Domo Kaya: Hukumu ni Kifo

“Nyanyuka upambane bwana Miguu ya kuku.” Kiongozi wa watekaji waliojinasibu kuwa ni maofisa wa jeshi la polisi, alimwambia huku akimwinua na kumpigisha magoti. Wengine walitengeneza duara na kumzunguka.

“Mr Miguu ya kuku, amka uruke kijogoojogoo..” Jamaa alimdhihaki huku akimshushia konde zito usoni mwake, Zuki hakutaka kulikwepa, aliacha lipige palipolengwa. Wale jamaa walianza kumshushia kipigo kwa kupeana zamu, kila aliyepiga alipochoka alimwachia mwenzake nae apige.

Kipigo chao kilimchakaza bwana Zuki Gadu, uso ulivimba na mdomoni alitoka damu nzito iliyochanganyikana na mate, jicho lake moja lilivimba na hakuweza kuona vizuri, masikio yake hayakusikia kwa ufanisi mkubwa, kila kiungo cha mwili wake kilikuwa hoi kwa maumivu.

Licha ya kupigwa sana lakini jambo moja alilokuwa na uhakika nalo ni kuwa, wale jamaa wasingeliweza kumuua na kulikuwa na kitu walihitaji kutoka kwake na ili kurahisisha mambo, aliamua kuwachokoza ili wamwadhibu na baada ya hapo aliamini wangelivuka hatua ya mwanzo waliokuwa wakimuuliza swali tata na kurukia hatua nyingine ambayo hakuwa akiijua. Hila zake zilifanikiwa kwa sababu aliitabiri vema tabia ya kiongozi wa wale watu, alionekana kuwa mjivuni na mtu ambae hakuwa na uzoefu na aina ya kazi kama zile za utekaji, alionekana ni mropokaji hovyo bila kujali alichoulizwa. Utabiri wake ukatimia pale aliposhushwa na kushushiwa kipigo hadi kuwa na hali mbaya, wakamchukua na kumhamishia kwenye nyumba nyingine safi kwa lengo la kumtibia majeraha aliyokuwa ameyapata. Wakati wakingoja tabibu afike kumsaidia mateka wao, maumivu yalimzidi uwezo na akapoteza fahamu. Zuki Gadu p.a.k Miguu ya kuku, hakufahamu kilichokuwa kikiendelea.

*******

3:
Zuki Gadu alipata fahamu baada ya saa zaidi ya sita kupita, akafumbua macho yake na kujipa utulivu wa dakika kadhaa ili kuziweka vema kumbukumbu zake. Dakika moja ilitosha kuzirejesha kumbukumbu za kilichotokea, kisha akazungusha kichwa chake taratibu na kukitazama chumba alichokuwepo. Hakupata chembe ya shaka kujua ya kwamba alikuwa kwenye chumba cha huduma ya kwanza, hakukuwa na vitu vingi zaidi ya kitanda kidogo alichokuwa amelala na meza iliyokuwa na boksi la vifaa vya huduma ya kwanza. Mwili wake haukuwa umefungwa na kitu chochote, majeraha yalikuwa wazi licha ya kunusa harufu kali ya dawa za kuondoa wadudu kwenye vidonda, jicho lake lilikuwa limepungua uvimbe kiasi aliweza kuona vizuri. Mikono na miguu yake ilikuwa imefungwa vema kwenye tendegu za kitanda, jaribio lolote la kujifungua lisingeliweza kuzaa matunda kwa namna walivyokuwa wamemfunga. Zuki hakutaka kujihangaisha kujinasua kwenye kamba alizofungwa, alitulia na kuruhusu ubongo wake ukabiliane na fikra tunduizi na moja ya maswali mengi yaliyopita kichwani mwake ni kuhusu kilichokuwa kipo nyuma ya tuhuma zilizokuwa zikimkabili swahiba wake, Dodi Danga.

“Namfahamu Dodi, hawezi kuua mtu, Dodi ni miongoni mwa watu wachache ambao hawakupenda kukurukakara na vyombo vya ulinzi na usalama.” Aliwaza huku akiwa kalala chali, macho yake yakitizama juu.

“Kuna kitu kipo nyuma na hicho ndicho kilichonileta huku ili kumsaidia, akipotea ina maana itanilazimu kutafuta mtu mwingine mwaminifu kama yeye aweze kusimamia mradi wa kulea watoto yatima na watu wenye mahitaji maalumu” Alizidi kuwaza huku ari ya kujinasua kwa mabazazi wale ikiongezeka.

“Aliye nyuma ya kutekwa kwangu ni nani? Ndiye aliyenyuma ya sakata la Dodi? Anapanga nini juu yetu?” Alijiuliza maswali mengi bila kupata majibu, wakati akiendelea kujiuliza, akakumbuka kitu kingine cha muhimu kwake.

“Yuko wapi Bob Rando? Yupo salama kweli?” Alipojiuliza kuhusu rafiki yake huyo, ile ari ya kujinasua ikaongezeka kwa sababu alihitaji majibu ya kila swali na hakukuwa na wa kumjibu kama angeliendelea kulala kitandani.

“Mimi si mgonjwa wa kulala kitandani, nahitaji majibu.” Alijiambia mwenyewe huku akipinda shingo yake kutizama kamba zilizokuwa zimifunga mikono yake, akataka kufanya jambo japokuwa hakujua kama atafanikiwa, lakini kabla ya kulitekeleza jambo hilo, pale ndani aliingia mtu, akaahirisha alichotaka kufanya na hesabu zake akazihamishia kwa yule mtu. Yule aliyeingia nae hakuwa na wema wala huruma, alikuwa na jambo lake zito kwa Zuki.

