Dodoma-Ofisi ya Spika yatamba!

Dodoma-Ofisi ya Spika yatamba!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Katika kile kinachoonekana kama upofu wa viongozi wa kitaifa katika kufanya yawapasayo kuyafanya kwa ajili ya wananchi wote,Ofisi ya Spika wa Bunge imetamba kuwa itahakikisha kuwa Bunge la Bajeti halioneshwi luningani. Afisa mmoja Mwandamizi wa Bunge,leo asubuhi ya saa tatu na nusu, alituambia kuwa Ofisi ya Bunge itasimamia uamuzi wake wa awali wa kutorusha moja kwa moja vikao vya Bunge ili kulinda hadhi ya Bunge hilo.

'Katibu Mkuu wa Bunge(Dr.Kashililla) alishasema kuwa Bunge halitaoneshwa 'live'. Watu wakamzongazonga sana kimaneno. Lakini,mwisho wa siku yeye ameibuka mshindi. Si mnaona mpango wa kutolionesha 'live' umeshaanza? ' alisema Afisa huyo wa Bunge

'Watanzania ni rahisi sana kuwaongoza mtu atakavyo. Unasema kwanza. Wakibisha,unawadanganya kuwa umekubaliana nao. Halafu,unafanya utakavyo.Hawabishi tena. Ndivyo Ofisi ya Spika ilivyofanya. Spika na Naibu wake wameubariki uamuzi huu,nani hapa nchini ataupinga?' aliuliza kwa kejeli Afisa huyo aliyekuwa akificha kitambulisho chake ingawa jina la kwanza ni Frank.

Watanzania mpo? Taarifa ni kuwa,mtapata 'edited version' ya Bunge la luningani. Wa kubisha na abishe. Ofisi ya Spika wa Bunge imeapa kusimamia uamuzi wake wa kuzuia kuoneshwa moja kwa moja kwa Bunge.

Tafakari na uchukue hatua!

VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam(sasa Dodoma)
 
Last edited by a moderator:
Kwa hiyo wanachokiaonyesha sasa inawezekana ikawa mwisho leo,ukweli ni kwamba wanajitahidi kuongeza hasira za wananchi kwa MACCM na mwenyekiti wao Jakaya
 
Muda utatuambia..! Matatizo yawananchi tunajua sisi wananchi, tunayaishi matatizo hayo, tukitafuta namna yakuyaondoa. Bungeni wanaoitwa wawakilishi wetu wanaenda kuyasema nasi twawaona kupitia luninga, hivyo hata wasiporusha live sisi ndio kiini chamatatizo hayo nabado tunayatafutia dawa sikupitia luninga
 
Katika kile kinachoonekana kama upofu wa viongozi wa kitaifa katika kufanya yawapasayo kuyafanya kwa ajili ya wananchi wote,Ofisi ya Spika wa Bunge imetamba kuwa itahakikisha kuwa Bunge la Bajeti halioneshwi luningani. Afisa mmoja Mwandamizi wa Bunge,leo asubuhi ya saa tatu na nusu, alituambia kuwa Ofisi ya Bunge itasimamia uamuzi wake wa awali wa kutorusha moja kwa moja vikao vya Bunge ili kulinda hadhi ya Bunge hilo.

'Katibu Mkuu wa Bunge(Dr.Kashililla) alishasema kuwa Bunge halitaoneshwa 'live'. Watu wakamzongazonga sana kimaneno. Lakini,mwisho wa siku yeye ameibuka mshindi. Si mnaona mpango wa kutolionesha 'live' umeshaanza? ' alisema Afisa huyo wa Bunge

'Watanzania ni rahisi sana kuwaongoza mtu atakavyo. Unasema kwanza. Wakibisha,unawadanganya kuwa umekubaliana nao. Halafu,unafanya utakavyo.Hawabishi tena. Ndivyo Ofisi ya Spika ilivyofanya. Spika na Naibu wake wameubariki uamuzi huu,nani hapa nchini ataupinga?' aliuliza kwa kejeli Afisa huyo aliyekuwa akificha kitambulisho chake ingawa jina la kwanza ni Frank.

Watanzania mpo? Taarifa ni kuwa,mtapata 'edited version' ya Bunge la luningani. Wa kubisha na abishe. Ofisi ya Spika wa Bunge imeapa kusimamia uamuzi wake wa kuzuia kuoneshwa moja kwa moja kwa Bunge.

Tafakari na uchukue hatua!

VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam(sasa Dodoma)

kuliko kuonyesha udhaifu wako hapa ni bora ukalale
 
Mkuu VUTA-NKUVUTE kwa kipindi kirefu nimekuwa sikuamini kulingana na taarifa zako za namna yake unazoweka humu jukwaani ila jana nimeanza kukuamini kidogo baada ya kufanyia utafiti wa kina taarifa yako fulani.Hii ya leo ni kipimo cha mwisho kwangu. Ikitokea kuanzia kesho bunge likawa halirushwi tena mimi ntakuamini sasa.Mpaka kufikia leo bunge bado lilikuwa linakenda live.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu VUTA-NKUVUTE kwa kipindi kirefu nimekuwa sikuamini kulingana na taarifa zako za namna yake unazoweka humu jukwaani ila jana nimeanza kukuamini kidogo baada ya kufanyia utafiti wa kina taarifa yako fulani.Hii ya leo ni kipimo cha mwisho kwangu. Ikitokea kuanzia kesho bunge likawa halirushwi tena mimi ntakuamini sasa.Mpaka kufikia leo bunge bado lilikuwa linakenda live.
Mkuu betlehem,yawezekana huo ni mpango utakaotekelezwa kwa hatua. Yawezekana ikawa ni taarifa tu hii.Ngoja tusubiri.
 
