Mkereketwa_Huyu
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 10,590
- 7,951
Nimepatwa na mshtuko baada ya kupata majibu ya DNA yakionyesha mtoto niliekuwa na wasiwasi nae kwamba nimebambikiwa ni wakwangu tena kwa asilimia 99.99%.....ilikuwa hivi, mimi ni mtanzania kabila mpare na nimeoa mwanamke wa kirangi tuliejaaliwa kupata watoto wanne, wakiume watatu na wakike mmoja....chakushangaza mtoto wetu wanne alitoka na nywele za kiarabu na ukimuangalia huulizi sababu ni mwarabu kabisa,,,nilichofanya ni kumchukua kisirisiri bila mama yake kujua na kwenda kumpima DNA nikitarajia majibu yakionyesha si wangu nianze sasa movement au step forward...
sasa nashangaa majibu yametoka eto mtoto ni wa kwangu kwa asilimia zote,,kwakweli nimepata maswali mengi kama ni kweli vipimo hivi ni sahihi ama lah...vilevile watu wengi wameniambia eti siku hizi jamaa hawa huwa wanadanganya na kukupa majibu ya uongo kuonyesha mtoto ni wa kwako hata kama si kweli ili kupunguza watoto wa mitaani sasa niko njia panda jamani nifanyaje katika hili? naomba mwenye uzoefu na hawa jamaa atueleze ukweli katika hili tafadhali
Yote hayo uliyodanganywa na jamaa huko mitaani juu ya hali hii huenda ikawa ni kweli. Ila hapa kuna mawili: La kwanza huenda huyo aliyempima mwanao ni ndugu na huyo mwanamke hivyo anamlinda kwa kukudanganya kwa kukuambia mtoto ni wako japo wewe si mwarabu. La pili hapa ambalo ni hali ya kawaida hapa Bongo ni hivi; huenda hiii mashine ni ya kichina na inatoa vipimo feki au aliyekupima si mjuzi wa hii kitu (DNA). Jaribu kwenda Muhimbili ama toka nje ya nchi kupima kama uwezo unaruhusu.