DNA & hobbies

DNA & hobbies

Eiyer

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2011
Posts
28,259
Reaction score
20,916
Wakuu habarini za wakati huu,

Kuna swali ambalo nimekuwa najiuliza sana na nimekosa jibu na hili nadhani naweza kupata jibu hapa kwenu wakuu maana hapa hakuna kinachoweza kuharibika.

Kimsingi nina maswali mawili...

1; Hili la kwanza ni kuhusu DNA [vinasaba]

Binadamu tunarithi vinasaba hivi kutoka kwa wazazi wetu na wazazi wetu nao hivyo hivyo pia,inaelezwa kuwa chanzo cha binadamu ni kimoja,yaani tuwe tuliumbwa au iwe ni kwa kupitia evolution bado haiondoi ukweli kuwa huko tulikotokea chanzo ni kimoja.

Sasa kama tuna chanzo kimoja na sisi tunarithi hivi vinasaba kutoka kwa wazazi na wazazi walirithi kutoka kwa wazazi wao, nao wazazi wa wazazi wetu walirithi hivyo hivyo na kuendelea, inakuwaje vinasaba hivi vinakuja kutofautiana kwa mtu mmoja hadi mwingine wakati chain yetu inatuelekeza kwenye chanzo kimoja?

2; Hili la pili ni kuhusu hobby

Ni kitu gani kinasababisha mtu anakuwa anapenda kitu fulani?
Kama ni malezi au wazazi, inakuwaje watoto wawili wanakulia kwenye mazingira yale yale na wanazaliwa na wazazi wale wale halafu wanakuja kuwa na hobby tofauti?

Unakuta mmoja hapendi kabisa chai ya maziwa na mwingine bila kuinywa bado anakuwa hajaiona siku, hili linasababishwa na kitu gani?

Karibuni kwa majibu.

CC: Monstgala Ishmael ......
 
Mungu hudhihirisha uwezo wake kwa maswali kama haya;

HOBBY:
Kwa haraka haraka tu; Hobby huzalishwa na mambo mengi sana. Lakini sababu kubwa kwa kweli ni kupitia milango ya fahamu. Nini tunaona, nini tunasikia, nini tunahisi, nini tunaonja, nini nini nini!

Utofauti baina ya mtu na mtu unaletwa na mazingira, maumbile, n.k.

Kuhusu DNA, sina utaalamu nalo kwa kweli!
 
Asante kwa changamoto ya haya maswali, nimeyapenda kwani yamenipa dk chache za kujaribu kufikiria majibu, inawezekana kwa wataalamu wanajua kama kuna sababu hasa maalumu zinazopelekea tofauti hizo. Mimi najibu kwa kutumia tu akili ya kuzaliwa, binafsi sijafikiria ktk mambo ya kitaalamu zaidi.

DNA.
Binafsi nadhani iko hivi; japo tunazaliwa na Vina sawa kila mmoja akirithi toka kwa wazazi wake, lakini bado hatufanani mkuu,

1 .naamini kila mmoja anazaliwa na kitu kingine tofauti cha ziada ukiacha kile anachopata toka kwa wazazi. - Ndio maana unakuta huyu kazaliwa na kasoro hii na yule kasoro ile, japo wote tunaweza toka bila kasoro ya wazi, lakini kwa ndani zipo kasoro ambazo ndio hupelekea tofauti zetu. Amini tofauti zipo tu.

2. Tunazaliwa na wazazi (baba na mama), wazazi kila mmoja alikuwa na vina vyake, hivyo wanapokutana na kuwa mwili mmoja kuna vitu wanaunganisha na kupata kitu tofauti na kile alichokuwa nacho, ndo mana unakuta watoto wanafanana vina na baba yao, lakini ukimpima na babu yake mzaa baba wahafanani kabisa.

HOBBY
Bado naamini hatuzaliwi sawa kabisa, lazima kuna vitu vya ndani tunatofautiana, ndio maana unaweza kuta mtoto kazaliwa yupo vizuri, zen baada ya miaka 2 anapata shida fulani, baada ya uchunguzi, wanasema huyu alizaliwa bila hiki, au alizaliwa ikiwa kitu fulani kimezidi mwilini, na hivi vyote vinaweza kwa namna fulani kuja kuwa sababu ya tofauti za hobby kwa watoto. + mazingira unayokulia hapo badae hujenga hobby.

