PAYE
JF-Expert Member
- Jun 19, 2025
- 354
- 395
Hii leo Disemba 19, 2025, Spika Mstaafu wa Bunge la Tanzania ambaye ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Jimbo la Uyole Dkt. Tulia Ackson amepeleka nuru kwa Familia ya Anyomwisye Mwalyaje ambayo ilipata janga la nyumba kuungua kwa moto katika kata ya Ilemi.
Dkt.Tulia amekabidhi Nyumba iliyojengwa na Taasisi ya Tulia Trust kwa familia hiyo ambayo walipata majanga hayo mnamo Septemba 5,2025 na kufanya idadi ya nyumba alizo wajengea watu kufikia nyumba 22.
Mwisho, Dkt. Tulia amewashukuru wananchi wa mtaa wa Mwamfute kata ya Ilemi ambao walishirikiana na familia hiyo tangu mwanzo wa changamoto hiyo ilipojitokeza kwa kuwapatia misaada mbalimbali ikiwepo hifadhi ya kuishi pamoja na chakula.
Soma pia