Last edited by a moderator:
Namuona kabisa mbunge wa Vunjo mkazi wa Sinza na Kiraracha akiliporomosha denda ndembendembe baada ya kuzidiwa na usingizi mkali na mzito.
images
 
Kenya wenzetu wanaonesha Mahakama Kuu yao ikiendesha kesi yz kupinga matokeo ya Rais. Tanzania (Bunge) linataka kuficha yanayojadiliwa. Hakika huku ni kukosa ukomavu kulikokubuhu.

Hili likitokea, Hatutakuwa na sababu ya kuwa na bunge lilochaguliw na wananchi. Hii itakuwa ni sawa na mikutano ya ya baraza la mawaziri
.
 
hakuna jipya kwako wewe vuta nikusukume

umekosa weledi.. mbona tunaangalia bunge hapa....

kuliko kuonyesha udhaifu wako hapa ni bora ukalale

silense is gold...vuta nkuvute u better keep quiete
bungeni unahesabiwa idadi ya post nini? haiwezekani post nne zote zikijibu post moja tu. Unatia mashaka jaribu kutulia na kandika majibu yako sio kukurupuka unatujazia jamvi.
 
Last edited by a moderator:
bungeni unahesabiwa idadi ya post nini? haiwezekani post nne zote zikijibu post moja tu. Unatia mashaka jaribu kutulia na kandika majibu yako sio kukurupuka unatujazia jamvi.

Huyo anamatatizo mengi sana.Nadhani atakuwa analipwa kutokana na ananvyo post humu kwenye Jamvi.
 
Wallah hawawezi kutunyima uhondo huu,Tutahamasishana tutinge hapo hapo mjengoni.Tm will tell.
 
bungeni unahesabiwa idadi ya post nini? haiwezekani post nne zote zikijibu post moja tu. Unatia mashaka jaribu kutulia na kandika majibu yako sio kukurupuka unatujazia jamvi.

Mkuu hiyo ndo ajira yake inayo muweka mjini, nasikia siku hizi posho za Lumumba zinatolewa kufuatana na idadi ya post.
 
Katika kile kinachoonekana kama upofu wa viongozi wa kitaifa katika kufanya yawapasayo kuyafanya kwa ajili ya wananchi wote,Ofisi ya Spika wa Bunge imetamba kuwa itahakikisha kuwa Bunge la Bajeti halioneshwi luningani. Afisa mmoja Mwandamizi wa Bunge,leo asubuhi ya saa tatu na nusu, alituambia kuwa Ofisi ya Bunge itasimamia uamuzi wake wa awali wa kutorusha moja kwa moja vikao vya Bunge ili kulinda hadhi ya Bunge hilo.

'Katibu Mkuu wa Bunge(Dr.Kashililla) alishasema kuwa Bunge halitaoneshwa 'live'. Watu wakamzongazonga sana kimaneno. Lakini,mwisho wa siku yeye ameibuka mshindi. Si mnaona mpango wa kutolionesha 'live' umeshaanza? ' alisema Afisa huyo wa Bunge

'Watanzania ni rahisi sana kuwaongoza mtu atakavyo. Unasema kwanza. Wakibisha,unawadanganya kuwa umekubaliana nao. Halafu,unafanya utakavyo.Hawabishi tena. Ndivyo Ofisi ya Spika ilivyofanya. Spika na Naibu wake wameubariki uamuzi huu,nani hapa nchini ataupinga?' aliuliza kwa kejeli Afisa huyo aliyekuwa akificha kitambulisho chake ingawa jina la kwanza ni Frank.

Watanzania mpo? Taarifa ni kuwa,mtapata 'edited version' ya Bunge la luningani. Wa kubisha na abishe. Ofisi ya Spika wa Bunge imeapa kusimamia uamuzi wake wa kuzuia kuoneshwa moja kwa moja kwa Bunge.

Tafakari na uchukue hatua!

VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam(sasa Dodoma)


Kama haya uliyoyaandika yataonekana kuwa sio kweli ,watu wa sampuli yako wanaitwa WACHOCHEZI na ni hatari kwa Taifa!!!
 
bungeni unahesabiwa idadi ya post nini? haiwezekani post nne zote zikijibu post moja tu. Unatia mashaka jaribu kutulia na kandika majibu yako sio kukurupuka unatujazia jamvi.


Mkuu unashangaa kwenye hii thread tuu, nenda kwenye ile ya hotuba ya Mbowe kuna michango yake kama 50 hivi, rudi kwa ile ya Arusha kuhusu uchaguzi wa madiwani napo kuna michango ya jamaa kama 10. Imagine kajiunga juzi lakini score bodi inaonyesha anamichango zaid ya 150, na ukizingatia yote pumba tupu.
 
Kama sisi ndo tuliowatuma lazima lioneshwe na kama wametumwa bungeni na familia zao lisioneshwe.
Ivi unatoa wapi kiburi cha kusema bunge lisioneshwe ivi unaficha nini?
Mikataba ya Tz na wawekezaji au China ni siri sasa ata vikao vya bunge ni siri
Tunakoelekea ni kubaya
 
Back
Top Bottom