Chumba kikafukuta joto, joto la kifo na uhai.

Nani mshindi? Mimi sijui.


***********

Kwenye moja ya ofisi ndani ya gereza fulani ndani ya jiji la Dar, kulikuwa na ugeni. Ugeni wa mtu aliyejitambulisha ya kuwa ni mwanasheria wa kujitegemea kutoka moja ya kampuni za wanasheria hapa nchini. Mwanasheria yule hakuwa peke yake, alikuwa ameambatana na mwandishi wa habari kutoka moja ya vituo vikubwa vya habari nchini. Mwanasheria yule alikuwa anaelekea kuwazidi hoja maofisa wa jeshi la magereza kwa kile alichohitaji, hoja zake zilibeba uzito zaidi kwa kuwa pembeni yake alikuwepo mwanahabari ambae hakuwa na mipaka kwenye habari za aina ile kama wangeruhusu jambo lile ligeuzwe habari, iwe kwa kutaka ama kutokutaka na endapo habari jngelifika nje ya gereza, ajira zao zingelikuwa mashakani.

“Mimi naondoka, lakini tambueni ni kosa kisheria ofisa wa jeshi la magereza kuzuia mwanasheria kukutana na mteja wake ndani ya gereza, tena nikiwa nimefuata taratibu zote.” Mgeni aliwaambia maofisa waliokuwa kwenye ile ofisi huku akiwa amesimama.

“Aah siyo kama tumekuzuia ila tumepewa zuio la mtu yeyote kuonana na huyo mahabusu na…” Ofisa mmoja aliyekuwa na nyota moja begani alijaribu kutetea.

“Mimi namhitaji huyo mtu aliyetoa zuio la watu kuonana na Dodi Danga.” Mgeni alifoka.

“Itoshe kusema hatujapewa haturuhusiwi kuruhusu mtu yeyote kuonana na Dodi Danga.” Afande aliendelea kushikilia msimamo wake.

“Naomba nikuoneshe nguvu ya sheria.” Mgeni alisema huku akiinua simu yake na kuzitafuta namba fulani kisha akapiga.

“Unampigia nani ndugu.” Afande mwingine aliyokuwa kwenye chumba cha masijara aliuliza huku akimtizama yule mwenye nyota mbili ambae alikuwa haelewi lengo la Mgeni wao kupiga simu.

“Nampigia waziri wa utawala bora, kisha nitampigia waziri wa mambo ya ndani.. Au hamuamini?” Mgeni alisema huku akiwaonesha kioo cha simu yake.

“Hii namba bila shaka mnayo hapa ofisini kwenu.” Alisema huku akirejea kupiga baada ya muito wake kutopokelewa na mhusika.

“Nitamtajia namba zenu za kazi mlioko humu kwa sababu ni ninyi mlionizuia, huyo aliyewatuma endeleeni kulihifadhi jina lake.” Alizidi kupiga mikwara.

“Naomba usubiri kidogo ndugu Wakili msomi.” Ofisa mwenye nyota mbili alimwanbia mgeni wake huku akihangaika kuzungusha mkonga wa simu ya mezani. Sekunde chache baadae aliushusha chini na kumtazama mgeni wake.

“Ulisema unaitwa nani?” Alimuuliza mgeni.

“Wakili msomi, Rashidi Chota.” Mgeni alijitambulisha.

“Sawa bwana Rashidi Chota, nimeambiwa usitumie zaidi ya dakika kumi kuongea nae, lakini uende peke yako na huyu mwenzako abaki hapa.”

“Hapana!” Mwandishi alikataa kisha akasema..

“Ninakibali kutoka mamlaka husika kufanya mahojiano na Dodi Danga” Mwandishi alisema huku akiweka barua mezani, barua ambayo ilikuwa na mihuri mitatu kutoka ofisi alizotaja.

Ofisa alibaki kuduwaa na asijue achukue hatua gani, kukataa alitaka na kukubali alitaka. Mwishowe akaamua kurejea kumpigia aliyekuwa amempigia awali, alieleza shida yake kisha akasikiliza kidogo na kurejesha mkonga kwenye kitezo.

“Wote wawili mtaonana nae ila atatangulia bwana Rashidi Chota, kisha utaingia wewe.” Afande alisema, sekunde chache baadae alimuita ofisa mwingine mwenye cheo cha chini na kumpa maelekezo ya kuwapeleka wageni kwenye vyumba maalumu kwa ajili ya kukutana na mteja wao.

Wakati Wakili Rashidi Chota na Mwandishi Kumbi wakielekea kuonana na Dodi Danga, kwenye moja ya ofisi ya kiongozi wa ngazi za juu pale gerezani, kulikuwa na jambo linaendelea. Kiongozi huyo alikuwa ameshika simu yake akiwasiliana na mtu fulani.

“Sasa inakuwaje mtu anafika ngazi zote hizo ninyi hamfahamu?” Alimfokea aliyekuwa akizingumza nae.

“Unakataa nini wakati Mwandishi huyo yupo hapa na ni Mwandishi kutoka kituo cha taifa, unahisi amekosea gereza?... Au mnataka nifukuzwe kazi ili mnilipe ninyi?” Bwana jela aliendelea kumfokea mtu wa upande wa pili.

“Ooh, kwa hiyo unanitisha kisa kupokea muamala? Basi naurejesha na kesi ikifika nasema ulikosewa nikaurejesha.” Bwana Jela alitamba. Akakaa kimya sekunde chache kisha akashusha pumzi nyingi na kutabasamu.

