na marafiki zake kama wa4 na w/me kama wa3 hivi, walikua wanapiga story kwa fujo sana, wakishushia na pombe za kila aina. Mwanzoni tulimwona yule binti akinywa Novida, lkn baada ya muda tukashangaa anakunywa pombe. Tuliamua tukae kimya tusimstue yule jamaa yetu kuepusha kuvunja mahusiano yao. Basi, ½ time ilivyofika yule binti aliongozana na marafiki zake na wale w/me kwenye Noah iliyokua imepaki pale nje,wakasepa... Hiki kitendo kilinikwaza sana, sikuweza kuficha ukweli, nikizingatia huyu jamaa alikua rafiki wa karibu sana.

Keshowe mida ya jioni, nilimwita huyu jamaa angu sehemu tulivu, tukawa tunapiga story za hapa na pale. Baadae nikaamua nimwambie ukweli wa mambo kuhusu binti yake, jamaa alikataa katu katu kuniamini, mbaya zaidi tulikua tumezoeshana matani na masihara. Nilimsisitizia kwa umakini sana kuhusu tabia ya mpenziwe, tulivyoachana alijaribu kuwauliza wale jamaa niliokuwa nao usiku ule pale Daruso, nao waliadmit the truth.

Basi keshowe jamaa alikutana na binti 'ake, wakaongea. Mwanzoni mwa maongezi yao yule binti alikataa kabisa kukubali, lkn at last aliconfess na akaahidi kubadilika, tena na machozi alitoa na kuapa kwamba kamwe hatarudia kile alichokifanya....

Vitimbi vingi viliendelea, kwakweli huyu dada alibadilika na kua mtu wa ajabu sana. Ule uzuri tuliokua tunauadmire wote uliisha, tulijitahidi kumshauri sana jamaa aachane na yule binti, lkn he never wanted to lose her.naeza sema Yule binti alikua bingwa wa kuomba msamaha, akiwa na kosa aliomba msamaha tena kwa machozi ya kujutia kosa. Basi jamaa alikua mwepesi wa kusehe+kusahau. Chakushangaza yule binti alikua anatulia then baada ya siku 2 anarudia kosa lile.

Kama kawaida ya w/funzi, baada ya kumaliza test hua ni kupata mapumziko kidogo, na kurefresh ubongo.
Nakumbuka ilikua jmosi, finale UCL chels vs bayern saa4 usiku, tulienda na jamaa na mafrendz wengine kucheki game pale Calabash. Game ilikua tamu sana, tulicheck mpk ikaisha, ilikua kama mida ya sa6 hivi. Sasa tulipanga tupite samaki² mara 1, then twende ambianse. Mmmh, tulipofika hapo samaki² tukakaa kidogo, kushtua tumbo. Very sad, doleful in deed, jamaa alishuhudia kwa macho yake, tukio ambalo nahisi halitafutika kichwani mwake.

Kwenye meza kama ya 3 kutoka pale kwetu, kulikua na mdada m1 na majamaa wa2, walikua wanapata chakula lkn kulikua na viti vi4 na sahani 4, baada ya kama ¼saa hivi ile siti ilipata mwenyewe, alikua ni m/ke. Kwasababu kulikua na mwanga hafifu sikuweza kumwangalia kwa umakini yule dada. Tuliagiza nyamachoma pale, tukawa tunaisubiri huku tukipiga story, ghafla yule jamaa akatunyamazisha ili askilize kitu, aliconcentrate kwenye maongezi ya wale washkaji wa meza yapembeni, nahisi aligundua sauti ya yule mpenzi wake, then akaamua kupiga simu ya mpenziwe ajithibitishie. Ah nikweli yule dada alikua ndiye, simu iliita na kukatwa. Jamaa alichanganyikiwa, alikosa ata cha kuongea japo hakusema alijikausha lkn mm niligundua kitu. Chakula kilikuja, jamaa alishindwa kula kabisa akisingizia kua tayari ameshiba. Baadae kidogo, wale jamaa kwenye hile meza wakawa wanajiandaa kusepa, wakalipa bill. Bahati mbaya/nzuri njia ya kutokea ilikua lazima wapite karibu na hile meza tuliyokuapo.

Jamaa alipoteza nguvu kabisa, chozii likawa linadondoka dropwise, yule demu wake akapita mbele yetu, tena nahisi alituona, akatupuuza kabisa tena akapita ameshikwa kimahaba. Jamaa hakuamini kbs macho yake, alipatwa na hasira kali lkn tulijitahidi kumtuliza. Since then, jamaa akawa very distressed

Jamaa hata kusoma alishindwa, amani ilikatika kabisa. Ilibidi agraduate huo mwaka lkn alikula sap 2, ambayo 1 ilizaa carry over. Kumbuka jamaa alikua bright sana, hbr ya sap kwake ni hadithi.


MY TAKE.
Always better to catch up, than to clean up the mess of a bad r/ship. The available person is not always the best person for us. It's hard to do, but run as much possible from a r/ship that will seriously do you harm in the future. Some come for a reason, some come for a season, others to stay and bring best or demon out of u. Be keen wen sorting out who we allow to stay in our hearts for a long ran, b'se it will make or mar the rest of your life.
Don't travel with wrong patner, it's too expensive.
Aisee umeandika vizuri sana hongera sana pia ulichoandika kilinikuta matukio ni hayohayo kweli Mungu wa ajabu,sasa hivi nimepona ila imenigharimu sana.
 
Hii story ni cut & paste ya kilichonitokea, ukiondoa minor edits za UDsm na Mlimani City na kwingineko. Tofauti ni settings tu. Masomo na malavidavi havichangamani kabisa. Nawashukuru sana marafiki zangu walionisaidia ushauri nasaha mpaka nikamaliza bila kukamatwa masomo, na sasa nadunda mzigo.

Pole aiseee
 
Aisee umeandika vizuri sana hongera sana pia ulichoandika kilinikuta matukio ni hayohayo kweli Mungu wa ajabu,sasa hivi nimepona ila imenigharimu sana.


Pole sana mkuu...

Lakini mkuu next time, ukiona thread ndefu usii-quote, unatutesa sisi watumia simu
 
Mi nacheka tuu hapa...manake nikikumbuka mikasa....kirambasi chake kikubwa
 
Back
Top Bottom