Dokta Slaa aitisha Press Conference Iringa!

Dokta Slaa aitisha Press Conference Iringa!

Sasa naweza kuunganisha doti jinsi wanasiasa wetu wanavyojiuza. Rafiki yangu mmoja (ni askari wa JW) aliwahi kunieleza Zitto alivyokuwa akifanya vikao tata hapa Dar na Dom na akina Rostam na Sitta so kuna mengi tutasikia baada ya Dokta kutoa kifuniko cha tanuru la ukweli
Du hata mm naunganisha ..... zako kweli kuna kitu hapa kweli uongozi ni mtamu, km Zitto, Rostam, Sitta naye alikuwemo tuwasubiri kina Mnauye na January kweli pesa na Hummer ni tamu
 
Sasa naweza kuunganisha doti jinsi wanasiasa wetu wanavyojiuza. Rafiki yangu mmoja (ni askari wa JW) aliwahi kunieleza Zitto alivyokuwa akifanya vikao tata hapa Dar na Dom na akina Rostam na Sitta so kuna mengi tutasikia baada ya Dokta kutoa kifuniko cha tanuru la ukweli

Nabado mtashangaa sana miaka hii.....Nilileta thread imefutwa nisawa lakini be informed authority without power to effect change is meaningless! With the power bestowed upon me I decree and declear hakuna fisadi atakatiza hiki kimbunga; wakwanza ni huyu mnafiki ndoto zake tayari zimezimwa baada ya kukatakata miguu yake iliyokuwa inakimbilia nyumba yetu tukufu huku moyoni akiwa na agenda yake binafsi......Anafuata mwingine not very far from now hadi mafisadi wote watambue kuwa when we speak we speak with authority full supported with heavenly powers and therefore our comands are yee and amen!
 
Lowasa anazidi kusafishiwa njia.

Good for him!!

Sadly CCM imebaki kukanusha na kuattack personalities instead of working ....nyie ndio mmeshika dola, kazi rasmi ya upinzani ni kuwachapeni bakora....angali Romney anapopangua hoja za Obama based on what he said and haven't delivered sio nyie mara mzee kaishiwa sera...oooh vyama vya msimu...leteni single nyingine
Btw Mitt Romney is about 68 ....so go figure
 
Good for him!!

Sadly CCM imebaki kukanusha na kuattack personalities instead of working ....nyie ndio mmeshika dola, kazi rasmi ya upinzani ni kuwachapeni bakora....angali Romney anapopangua hoja za Obama based on what he said and haven't delivered sio nyie mara mzee kaishiwa sera...oooh vyama vya msimu...leteni single nyingine
Btw Mitt Romney is about 68 ....so go figure

Mzee upo up to date eeh?
 
6 alichokosea ni ku-attack cdm na uongozi wake. Cck yake iko wapi? Wakati anaongelea hilo kule kagera, wanamagamba wenzake bashe na kigwangwallah wanachomoleana bastola tabora ambako ni mkoani kwake kwa kugombea madaraka. Shame upon him! M4c 4ever.
 
Jadili hoja sio mimi. Nakushauri usome tena maneno ya Slaa, Sitta nafasi aliyo iomba hawakukataa.Ni Sitta mwenyewe ndio alibadili mawazo. Leo hii mnasema hafai wakati viongozi wenu walikua tayari kumpa cheo kikubwa CDM. Na kama Sitta kutaka kuhama CCM amekua mnafiki je hao walio hama watakua ni nini?

Nasisitiza umejizingira na mtindio wa ufahamu kalaga baho
 
images
images

Katika uchaguzi mkuu uliopita, Chadema kilikuja kutangaza mwanachama wa kumsimamisha kugombea kiti cha Urais mwishoni kabisa baada ya kumwangukia na kumsihi Dr. Slaa agombee ambaye alishachukua tayari form za kugombea ubunge katika jimbo lake la uchaguzi.

Hii inatoa taswira kamili ya kila ambacho Katibu Mkuu wa Chadema alichosema Samweli Sitta alikubaliana nao kuwa atagombea Urais kupitia Chadema, lakini akawaacha kwenye mataa dakika za majeruhi, na wakati huo huo alikuwa ndiye mwanzilishi wa CCJ.

Kipindi cha Kampeni katika uchaguzi Mkuu uliopita, Dr. Slaa mara kadhaa alimwanika Samweli Sitta kwamba si mkweli, mnafiki, ana tabia ya hadaa, hana msimamo, ni ndumila kuwili mambo ambayo leo ameamua kumwaga mtama kwenye kuku wengi. Ukweli huu Sitta hawezi kuukwepa maana wakati uli alikuwa akifanya kampeni makanisani kwa kisingizio cha kuwa mgeni wa mahafali vyuo vya dini na matukio mengine ya dini ili kuungwa mkono.