“Eeh, mambo ndiyo hayo sasa. Picha zao nawatumieni sasa hivi.” Alisema na kukata simu kisha akainuka haraka Kwenye kiti chake na kuelekea kwenye ofisi fulani ambayo haikuwa mbali na ofisi yake. Huko aliingia na kuomba vijana waliokuwa wakifuatilia baadhi ya kamera za usalama pale gerezani, wawashe kamera za vyumba vya mazungumzo ya faragha.

“Mrekodi hizo picha zote na nazihitaji ofisini kwangu.” Aliwaamuru na bila kisubiri jibu lao, alitoka kwenye zile ofisi na kurejea ofisini kwake.

Wakati bwana jela alipokuwa akirejea ofisini kwake, Dodi Danga alikuwa akikaa kwenye kiti na kutazamana na mgeni wake.

“Pole sana bwana Dodi Danga.” Rashidi Chota alianzisha mazungumzo kwa sauti ya chini ili asisikilizwe na ofisa mmoja aliyekuwa ndani ya kile chumba akiimarisha ulinzi.

“Bob Rando…” Dodi alianza kuongea kwa sauti dhaifu huku akioneka kudhoofika kuliko kawaida.

“Hey, usiniite jina langu, hapa nimejitambulisha kwa jina la Rashidi Chota na nipo hapa kama mwanasheria wako.” Bob alimpasha mwenzake.

“Kwa nini umejihatarishia maisha namna hiyo? Hii kesi ina watu wenye nguvu sana nyuma yake.” Dodi Danga alisema huku akionekana kutopendezwa na uwepo wa Rashidi Chota wa bandia.

“Usijali kuhusu mimi, uwepo wangu hapa ni njia ya kusafisha ili wanasheria wa kweli waje kwenye hii kesi yako.” Bob alimwambia dhamira yake.

“Msiendelee kuhatarisha usalama wa wengine, hii namwachia Mungu.” Dodi alisema huku chozi likishuka.

“Acha uzwazwa bwana mdogo, Mungu anakazi nyingi sana za kufanya, usidhani yupo kushugulikia matatizo yako tu na kikubwa nikwambie, Mungu humalizia kazi iliyokwishaanzwa. Ukianza biashara, yeye hutia mkono wake ufanikiwe na kamwe hakuanzishii yeye. Hata wale waovu huwalipa kwa kile walichokianzisha, ndiyo sababu waovu huishia pabaya na wenye wema huishia pazuri, Mungu hilipa sawa na matendo yako.” Bob Rando p.a.k Rashidi Chota, alimpa somo dogo Dodi Danga ambae hakutia neno zaidi ya kukaa kimya.

“Nataka unipe mwanga wa sakata hili kwa haraka haraka.” Bob alimwambia.

“Nenda kwenye nyumba ya zamani ya Zuki iliyoko Tegeta, kwenye boksi la kuhifadhi namba za Luku, kuna ujumbe hapo.” Dodi alimpa maelekezo.

“Good..” Dodi alisema na kunyamaza kidogo kisha akaendelea.

“Kwa kuwa muda wangu nilihisi hautatosha kuongea na wewe, niliambatana na mtu mwingine ambae ungelihitajika kuongea nae kwa kirefu zaidi.”

“Yupo wapi mtu huyo?”

“Yupo kwenye foleni nje ya chumba hiki.. Lakini kwa kuwa kuna sehemu naweza kuanzia, naomba ukatae kuongea nae…”

“Una maanisha nini?”

“Namaanisha unayo haki ya kukataa kuongea na mgeni yeyote, tumia haki yako kumkataa.”

“Ni vipi kama hataukuta ujumbe huo, huoni kama utakuwa umekosa vyote?”

“Nikiukosa, atarejea tena” Dodi alisema huku akiinuka na kabla ya kupiga hatua nyingine, alimtazama Dodi kwa macho makavu.

“Nini!” Dodi alishangaa aina ya jicho lile, alijua kuna jambo.

“Una uhakika huhusiki na yaliyotokea?” Bob alimuuliza kwa sauti kavu tofauti na mwanzo.

“Hakika hakuna ninalojua.” Dodi alijibu.

“Basi usikae kinyonge. Ngoja tuuze roho hadi tununue wako” Bob alimwambia.

“Kuwa makini Bob!” Dodi alimuonya.

“Siitwi Bob, naitwa Rashidi Chota..” Bob alinyamaza kidogo kisha akasema,

“Miguu ya kuku kakanyaga ardhi hii. Vimba mwanangu.” Bob alitabasamu na kusukuma kiti nyuma kisha akapiga hatua kuelekea mlangoni, nyuma yake alisindikizwa na jicho la Dodi Danga aliyekuwa amejawa na furaha baada ya kusikia uwepo wa Zuki Gadu p.a.k Miguu ya kuku. Alijihisi mshindi japo hakujua ameshinda mtihani upi kati ya mingi iliyokuwa mbele yake.

“Ahsante Mungu.” Alisema huku akisimama, askari aliyekuwa kando alimfuata na kumpa taarifa ya uwepo wa mtu mwingine aliyehitaji kuonana nae.

“Nimechoka, sihitaji kuongea na mtu mwingine tena. Nirejeshe ninakotakiwa kuwa.” Alisema huku akisukuma kiti nyuma na kupata nafasi ya kurudi nyuma huku akiiacha meza ya mazungumzo ikiwa haina mtu. Askari hakuwa mbishi alielewa haki za mahabusu na wafungwa wake, moja ya haki hiyo ni kuheshimu maamuzi yao ambayo hayaingiliani na utendaji kazi wake. Alimsindikiza kurejea kwenye sero yake huku yule mgeni aliyekuwa akisuburi, aliishia kupewa taarifa na kutakiwa kurejea siku nyingine.

