Donald Trump: Sidhani kama nitaenda Mbinguni

PAYE

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2025
Posts
424
Reaction score
567
Rais wa 47 wa Taifa la Marekani, Donald John Trump (79) ameeleza mashaka yake ya kuingia mbinguni ambapo amesema hana hakika kama kuna kitu kinachoweza kumfanya aingie mbinguni ila ana uhakika amesaidia maisha ya watu wengi.

Trump alisema hayo akijibu swali la mwandishi wa habari aliyemuuliza kuhusu ratiba yake ya kusali na jinsi itakavyomsaidia kuingia mbinguni ndipo Trump akasema;

"Unajua mimi sidhani kama kuna kitu chochote kitakachonipeleka mbinguni. Kweli, sidhani. Huenda mimi si mtu wa kwenda mbinguni. Labda niko mbinguni sasa hivi, tunaposafiri kwa ndege ya Air Force One. Sina uhakika kama nitaweza kwenda mbinguni, lakini nimefanya maisha ya watu wengi kuwa bora zaidi."

Amesema Trump baada ya kauli yake Wiki kadhaa zilizopita kudai kutaka kuimaliza Vita ya Ukraine kwani itamsaidia kwenda Mbinguni.

Your browser is not able to display this video.
 
Of coz kazi za mikono yako hazikupeleki mbinguni in Christianity.
 
Uhakika wetu unatokana na kumwamini Kristo
 
Hilo lipo wazi.....

Mfuasi wa Hiram Abiff mwenye daraja namba 33° anaanzaje kwenda mbinguni?
 
Hilo lipo wazi.....

Mfuasi wa Hiram Abiff mwenye daraja namba 33° anaanzaje kwenda mbinguni?
unataka kusema ni mwanachama wa skull and boner/illuminat/freemason na magenge mengine ya namna hiyo?
 
unataka kusema ni mwanachama wa skull and boner/illuminat/freemason na magenge mengine ya namna hiyo?
Hayo magenge bado hayashtui...

Ushawahi sikia Club/Society inaitwa Bohemian Grove? Sasa huko ndipo kwamoto zaidi, na ndipo ukienda unamkuta bwana trump akiwa siti za mbele.
 
"Labda Niko mbinguni Sasa hivi"
Huo ndiyo ukweli baba kula maisha, Duniani hapa ndiyo mbinguni na kuzimu ni Duniani hapa hapa
 
.
"Labda Niko mbinguni Sasa hivi"
Huo ndiyo ukweli baba kula maisha, Duniani hapa ndiyo mbinguni na kuzimu ni Duniani hapa hapa
Kama hakuna kufufuliwa kwanini kuna DNA 🧬 ambayo inabeba utambulisho wetu
 
.

Kama hakuna kufufuliwa kwanini kuna DNA 🧬 ambayo inabeba utambulisho wetu
Kwahiyo mkuu unaamini Kuna siku atakuja jamaa awafufue watu wote waliokufa 🤣
Ili iweje?
 
Ninaimani kuwa haki haipotei na nina Imani kuwa kuna Kumbukumbu za matukio zilizo hifadhiwa, kwa hiyo nachukulia DNA kama mbegu .
 
Kwani lazima kwenda mbinguni ambako hukuwekeza wala kuwa na chako? Ukishakufa, kazi kwisha. Unarudi kwenye nobodity/nonentity kama ulivyokuwa awali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…