Kwa nafasi kadhaa Sitta aliwahi kutamka kwamba ametafutwa na vyama kadhaa vya upinzani agombee uraisi, na akasema urais ni isue nzito na kuu ya yeye kubombaniwa na vyama vya upinzani.

Kuna dalili kwamba pamoja na kutaka kugombea huko, alikuwa hajiamini na hakuamini kama anaweza kumshinda Kikwete, na hivyo kuishia kutorokea mitaani kuwakwepa Chadema aliowaahidia, na mwishoni kabisa Chadema wakafanya kama zima moto kumwangukia Dr. Slaa ambaye tunavyojua aliweza kumtikisa Kikwete hadi kuchanganyikiwa na kuanza siasa za udini.

Naweza kusema lilikuwa kosa lenye heri kwa Sitta kukimbilia mafichoni, kwani angegombea huenda Chadema kisingepata kukua na kukubalika kama Dr. Slaa alivyokijenga hadi sasa.

Nahitimisha kwa kusema Samweli sitta ni ndumila kuwili, ni sawa na kinyonga anayejigeuza rangi kutegemeana na mazingira aliyo nayo, na akisha toka hapo hutaamini alivyobadilika rangi, labda amebaki na sura tu lakini rangi yake hubadilikabadilika. Sitta kigeugeu, ana tamaa ya madaraka, anajikweza, na pengine yaliyosababishwa yeye kuenguliwa na CCM kugombea uspika ni tabia hiyo ambayo wanaCCM waliona anaweza kuwageuka baadaye na pengine kutolinda masilahi ya chama. CCJ mwasisi halisi ni Sitta, akina Nape walitumiwa tu, na walipona wameingizwa kicha kichwa wakaamua nao kusepa.

safari hii CDM watamweka nani? maana haya maamuzi ya dk za mwisho ndiyo limekuwa tatizo. na kwanini watu hawataki kujadili future presidents? kwani wakijulikana mapema ili mapungufu na potential zao ziaze kujadiliwa mapema ni tatizo? huwa naona USA wanakuwa na muda mrefu wa kuwajadili wagombea wao, lakini huku kwetu inakuwa siri mpaka dk za mwisho kuelekea uchaguzi. ni vyema kwenye katiba likawekwa wazi angalau kuwe na mwaka hivi wa kuwajadili.
 
safari hii CDM watamweka nani? maana haya maamuzi ya dk za mwisho ndiyo limekuwa tatizo. na kwanini watu hawataki kujadili future presidents? kwani wakijulikana mapema ili mapungufu na potential zao ziaze kujadiliwa mapema ni tatizo? huwa naona USA wanakuwa na muda mrefu wa kuwajadili wagombea wao, lakini huku kwetu inakuwa siri mpaka dk za mwisho kuelekea uchaguzi. ni vyema kwenye katiba likawekwa wazi angalau kuwe na mwaka hivi wa kuwajadili.

Tatizo ni mfumo uliopo. Huruhusiwi kufanya kampeni mpaka ndani ya ule mwezi mmoja na nusu kabla ya uchaguzi Mkuu, jambo ambalo hugharimu zaidi na pengine kulazimika kutumia chopper ili kuwahi kufika maeneo mengi. Ukifanya kampeni kabla ya muda wake kadiri ya sheria za uchaguzi za nchi hii candidate ataondolewa kwenya uchaguzi kwa kukiuka sheria na taratibu za uchaguzi hasa akiwa wa chama cha upinzani.

Marekani uchaguzi wa mwaka huu harakati zimeanza tangu mwaka jana na baada ya kura za maoni kupitisha jina la mgombea wa Republican, alianza kufanya kampeni kabla ya nomination iliyofanyika Jana huko Florida. Hili kwa bongo haiwezekani.

Kwa tanzania kwa sasa bora ibaki ilivyo kwani bado tuko nyuma katika mambo mengi ya kidemokrasia vinginevyo kutazuka mitafaruku mingi sana tu.
 
Sasa kwanini unliniambia nirudi shule?
Dogo na wewe magwanda yashaanza kukuwasha nini?
Kayafue!!

Kukuambia urudi shule sio kwamba hujasoma bali katika mjadala husika ukiiweka kando akili na maarifa, unakumbushwa kwenda shule, maana yake irejeshe hapa akili yako na itumike.
 
Back
Top Bottom