Nje ya gereza wageni wa Dodi Danga walipanga gari moja huku dereva akiwa ni Bob Rando. Waliondoka kwenye viunga vya gereza huku kazi yao ikiwa imefanikiwa kwa kiasi kikubwa, walipongezana wakati wakiendelea na safari yao.

“Ila wewe jamaa ni noma aisee!” Mwandishi alianza kuongea huku akimtizama mwanasheria bandia.

“Huamini kama mimi ni mwanasheria?” Bob alimuuliza huku akicheka kwa kebehi.

“Asiyekujua anaweza kuamini.. Ila umeuvaa uhusika pale ofisini hadi nikatamani kuachia cheko.” Mwandishi aliendeleza mjadala.

“Unashangaa uhusika wa dakika chache hizo, nimewahi kukaa Congo nikiwa mchungaji kwa zaidi ya miaka mitano, nikaaminika na uchungaji wangu, nikauza silaha nyingi kwa mgongo wa utumishi, mwisho wa siku nikapotea bila kuaga.” Bob alimpasha asiyoyajua huku akiangalia kioo cha upande wake, akaishia kuguna.

“Oya Kisu! Hebu kuwa makini na hiyo pikipiki nyuma ya hilo gari jeupe.” Bob alimwambia mwenzake huku yeye akiwa makini kutizama mbele, alihitaji kuwa na uhakika na kile alichokihisi kuhusu watu waliokuwa kwenye pikipiki. Kila alipokuwa akiongeza mwendo na wao waliongeza huku wakionekana kutokutaka kuipita gari iliyokuwa mbele yao.

“Huu ni mkia wa fisi, wapo na sisi.” Kisu alimwambia Bob.

“Twende tuwabwage hapo mataa.” Bob alisema huku akiipita gari moja iliyokuwa mbele yake kisha akaongeza mwendo zaidi na kuweka umbali fulani na ile pikipiki.

“Chukua hayo mafuta upake kioo cha mbele usawa wa mtu kupita.” Bob alimwelekeza mafuta yalipokuwa kwa kumnyooshea kidole, Kisu akayachukua na kufanya kama alivyoelekezwa.

“Chukua kilicho chako na ukikumbatie vizuri kabisa.” Bob aliendelea kumwelekeza Kisu ambae alitii maelekezo bila kuhoji.

Mita chache mbele kulikuwa na foleni ya magari baada ya taa nyekundu kuwaka kuashiria magari ya upande wao kusimama.

“Tunawabwaga hapa.” Dodi alisema huku akizima gari na kuweka mkono wake mmoja pale alipoelekeza kupakwe mafuta fulani ya kuvunja vioo, alisukuma kidogo na kioo kilitawanyika.

“Nenda zako, usipite mlangoni.” Bob alimwelekeza Kisu ambae kwa kasi alichomoka na kuwa juu ya boneti kisha akaruka na kutua mbele ya gari, Bob nae alifuata na kuliacha gari tupu.

“Tunyooshe mbele wale wajinga wasitune kama tumetoka.” Bob alimwambia mwenzake huku akianza kutembea kwa kasi kuelekea mbele, Kisu nae alipita upande mwingine na kusonga mbele huku akigeuka kutazama nyuma.

“ Wana wanachomoa zana kuelekea kwenye gari letu.” Kisu alimwambia Bob.

“Achana nao, vuka upande wa pili na…” Bob alisema huku akihamia njia nyingine, nyuma yake Kisu alifuatia. Walipiga hatua chache baada ya kuvuka na masikio yao yakasikia mirindimo ya risasi, walipogeuka walishuhudia watu wawili waliokuwa wamepakizana kwenye pikipiki, wakilishambulia gari lao kwa risasi kisha wakaondoa pikipiki kwa kasi na kuacha taharuki ikiwa imetanda kwenye barabara ile.

“Wajinga walidhamiria kutugeuza tenga kwa risasi zao.” Kisu alisema huku akiwatizama wale jamaa walivyokuwa wakiharakisha kukimbia na pikipiki yao.

“Acha walipwe ujira wa kazi ambayo hawajaifanya.” Bob alisema huku akisimamisha bajaji na kumshitua mwenzake wapande kuelekea mahali fulani
*****

Tukutane baadae
 
Mkuu hii kitu inaelekea kuwa tamu zaidi,jitahidi uongeze ongeze nyama mkuu
Inaonekana wahusika wa humu ni wajanja wajanja tu kina Zuki Gadu a.k.a miguu ya kuku,Rashid Chota a.k.aBob Rando ,Kisu
 
Kudo inapatikana vp hii?mi sitaki arosto,funguka tusiotaka arosto tujimilikishe! wanaopenda free waendelee kusubiri!
 
Kudo inapatikana vp hii?mi sitaki arosto,funguka tusiotaka arosto tujimilikishe! wanaopenda free waendelee kusubiri!
Wewe mzee mjanja sana. Umeleta story alafu unatumia id nyingine ili kujifanya unataka kununua ili uwavute wengine. Safi sana
 
Sisi akina sadala tumeamua kuweka kambi hapa....arosto ndio maisha tuliyochagua.
Kudo twende kazi.
 
“Wajinga walidhamiria kutugeuza tenga kwa risasi zao.” Kisu alisema huku akiwatizama wale jamaa walivyokuwa wakiharakisha kukimbia na pikipiki yao.

“Acha walipwe ujira wa kazi ambayo hawajaifanya.” Bob alisema huku akisimamisha bajaji na kumshitua mwenzake wapande kuelekea mahali fulani.

