Wengi hapa hata hawajui kwa nini Ukraine anapata shida sana katika mapigano yaliyopo DONBAS mwanzo Ukraine ilitaka kugawanya waUkraine halisi na Pro-Russian ili iwe Rahisi kutnganish wasaliti wa kirusi na wale wanaounga mkono Ukraine kwenye eneo la DONBAS, watu walipoanza kuondoka kuelekea magharibi mwa Ukraine Russia akaharibu Reli ili kuzuia watu kuelekea maghabiri, na anajua fika kuwa Ukraine anahofu ya kuua watu wake.Hivyo inamuwia ngumu Ukraine.Pia kwenye hili eneo wasaliti wengi na pia Ukraine anapigana na watu wake ambao ni Pro-Russian kama ilivyokuwa kwa Georgia na Cremia.Huu ndio ugumu pia anao pata Moldova kwenye mkoa wa Transistria, ambako pia pro russians nao wanataka kujitenga kutoka Moldova kwenda Russia.katika mazingira haya si kazi nyepesi kushinda labda uamue kujibu kwa makombola bila kujali uhai wa watu.ikumbukwe kuwa Russia ameshapenyaza mamluki hadi katika majeshi ya nchi zenye watu wanaoongea kirusi hasa katika nchi za Moldova,Georgia,Beralus na Ukraine.