Ni majibu tu kwa kufikiria, ila inawezekana zipo sababu maalumu toka kwa wataalamu.
 
nitajaribu kuweka akili zangu kwenye swali lako la kwanza. inakubidi uelewe kuwa kisayansi kuna aina mbili za kuzaliana (reproduction) ambozo ni; sexual na asexual reproduction. asexual reproduction hii ni aina ya reproduction ambapo ni kiumbe cha aina moja pekee kinatumika kujizalisha kwa kujigawa (FISSION/MITOSIS) chenyewe, na hapo wote mtoto na mzazi hufanana katika vinasaba vyao. aina hii ya kuzaliana hufanywa na single celled organisms pamoja na cell regeneration katika mwili wako na wa viumbe vingine, mfano mjusi huweza kuota mkia wake iwapo utakatika. ukija kwa sexual reproduction hapo ni lazma viumbe vya aina mbili (i.e kike na kiume) vikutanishe gameti zao ndipo mtoto anaweza kupatikana. na gameti hizi hutengenezwa kwa mchakato ambao kisayansi huitwa MEIOSIS. utofauti mkubwa wa meiosis na mitosis ni kuwa wakati wa meiosis kuna vitendo viwili hutokea. vitendo hivi ni CROSSING OVER & INDEPENDENT ASSORTMENT. siwezi kwenda kwenye details zaidi kutokana muda kutotosha. vitendo hivi viwili husababisha gameti na seli nyingine za mzazi kutofautiana. kwa vitendo hivi ukijumlisha na kuunganika kwa seli mbili kutoka kwa wazazi (ambao nao walitokana na wazazi tofauti ili huyo mtoto atokee basi tunapata kiumbe tofauti kabisa na wazazi wake. samahani kama majibu yangu yatakuwa hayajakusaidia UBAVU
 
Mungu hudhihirisha uwezo wake kwa maswali kama haya;

HOBBY:
Kwa haraka haraka tu; Hobby huzalishwa na mambo mengi sana. Lakini sababu kubwa kwa kweli ni kupitia milango ya fahamu. Nini tunaona, nini tunasikia, nini tunahisi, nini tunaonja, nini nini nini!

Utofauti baina ya mtu na mtu unaletwa na mazingira, maumbile, n.k.

Kuhusu DNA, sina utaalamu nalo kwa kweli!
Mkuu umesoma mfano wangu wa watoto wawili hapo juu?
 
Asante kwa changamoto ya haya maswali, nimeyapenda kwani yamenipa dk chache za kujaribu kufikiria majibu, inawezekana kwa wataalamu wanajua kama kuna sababu hasa maalumu zinazopelekea tofauti hizo. Mimi najibu kwa kutumia tu akili ya kuzaliwa, binafsi sijafikiria ktk mambo ya kitaalamu zaidi.
Ok,wacha tukaone mchango wako ......
DNA.
Binafsi nadhani iko hivi; japo tunazaliwa na Vina sawa kila mmoja akirithi toka kwa wazazi wake, lakini bado hatufanani mkuu,

1 .naamini kila mmoja anazaliwa na kitu kingine tofauti cha ziada ukiacha kile anachopata toka kwa wazazi. - Ndio maana unakuta huyu kazaliwa na kasoro hii na yule kasoro ile, japo wote tunaweza toka bila kasoro ya wazi, lakini kwa ndani zipo kasoro ambazo ndio hupelekea tofauti zetu. Amini tofauti zipo tu.
Unaposema kasoro unakuwa unamaana gani?
2. Tunazaliwa na wazazi (baba na mama), wazazi kila mmoja alikuwa na vina vyake, hivyo wanapokutana na kuwa mwili mmoja kuna vitu wanaunganisha na kupata kitu tofauti na kile alichokuwa nacho, ndo mana unakuta watoto wanafanana vina na baba yao, lakini ukimpima na babu yake mzaa baba wahafanani kabisa.
Kwa kujibu wa ufahamu tulionao kuhusu binadamu ni kuwa wote tuna chanzo kimoja,sasa kaka tuna chanzo kimoja hivyo "vina vyake" huyo mwenye navyo anavitoa wapi?

Kwa mujibu wa hili tulipaswa wote tuwe na vinasaba vinavyofanana na sio tofauti kwasababu wewe hapo na mama/baba yako vinasaba vyenu vinafanana,wazazi wako na wazazi wa wazazi wako nao hivyo hivyo na chain hii inaendelea hadi kwenye chanzo cha binadamu ambacho ni kimoja

Wacha nikupe mfano rahisi sana;

Sisi tunaoamini binadamu aliumbwa tunajua kuwa waliumbwa wawili mwanaume na mwanamke na hawa walizaa watoto,tunatarajia kuwa hawa watoto walifanana vinasaba na wazazi wao,watoto wa watoto wa awa binadamu wa kwanza walifanana vinasaba na wazazi wao ambao ni watoto wa wazazi wa kwanza,sasa ukija kuwapima vinasaba vya wajukuu wa wazazi wa kwanza kisha ukaja kulinganisha na vinasaba vya hawa wazazi wa kwanza utapata majibu gani?