*******

Mahali pengine ndani ya jiji la Dar es laam, watu wawili walikuwa wakitazamana kwa namna ya ajabu, mmoja akiwa amelala chali na kamba zikiwa zimemfunga mikono na miguu yake, mwingine alikuwa amesimama na karatasi mkononi mwake walitazamana bila kusemeshana kwa zaidi ya dakika mbili huku kila mmoja akionesha ufundi wa kutizama bila kupepesa macho.

“Hivi kumbe Zuki ni kimtu chembamba kama msanii Wabogojo?” Jamaa aliyekuwa amesimama alimkebehi bwana Zuki Gadu ambae hakuwa mnene wala mwembamba kama yule bwana alivyosema. Mwonekano wake ulikuwa katikati ya mtu mwembamba na mwembamba sana, pengine kwa sababu ya umbo lake refu ama kwa sababu ya hekaheka alizokuwa akipitia kwenye maisha yake, ilisababisha ashindwe kupata mwili wenye kuridhisha.

Licha ya kudhihakiwa lakini hakufungua kinywa chake na kusema kitu kutoka kwa yule jamaa, aliendelea kumtizama bila kusema kitu.

“Okey bwana Wabogojo, naomba unisanie hii karatasi ili niweze kuendelea na majukumu mengine.” Jamaa alisema huku akipeperusha karatasi iliyokuwa mkononi mwake, karatasi ambayo ilionekana kuwa na maelezo fulani ambayo Zuki hakuweza kuyasoma.

“Naomba nisome kabla ya kusaini” Zuki hatimae aliipata sauti iliyokuwa imejaa mikwaruzo.

“Kazi yako ni kusaini na mengine hayakuhusu kwa sasa.” Jamaa alijibu kwa sauti iliyojaa kiburi na ujivuni.

“Fanya unachoweza lakini siwezi kusaini kitu ambacho sikijui.” Zuki aliweka msimamo.

“Ukisaini kuna mambo yanaweza kuwa mepesi lakini ukiendelea na msimamo wako, utaendelea kusota hapa.”

“Hata nikifia hapa, lakini kusaini bila kusoma ni kitu nisichoweza kukifanya, labda niwe nimekufa.” Zuki alijibu, yule bwana alionekana kukereka na jibu alilopewa, aliweka pembeni karatasi na kumsogelea Zuki, kisha akaanza kumtupia makonde sehemu za kichwani na kifuani. Zuki aligugumia kwa maumivu lakini hakuwa na cha kufanya, mikono na miguu yake ilikuwa imefungwa na asingeliweza kujitetea.

“Kwa unampiga mtu ambae unajua hawezi kujitetea? Huoni unakuwa na tabia za fisi kuvizia mzoga?” Zuki alimwambia kauli yenye kukera, jamaa akasimama na kumtazama kwa hasira huku akitweta kama jogoo aliyeshindwa vita.

“Acha tabia za kupenda visivyochinjwa, unaonesha ni namna gani unavyoniogopa licha ya kunifanisha na Wabogojo.” Zuki aliendelea kumkera yule jamaa ambae alikuwa akipandisha na kukishusha kifua chake mithili ya mcheza mieleka aliyetolewa ulingoni bila ridhaa yake. Hasira ilimjaa pomoni, fikra za kijinga zikamjia kichwani mwake bila kupima madhara ya mawazo yake yaliongozwa na hasira zake, akasahau msemo wa wahenga uliowakumbusha watu kujiepusha kufanya maamuzi wakiwa na hasira, yule bwana akaamua kufanya uzembe usio na maana.

Yule jamaa akiwa anamtizama Zuki kwa hasira, alijisogeza pembeni ya kitanda na kujaribu kuchanganua mawazo yake huku akitupilia mbali mawazo ya tahadhari juu ya mtu aliyekuwa mbele yake, jeuri ikashinda jema, akasonya kwa sauti na kupiga hatua ndefu kuelekea nje ya kile chumba, aliipita sebule tupu kwa mwendo wa kasi mithili ya ndege kipanga, akauvuta mlango huku akisonya, akapiga hatua mbili na kutoka nje ya ile nyumba huku macho yake yakizunguka kila kona ya godauni, aliwaona walinzi watatu wenye silaha na utulivu aliouona, ulimfahamisha kundi kubwa la wenzake halikuwepo na alikuwa amebaki yeye na wale walinzi watatu. Akasonya na kugeuka kurejea ndani, akaufunga mlango kwa komeo na kupiga hatua za kishujaa kuingia ndani ya chumba huku akiwa amefura kwa hasira za mkizi.

“Aliyeagiza ukamatwe na uletwe hapa, itabidi umlaumu sana kwenye maisha yako. Leo nitakufanya chakula cha nguruwe na nitaenda kujibu mbele ya safari.” Yule jamaa alisema huku akichukua mkasi kwenye meza iliyokuwa pembeni yake na kuanza kuzikata kamba za manila zilizokuwa zimemfunga Zuki Gadu. Dakika moja ilitosha kuzikata kamba zote kisha kwa kasi akachomoa bastola kusikojulikana na kuiweka usoni kwa mateka wake.

“Taratibu shuka kitandani na unyooshe mikono juu.” Alifoka huku akionekana dhahiri kuzidiwa na hasira.
Zuki alitii alichoaelekezwa, alinyoosha mikono juu na kushusha miguu yake chini kisha akasimama huku akimtizama yule bwana.

“Geuka na uelekee sebuleni..” Jamaa alimpa maelekezo, alitii bila mbwebwe zozote. Alipiga hatua fupifupi huku akiwa amenyoosha mikono yake juu. Alipofika sebuleni alisimama kwa maelekezo ya mtesi wake, akasimama huku akiwa bado kanyoosha mikono juu. Wakati alipokuwa akingoja maelekezo mengine, alishangaa akitandikwa teke zito liliomjaa vema mgongoni mwake na kumsomba mzimamzima hadi chini, aliguna kwa pigo lile huku akiugulia maumivu yaliyokuwa yakisambaa mgongoni mwake.

