Dodoma iitwe Nyerere JK City

Dodoma iitwe Nyerere JK City

Joined
Feb 25, 2015
Posts
67
Reaction score
127
Hili ni wazo langu pekee mimi siyo mjumbe wa Kamati Kuu wala NEC wala mwanachama wa chama chochote cha siasa ni raia mzalendo wa kawaida tu niliyezaliwa miezi michache kabla ya uhuru wa nchi hii.

Baada ya kukubali kuwa Dodoma yawe Makao Makuu ya Serikali, nimetafakari kwa kina sana kwanini tusiupe heshima ya jina la Rais wetu wa kwanza kama ilivyo jiji la Washington DC na majiji mengine ulimwenguni?

Nimejiridhisha kwa sababu kuu zifuatazo;

1) Mwalimu JK Nyerere ni muasisi wa kwanza wa Taifa hili
2) Ndiye aliyesimamia na kupitisha wazo la Dodoma kuwa Makao Makuu
3) Ili kumuenzi kwa uzuri kabisa licha ya kutumia jina lake kwa majina ya Kiwanja cha Ndege, Barabara, mitaa, shule na Majengo basi tukajumuisha yote kabisa na kuuita Jiji lijalo la Dodoma kwa jina NYERERE JK CITY. Hii itatoa nafasi kwa vizazi vijavyo kutokuipoteza historia ya Mwalimu JK Nyerere muasisi wa Taifa.
4.) Ni mtanzania pekee wa kwanza kuweza kuwaunganisha watanzania wa kabila zote na kujenga utaifa.
Naelewa kuwa mji wa Dodoma una historia ya uasili wake, Nia yangu siyo kuipora hiyo historia bali ni kuiongezea thamani zaidi na kuinganisha katika historia ya nchi hii kikamilifu.

Dhamira yangu si kisiasa bali ni maono niliyoyapata baada ya kutathimini kwa kina mengi mema Mwalimu JK Nyerere aliyoifanyia nchi hii.Mbali ya wachangiaji mbali mbali wa safu hii naamini pia wanasiasa wetu wenye nia njema na nchi hii wataafiki wazo hili na kukaribisha mjadala wa kitaifa kuhusu wazo hili.Tusiingize malumbano ya kisiasa katika kujadili mustakabali wa wazo hili.
 
Majengo basi tukajumuisha yote kabisa na kuuita Jiji lijalo la Dodoma kwa jina NYERERE JK CITY. Hii itatoa nafasi kwa vizazi vijavyo kutokuipoteza historia ya Mwalimu JK Nyerere muasisi wa Taifa.
4.) Ni mtanzania pekee wa kwanza kuweza kuwaunganisha watanzania wa kabila zote na kujenga utaifa.
Naelewa kuwa mji wa Dodoma una historia ya uasili wake, Nia yangu siyo kuipora hiyo historia bali ni kuiongezea thamani zaidi na kuinganisha katika historia ya nchi hii kikamilifu.

yani kuna watu wajinga na wazito kufikiria... hatuja fikia hatua ya kuabudu watu... hii hali haitakiwi...! mwisho tuta taka taifa liitwe Nyerere, shenzii kabisa...

walio pigania uhuru na nyerere mbona wame sahaulika? nyerere alikuwa peke yake? msilete umimi na ujinga wenu wa kufikiri mambo kwa kina...

hata wewe una nafasi yako katika taifa hili ili liweze kupiga hatua, yule amepewa dhamana na wananchi bila wananchi hasinge kuwa yeye... pale alipo... na wengine wote waliofata

thamani ya wananchi na taifa ni kubwa kuliko mtu mmoja... juzi trump ali laani kuuwawa kwa watu nchini kwake na kusema taifa hilo lime jengwa kwa miaka mingi mpaka kufika hapo na thamni ya wamarekani ni kubwa pia, FBI na vyombo vingine vya ulinzi visiweke nguvu kubwa nje ya nchi na kuacha raia wa marekani waki poteza maisha ndani ya nchi yao, waanze kuimarisha ulinzi ndani ndipo watoke nje... wasikalie kupiga soga kuhusu udukuzi wa ushindi wake na kuacha raia wakiuwawa hovyo...
 
paitwe hivyo hivyo Dodoma ila iwe inatamkika kwa kiarabu yaani "Duwduwma
 
Nimekukubali hoja na wazo lako ni muafaka kabisa .Vizazi hivi hawajui umuhimu wa Mwalimu JK Nyerere kabisa.Twende mbele twende nyuma Dodoma inapaswa kupewa hadhi ya Jiji tena kwa jina pendekezwa.Nawasilisha.......
 
Back
Top Bottom