Tofauti sio?
Kwanini?
Yaani ni sawa wewe na babu na bibi yako vinasaba vutofautiane wakati mtoto wao ambae ni baba/mama yako vinafanana,unaona ni sawa?
HOBBY
Bado naamini hatuzaliwi sawa kabisa, lazima kuna vitu vya ndani tunatofautiana, ndio maana unaweza kuta mtoto kazaliwa yupo vizuri, zen baada ya miaka 2 anapata shida fulani, baada ya uchunguzi, wanasema huyu alizaliwa bila hiki, au alizaliwa ikiwa kitu fulani kimezidi mwilini, na hivi vyote vinaweza kwa namna fulani kuja kuwa sababu ya tofauti za hobby kwa watoto. + mazingira unayokulia hapo badae hujenga hobby.

Ni majibu tu kwa kufikiria, ila inawezekana zipo sababu maalumu toka kwa wataalamu.
Naona hujasoma nilichoandika ukakielewa vizuri....

Shida yangu sio "kasoro" kwasababu hizo zinaweza kupatikana wakati wa ujauzito ambao unategemea hali za wazazi wakati huo,shida yangu no hobby ambayo tunaelezwa mazingira yanahusika,hebu soma mfano wangu wa watoto wawili hapo juu uone shida inapoanzia ....!!
 
nitajaribu kuweka akili zangu kwenye swali lako la kwanza. inakubidi uelewe kuwa kisayansi kuna aina mbili za kuzaliana (reproduction) ambozo ni; sexual na asexual reproduction. asexual reproduction hii ni aina ya reproduction ambapo ni kiumbe cha aina moja pekee kinatumika kujizalisha kwa kujigawa (FISSION/MITOSIS) chenyewe, na hapo wote mtoto na mzazi hufanana katika vinasaba vyao. aina hii ya kuzaliana hufanywa na single celled organisms pamoja na cell regeneration katika mwili wako na wa viumbe vingine, mfano mjusi huweza kuota mkia wake iwapo utakatika. ukija kwa sexual reproduction hapo ni lazma viumbe vya aina mbili (i.e kike na kiume) vikutanishe gameti zao ndipo mtoto anaweza kupatikana. na gameti hizi hutengenezwa kwa mchakato ambao kisayansi huitwa MEIOSIS. utofauti mkubwa wa meiosis na mitosis ni kuwa wakati wa meiosis kuna vitendo viwili hutokea. vitendo hivi ni CROSSING OVER & INDEPENDENT ASSORTMENT. siwezi kwenda kwenye details zaidi kutokana muda kutotosha. vitendo hivi viwili husababisha gameti na seli nyingine za mzazi kutofautiana. kwa vitendo hivi ukijumlisha na kuunganika kwa seli mbili kutoka kwa wazazi (ambao nao walitokana na wazazi tofauti ili huyo mtoto atokee basi tunapata kiumbe tofauti kabisa na wazazi wake. samahani kama majibu yangu yatakuwa hayajakusaidia UBAVU
Majibu yako sio kwamba hayajanisaidia bali sijayaelewa...

Hebu tafuta muda uje hapa utueleze kwa kirefu mkuu....!!
 
Ok,wacha tukaone mchango wako ......

Unaposema kasoro unakuwa unamaana gani?

Kwa kujibu wa ufahamu tulionao kuhusu binadamu ni kuwa wote tuna chanzo kimoja,sasa kaka tuna chanzo kimoja hivyo "vina vyake" huyo mwenye navyo anavitoa wapi?

Kwa mujibu wa hili tulipaswa wote tuwe na vinasaba vinavyofanana na sio tofauti kwasababu wewe hapo na mama/baba yako vinasaba vyenu vinafanana,wazazi wako na wazazi wa wazazi wako nao hivyo hivyo na chain hii inaendelea hadi kwenye chanzo cha binadamu ambacho ni kimoja

Wacha nikupe mfano rahisi sana;

Sisi tunaoamini binadamu aliumbwa tunajua kuwa waliumbwa wawili mwanaume na mwanamke na hawa walizaa watoto,tunatarajia kuwa hawa watoto walifanana vinasaba na wazazi wao,watoto wa watoto wa awa binadamu wa kwanza walifanana vinasaba na wazazi wao ambao ni watoto wa wazazi wa kwanza,sasa ukija kuwapima vinasaba vya wajukuu wa wazazi wa kwanza kisha ukaja kulinganisha na vinasaba vya hawa wazazi wa kwanza utapata majibu gani?