“Inuka nikuoneshe kwa nini niliitwa Mataruma.” Jamaa alijigamba baada ya kumtandika mwenzake teke. Zuki aliinuka taratibu na kumgeukia mtesi wake na bila kusema kitu, alisimama wima huku akimtizama bwana Mataruma.

“Ni mimi na wewe kwenye hii nyumba, nataka tucharazane makonde hadi mshindi apatikane na ninakuhakikishia, nitakuvua sifa zote inazopewa huko mitaani bwana Miguu ya kuku.” Mataruma alimwambia huku akiweka chini bastola yake kisha akaweka mchoro tayari kwa mpambano. Mateka wake hakuhangaika kujipanga, alibaki akiwa amesimama kama vile hakuwa na nia ya ule mpambano. Jambo hilo lilimfanya Mataruma aghadhabike mara dufu, alihisi kudharauliwa. Akaunguruma kwa hasira huku akipiga hatua kumfuata, akarusha ngumi tatu kumwelekea lakini ni ngumi moja pekee iliyomgusa hasimu wake, ngumi nyingine zilipepea upepo. Mataruma hakuridhika na pigo moja kufanikiwa, akaunguruma tena huku akirusha teke na ngumi bila mpangilio, bahati ikawa kwake, akafanikiwa kumwangusha Zuki Gadu, akatabasamu kwa tukio lile la kumwamgusha chini mateka wake.

Zuki Gadu baada ya kuangushwa chini kwa mara nyingine hakufanya haraka kuinuka, alimtizama Mataruma akiwa palepale chini kisha akatema mate na kujiinua taratibu bila papara, akasimama na kujifuta mikono yake kisha akaweka mchoro na kuwa tayari kwa mchapo. Akachezesha miguu yake kama mtu anaejiandaa kucheza muziki wa singeli, macho yake yalimuona mtesi wake akimfuata kwa kasi huku akiwa anarusha makonde mfululizo, akamkwepa kidogo na kumtegea mguu, jamaa akaenda chini kwa kutanguliza kifua chini.

Mataruma baada ya kuangushwa, aliinuka kwa hasira kiasi alishindwa kuelewa apange pigo gani ili kumkabili adui yake, akajikuta akiruka kwa lengo la kumdaka Zuki, lakini alishangaa akienda chini kwa mara nyingine baada ya kukwepwa na kusindikizwa na ngumi nzito iliyojaa vema nyuma ya shingo, akapagawa, uoga wa kuzisikia sifa za mtu aliyekuwa akipambana nae, ulianza kumtafuna na angalau akili yake ikaanza kujutia maamuzi ya kumfungulia.

Zuki aliendelea kunesa huku akimsubiri mtesi wake ainuke, alinesa huku akitema mate kwa mara ya pili. Utemaji mate wake ulikuwa na maana ambayo Mataruma hakuijua na laiti angeliijua, ni vema angelipiga magoti na kuomba msamaha yaishe, lakini kwa kuwa hakuwa ametambua kwa nini Zuki alitema mate zaidi ya mara moja, aliamua kupambana kwa kuiamini bahati inaweza kuwa upande wake. Kitu ambacho hakujua ni kuwa, Zuki Gadu huwa na utaratibu wake wakati wa mapambano, utaratibu ambao humpa morali ya kupambana na kumaliza pambano ndani ya muda mfupi sana, akiwa amejiandaa kukabiliana na lolote, wakati wote hutembea na vipande vya karanga mdomoni na vipande hivyo huwa havizidi sita, endapo akiingia kwenye mpambano kwa kushitukizwa huangalia na eneo lenyewe, ikiwa ni nje au mzingira yenye mchanga, huokota vipande vya mchanga na kuviweka mdomoni na kama eneo litakuwa halina mchanga au kitu chochote ambacho kinaweza kukaa mdomoni, hutema kiasi kidogo cha mate huku akihesabu idadi ya mitemo yake na wakati wote huhakikisha haivuki mara sita kabla ya kumaliza mpambano
 
Zuki aliendelea kunesa huku akimsubiri mtesi wake ainuke, alinesa huku akitema mate kwa mara ya pili. Utemaji mate wake ulikuwa na maana ambayo Mataruma hakuijua na laiti angeliijua, ni vema angelipiga magoti na kuomba msamaha yaishe, lakini kwa kuwa hakuwa ametambua kwa nini Zuki alitema mate zaidi ya mara moja, aliamua kupambana kwa kuiamini bahati inaweza kuwa upande wake. Kitu ambacho hakujua ni kuwa, Zuki Gadu huwa na utaratibu wake wakati wa mapambano, utaratibu ambao humpa morali ya kupambana na kumaliza pambano ndani ya muda mfupi sana, akiwa amejiandaa kukabiliana na lolote, wakati wote hutembea na vipande vya karanga mdomoni na vipande hivyo huwa havizidi sita, endapo akiingia kwenye mpambano kwa kushitukizwa huangalia na eneo lenyewe, ikiwa ni nje au mzingira yenye mchanga, huokota vipande vya mchanga na kuviweka mdomoni na kama eneo litakuwa halina mchanga au kitu chochote ambacho kinaweza kukaa mdomoni, hutema kiasi kidogo cha mate huku akihesabu idadi ya mitemo yake na wakati wote huhakikisha haivuki mara sita kabla ya kumaliza mpambano.

Mbele ya Mataruma alikuwa ameshatema mate mara mbili na alisaliwa na idadi nyingine nne, lakini hakutaka ifike idadi hiyo kwa sababu hakutaka kutumia nguvu nyingi wakati mwili wake ulikuwa dhaifu.

