Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,234
Kiongozi wa Machifu wa Mkoa wa Dodoma, Chifu Yasin Bilinji amesema kuwa kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025, tambiko limeandaliwa mkoani Dodoma kwa lengo la kuombea uchaguzi huo ufanyike kwa amani.
Amesema kuwa kufanyika kwa amani na utulivu kwa uchaguzi huo ni mojawapo ya njia za kumuenzi Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Pia, ametoa wito kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura ili waweze kuchagua viongozi wanaowataka kwa ajili ya kuwaongoza kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Amesema kuwa kufanyika kwa amani na utulivu kwa uchaguzi huo ni mojawapo ya njia za kumuenzi Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Pia, ametoa wito kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura ili waweze kuchagua viongozi wanaowataka kwa ajili ya kuwaongoza kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.