Tofauti sio?
Kwanini?
Yaani ni sawa wewe na babu na bibi yako vinasaba vutofautiane wakati mtoto wao ambae ni baba/mama yako vinafanana,unaona ni sawa?

Naona hujasoma nilichoandika ukakielewa vizuri....

Shida yangu sio "kasoro" kwasababu hizo zinaweza kupatikana wakati wa ujauzito ambao unategemea hali za wazazi wakati huo,shida yangu no hobby ambayo tunaelezwa mazingira yanahusika,hebu soma mfano wangu wa watoto wawili hapo juu uone shida inapoanzia ....!!


K! hebu jaribu kufanya hivi hapo kwenye neno kasoro kote, litoe na uweke neno tofauti, nadhani hilo neno limepeleke lengo langu kueleweka kinyume. Lengo langu ni kueleza kuwa. Tunazaliwa na kitu/vitu vya tofauti na pekee kwa kila mmoja tofauti na vile tunavyopata toka kwa wazazi.
 
Kuna swali huulizwa kifalsafa "unaona nini na unajifunza nini". Hoppy ya mtu husababishwa na mazingira na makuzi huku akiongozwa na swali hapo juu. Kuna mtoto anaweza kuona mama wa jirani anaishi maisha duni huku mumewe akijenga heshima baa, hali hii ikauumiza moyo na kumfanya kuchukia pombe. Mtoto mwingine akamchukulia yule baba ni shujaa na yeye akatamani kuwa kama yy.
 
nitajaribu kuweka akili zangu kwenye swali lako la kwanza. inakubidi uelewe kuwa kisayansi kuna aina mbili za kuzaliana (reproduction) ambozo ni; sexual na asexual reproduction. asexual reproduction hii ni aina ya reproduction ambapo ni kiumbe cha aina moja pekee kinatumika kujizalisha kwa kujigawa (FISSION/MITOSIS) chenyewe, na hapo wote mtoto na mzazi hufanana katika vinasaba vyao. aina hii ya kuzaliana hufanywa na single celled organisms pamoja na cell regeneration katika mwili wako na wa viumbe vingine, mfano mjusi huweza kuota mkia wake iwapo utakatika. ukija kwa sexual reproduction hapo ni lazma viumbe vya aina mbili (i.e kike na kiume) vikutanishe gameti zao ndipo mtoto anaweza kupatikana. na gameti hizi hutengenezwa kwa mchakato ambao kisayansi huitwa MEIOSIS. utofauti mkubwa wa meiosis na mitosis ni kuwa wakati wa meiosis kuna vitendo viwili hutokea. vitendo hivi ni CROSSING OVER & INDEPENDENT ASSORTMENT. siwezi kwenda kwenye details zaidi kutokana muda kutotosha. vitendo hivi viwili husababisha gameti na seli nyingine za mzazi kutofautiana. kwa vitendo hivi ukijumlisha na kuunganika kwa seli mbili kutoka kwa wazazi (ambao nao walitokana na wazazi tofauti ili huyo mtoto atokee basi tunapata kiumbe tofauti kabisa na wazazi wake. samahani kama majibu yangu yatakuwa hayajakusaidia UBAVU

Umejitahidi mkuu ila hapo ktk suala la kujizalisha, nadhani sisi binadamu haituhusu kabsa.
 
Kuna swali huulizwa kifalsafa "unaona nini na unajifunza nini". Hoppy ya mtu husababishwa na mazingira na makuzi huku akiongozwa na swali hapo juu. Kuna mtoto anaweza kuona mama wa jirani anaishi maisha duni huku mumewe akijenga heshima baa, hali hii ikauumiza moyo na kumfanya kuchukia pombe. Mtoto mwingine akamchukulia yule baba ni shujaa na yeye akatamani kuwa kama yy.

Pia wakati mwingine hobby ya mtoto inajengwa na mama wakati wa ujauzito, kuna mama mmoja alipokua mjamzito alipenda sana mayai, mtoto alipozaliwa hadi leo dume kubwa humwambii kitu kuhusu mayai, ila kuna wengine hata apende nini kipindi cha ujauzito yeye hawezi kupenda hicho kitu kabisa hapo baadae. Au unasemaje mtaalamu ktk hili?
 