Mataruma aliinuka na kujipanga kukabiliana kisha akapiga hatua zake na kujizungusha, akapiga flying kick lakini ilipanguliwa kwa ustadi mkubwa, akageuka kwa haraka baada ya pigo lake kutofanikiwa, akarusha teke lingine nalo likapuanguliwa, akarusha ngumi mbili mfululizo nazo zikapanguswa kama mzaha, akajiandaa kubadili aina ya mkao ili aweze kufaulu pambano, lakini kabla hajatulia na kupanga mkao, alianza kushambuliwa yeye kwa mtindo wa ajabu kabisa; alimuona Zuki akichuchumaa kama nyani aliyeibeba mahindi, kisha alianza kumfuata akiwa amechuchumaa vilevile na kumfanya aonekane kama mjusi aina ya Kimodo atembeapo. Mataruma alirudi nyuma kwa kasi kwa kuwa hakuwa anaelewa aina ya mchapo alioupanga mwenzake, lakini ajabu nyingine ikawa ni kasi aliyokuwa nayo bwana Zuki Gadu licha ya kuwa alikuwa anajongea akiwa amechuchumaa kidogo.

“Heh!” Mataruma alibweka huku akigota ukutani na hatua moja mbele yake alikuwepo hasimu wake, akataka kupiga hatua kuelekea kushoto lakini alishangaa akipigwa ngumi ya paja, akataka kukimbilia upande wa kulia lakini nako alikutana na pigo lililotua kwenye goti lake, alipojaribu kurusha teke, alishangaa maumivu makali yakisambaa kuanzia kwenye korodani zake na maumivu aliyopata ilibidi ashike via vyake vya uzazi huku akiinama, uso wake ukawa sawa na uso wa Zuki Gadu ambae alikuwa amechuchumaa.

Zuki Gadu baada ya mapigo yake kufanikiwa kumlainisha mtesi wake, akaitumia nafasi hiyo kumuadhibu kwa namna akivyotaka yeye.

“Nakutoa meno yote ya mbele ili ukose mchumba.” Zuki alimtambia huku akitamtandika kichwa kizito kilichotua sawia mdomoni mwa Mataruma, meno mawili yakaruka huku papi za midomo zikichanika na kuanza kutoa damu. Kama alihisi kichwa alichopigwa ndilo pigo la mwisho alijidanganya, alitandikwa ngumi upande wa kushoto shingo, akapepesuka kuelekea kulia lakini huko nako alikutana na ngumi iliyotua vema upande wa kulia wa shingo, akapepesuka tena kurudi kushoto, hakupoa, akachapwa makofi mawili kila upande kisha akasindikzwa na ngumi iliyotua kichogoni mwake, viungo vikashindwa kuhimili akalegea na kwenda chini mithili ya fuko la maganda ya ndizi, Mataruma alitepeta.

“Siku nyingine ukilisikia jina langu, kimbia.” Zuki alimwambia huku akiinama kuokota bastola iliyokuwa imewekwa chini, akaifyatua kilinda usalama na kupiga hatua kumfuata Mataruma ambae alikuwa akihangaika kuinuka chini huku mdomo ukiwa umemlegea na udenda wa damu ukimchuruzika, ngumi za shingo alizopigwa zilikuwa zikimnyima nafuu ya kupumua, akabaki akihema kwa vituo kama Kobe aliyefika mshindo.

“Sasa utayajibu maswali yangu bila kusita la sivyo, nakugeuza chakula cha mchwa.” Zuki aliwambia huku akimnyooshea bastola usoni.

“Kwa… kwani wewe ni nani hasa?” Mataruma alijitahidi kuipata sauti yake na kuuliza, hakudhani kama aliyekuwa mbele yake ni jambazi wa kawaida, alikuwa ni zaidi ya komando wa jeshi.

“Naitwa Zuki Gadu ukipenda niite Miguu ya kuku, kawasimulie na wenzio.” Zuki alimjibu.

“Namaanisha wewe ni nani ukiachana na jina lako?” Mataruma aliuliza kwa mara nyingine.

“Mimi ni huyo niliyekutajia, mengine hayana maana kwa sasa.” Zuki alimjibu huku akimtizama kwa umakini kisha akauliza.

“Una watoto wangapi?”

“Nina mke na watoto watatu.” Mataruma alijibu akiwa amefanikiwa kuinuka na kupiga magoti huku akiendelea kuhema kwa kuibiabia kwa kuwa bado hewa hakuwa akiivuta sawia.

“Una machaguo mawili; kufa uwaache au kuishi uwalee. Zoezi ni dogo, jibu maswali yangu.”

Mataruma alifumba macho hakuwa na namna ya kujitetea, viungo vyake vilikuwa havina ushirikiano na asingeliweza kujitutumua kupambana. Chozi la hasira likamtoka.

“Uliniletea karatasi ya maelezo niisaini, imetoka wapi hiyo karatasi?” Zuki alimuuliza.

“Nilipewa na Gunda.” Mataruma alimjibu.

“Ni nani huyo?”

“Ni kiongozi wetu.”

“Ninyi ni kina nani?”

“Kikosi maalumu cha kupambana na ugaidi nchini.”

“Kosa langu ni nini hadi mkaniweka hapa?”

“Yalikuwa ni maelekezo ya Gunda.”

“Yeye alielekezwa na nani?”

“Sifahamu.”

“Nawezaje kumpata huyo Gunda?”

“Anapoishi sipafahamu, ila kituo chake cha kazi ni kituo cha polisi cha Sitakishari”

“Ina maana ninyi hamna kituo chenu maalumu?”

“Huwa tunakutana kwa dharura tu na kila mmoja anafanya kazi kituo chake, huwa tunakutana kwenye kambi zetu za siri kila tunapohitajika.”

“Sasa ikitokea ugaidi mahali fulani na hampo pamoja huwa mnafanya nini?”

“Kitengo kilicho chini ya Gunda ni kitengo cha kuhoji watuhumiwa wa ugaidi, kuvamia maeneo yanayohisiwa kuhifadhi wahalifu…”

“Kwa hiyo kuna kikosi kingine kilicho maalumu kwa kufika maeneo yenye tukio la ugaidi?”

“Upo sahihi”

“Sawa, kanisimulie” Zuki alisema huku akifyatua risasi iliyotua kwenye paja la kushoto na kumwacha Mataruma akipiga yowe la uchungu huku akigalala chini kama mbwa aliyekwamwa na mfupa kooni.

Sauti ya risasi iliwafikia walinzi waliokuwa nje na kwa kuwa hawakuwa na taarifa ya kilichokuwa kikiendelea kwenye nyumba yao ya huduma ya kwanza, walikurupuka kwenye viota vyao vya ulinzi na kukimbilia kwenye ile nyumba ili kujua kilichotokea, hawakuwa na shaka sana kwa sababu mtuhumiwa wao walimfunga na mwenzao ndiye aliyekuwa na uwezo wa kufyatua risasi pengine kumtisha mtuhumiwa, lakini iliwalazimu kukimbilia huko ili kuwa na hakika na walichokisikia. Kitu ambacho hawakujua ni kwamba, mpiga risasi alifanya vile makusudi ili kuwaita waliokuwa nje, alijua miongoni mwao ni lazima wangelikimbilia pale ndani, ilikuwa vema zaidi kwake kuwapunguza.

Zuki Gadu baada ya kumchapa risasi Mataruma, alikimbilia nyuma ya mlango huku akiwa ameondoa komeo kwenye mlango.
Walinzi wawili waliingia kwa kasi huku macho yao yakiangukia kwa mwenzao aliyekuwa akiugulia maumivu huku akiwa kwenye dimbwi la damu, umakini uliwapotea na haraka walikimbilia alipokuwa mwenzoa bila kuchukua tahadhari, mlinzi wa tatu aliwahi kushituka baada ya kuingia mlangoni, aliiweka vema bunduki yake na kufyatua kilinda usalama, lakini alipotokeza ndani aliambulia kuchakazwa risasi mbili, wale wawili nao walishituka na kugeuka lakini walikuwa wamechelewa, risasi ziliwaingia bila kupenda na kila mmoja alianguka chini na kusambaratika kivyake huku uhai ukiwa mbali na miili yao.

Zuki Gadu aliendelea kutulia nyuma ya mlango na kutega sikio lake kunasa kishindo cha mtu yeyote aliyekuwa akisogea, dakika zilipita bila kusikia chochote. Haraka alipiga hatua na kwenda kumgusa Mataruma ambae alikuwa anaendelea kugugumia kwa maumivu.

“Nimekupiga risasi ili wenzako wasikutilia shaka, pia iwe funzo kwako ya kuwa usiongozwe kwa hasira maana, hasira za mkizi furaha ya mvuvi. Mimi naondoka, kasimulie kuhusu Miguu ya kuku” Alimwambia kisha alipiga hatua na kutoka nje kwa umakini mkubwa, macho yake yalizunguka kila eneo ndani ya godauni ile lakini hakuweza kumuona mtu mwingine, akajitokeza na kupiga risasi moja juu kisha akakimbia na kwenda kujibanza kwenye kichaka cha maua huku akisubiri kuona kama kuna yeyote ambae angelitokea mafichoni. Dakika mbili zilikatika bila kumuona yeyote, akajitokeza na kukimbia haraka kuelekea kwenye nyumba ambayo alifungwa siku alipoingizwa kwenye ile kambi ya siri ya kikosi cha kupambana na kuzuia ugaidi.

Alifika mlangoni na kulikuta kufuli kubwa likiwa linaning'inia, akazinga bastola na kufyatua risasi iliyotawanya kufuli, akavuta mlango na kuingia ndani. Haraka alizungusha macho kwenye kona moja ya ile nyumba, alitabasamu huku akipumua kwa matumaini. Alipiga hatua na kuinama, alipoinuka alikuwa na begi lake, hakuhaangaika kulikagua kwa kuwa aliona lilikuwa vilevile kama alivyoona lilivyotupwa wakati akiingizwa pale ndani. Alishukuru kwa kuwa aliamini vitu vyake muhimu vitakuwa vipo salama.

Alitoka nje kwa kasi kubwa kuelekea upande ambao kulikuwa kumepangwa kontena zaidi ya mbili, aliruka na kutua juu ya kontena moja wapo kisha akaaanza kukimbia juu ya kontena hadi alipofika kwenye ukuta wa ile ngome, akatizama upande wa nyuma wa ngome ile na kuliona shamba dogo la migomba. Bila kujishauri zaidi, alikanyaga juu ya ukuta na kujirusha upande wa nje wa ile kambi na kuangukia shambani, kisha akaanza kukimbia kuelekea nje ya lile shamba huku masikio yake yakisikia miungurumo ya ndege zikitua uwanjani..

“Kumbe wapuuzi walinifunga hapa Banana!” Aliwaza huku akizidi kujiweka mbali na ile kambi ya wanausalama wa kupambana na ugaidi. Alikimbia huku akiapa kuwaadabisha wote waliokuwa wakitaka kumzamisha gerezani, akapanga kuliongezea joto jiji la Dar es laam
 
Back
Top Bottom