Mimi mwenyewe nataka kujua ukipata jawabu limekuridhisha namie naliomba
 
Pia wakati mwingine hobby ya mtoto inajengwa na mama wakati wa ujauzito, kuna mama mmoja alipokua mjamzito alipenda sana mayai, mtoto alipozaliwa hadi leo dume kubwa humwambii kitu kuhusu mayai, ila kuna wengine hata apende nini kipindi cha ujauzito yeye hawezi kupenda hicho kitu kabisa hapo baadae. Au unasemaje mtaalamu ktk hili?
Malezi ya mtoto huanza mapema wakati wa kipindi cha kutafuta ujauzito (ukiondoa mimba zisizo tarajiwa) na kipindi chote cha ujauzito. Mfano ukiwa unamsikiliza Wimbo fulani mtt wakati akiwa tumboni ukija kujifungua usishangae mtt huyo akisikia ule Wimbo hata kama analia atatulia. (NB: Nisamehe bure wakati mwingine nataka kukupa "like" simu yangu inaniangusha)
 
Malezi ya mtoto huanza mapema wakati wa kipindi cha kutafuta ujauzito (ukiondoa mimba zisizo tarajiwa) na kipindi chote cha ujauzito. Mfano ukiwa unamsikiliza Wimbo fulani mtt wakati akiwa tumboni ukija kujifungua usishangae mtt huyo akisikia ule Wimbo hata kama analia atatulia. (NB: Nisamehe bure wakati mwingine nataka kukupa "like" simu yangu inaniangusha)

Aha aha ha ah like zangu banaaaa thanks mkuu
 
Eiyer, what a wonderfully written article! I am so happy that science will eventually PROVE our Creator!. Ngoja nitengeneze majibu thabit.

Nitaanzia na DNA, Kiufupi ninasema kuwa DNA is God's language. It has been found that DNA consists of a four bit digital code, inter-alia, such code cannot possibly be changed in a gradual manner as envisioned by Charles Darwin. Consequently, to alter and or amend batches of code would require either extreme outside intelligence, and even more so and simultaneously, to implant automatic rules (which appears to be the case) that would permit variations without damage.

That is why I am saying, DNA is God's language. Eiyer, through this thread "DNA", I will prove God's existence.
 
K! hebu jaribu kufanya hivi hapo kwenye neno kasoro kote, litoe na uweke neno tofauti, nadhani hilo neno limepeleke lengo langu kueleweka kinyume. Lengo langu ni kueleza kuwa. Tunazaliwa na kitu/vitu vya tofauti na pekee kwa kila mmoja tofauti na vile tunavyopata toka kwa wazazi.
Ukisoma majibu yako utagunduanyamejikita kwenye suala zaidi ya moja na ndio maana ninejibu hoja kwa hoja....

Hilo ka kasoro nakushauri hebu rudia ulichoandika kisha usome halafu utaona ni namna gani tofauti unayotaka kuiingiza hapo vile ambavyo hukua unamaanisha tofauti....
 
Eiyer, what a wonderfully written article! I am so happy that science will eventually PROVE our Creator!. Ngoja nitengeneze majibu thabit.

Nitaanzia na DNA, Kiufupi ninasema kuwa DNA is God's language. It has been found that DNA consists of a four bit digital code, inter-alia, such code cannot possibly be changed in a gradual manner as envisioned by Charles Darwin. Consequently, to alter and or amend batches of code would require either extreme outside intelligence, and even more so and simultaneously, to implant automatic rules (which appears to be the case) that would permit variations without damage.

That is why I am saying, DNA is God's language. Eiyer, through this thread "DNA", I will prove God's existence.

Kiongozi,wacha tuendelee kujifunza pamoja

Cc: Mashaxizo
 
Last edited by a moderator:
:Hobby:
Kila Mtu Mungu Amempa Zawadi Au Kipawa Chake,yaan Uwezo Binafsi Tofauti Na Mwinge. Kwa iyo tunaweza kuita hobby au kipawa ni uwezo mtu aliopewa na mungu kwa ajili ya kumfanikisha.
DNA
huo ni utaratibu tu wa mungu mwenyewe
 
:Hobby:
Kila Mtu Mungu Amempa Zawadi Au Kipawa Chake,yaan Uwezo Binafsi Tofauti Na Mwinge. Kwa iyo tunaweza kuita hobby au kipawa ni uwezo mtu aliopewa na mungu kwa ajili ya kumfanikisha.
DNA
huo ni utaratibu tu wa mungu mwenyewe.
 
Back
Top Bottom