Dkt. Slaa Kutua Mbagala (Mianzini) Kesho...

Dkt. Slaa Kutua Mbagala (Mianzini) Kesho...

Mwita Maranya

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2008
Posts
10,565
Reaction score
7,988
Salam wana JF.

Baada ya kukamilisha ziara ndefu na iliyojaa mafanikio katika mkoa wa Manyara, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni Kiongozi Mkuu wa upinzani nchini, kesho anatarajiwa kuzungumza na watanzania kupitia mkutano wa hadhara utakaofanyika katika viwanja vya Mbagala Zakhem jijini Dar es salaam.

Kabla ya mkutano huo wa hadhara Dkt. Slaa atapata fursa ya kukutana na timu inayoratibu kampeni za mgombea wetu wa udiwani katika kata ya Mianzini kamanda Cuthbert Saulo Ngwatta (almaarufu Mdudu) ambaye ndiye chaguo la wana mianzini.

Katika ziara hiyo Katibu mkuu katika kata ya Mianzini, ataambatana na viongozi wa kanda ya Pwani iliyo chini ya uenyekiti wa msomi na nguli Profesa Abdallah Safari.

Makamanda pamoja na wananchi waishio wilaya ya Temeke hasa maeneo ya jirani na Mbagala mnakaribishwa kumlaki na kumsikiliza kiongozi mahiri wa upinzani nchini kusikia atakuwa na ujumbe gani kwa watanzania hiyo kesho.

Nawasilisha. Peoples Power!
 
Rais ambaye hukutangazwa kutokana na tume chafu ya uchaguzi pole nakazi za chama karibu mianzini kuimarisha chama 2015 utatangazwa iam sure!!
 
Kiongozi aliyeko kwenye mioyo ya watu Dr Slaa.Hakika Jiji la Dar kesho litatikisika.
 
Kiongozi aliyeko kwenye mioyo ya watu Dr Slaa.Hakika Jiji la Dar kesho litatikisika.

Kamanda Molemo hatujaonana muda mrefu sana bila shaka kesho tutakuwa pamoja.
 
Last edited by a moderator:
Salam wana JF.

Baada ya kukamilisha ziara ndefu na iliyojaa mafanikio katika mkoa wa Manyara, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia ni Kiongozi Mkuu wa upinzani nchini, kesho anatarajiwa kuzungumza na watanzania kupitia mkutano wa hadhara utakaofanyika katika viwanja vya Mbagala Zakhem jijini Dar es salaam.

Kabla ya mkutano huo wa hadhara Dkt. Slaa atapata fursa ya kukutana na timu inayoratibu kampeni za mgombea wetu wa udiwani katika kata ya Mianzini kamanda Cuthbert Saulo Ngwatta (almaarufu Mdudu) ambaye ndiye chaguo la wana mianzini.

Katika ziara hiyo Katibu mkuu katika kata ya Mianzini, ataambatana na viongozi wa kanda ya Pwani iliyo chini ya uenyekiti wa msomi na nguli Profesa Abdallah Safari.

Makamanda pamoja na wananchi waishio wilaya ya Temeke hasa maeneo ya jirani na Mbagala mnakaribishwa kumlaki na kumsikiliza kiongozi mahiri wa upinzani nchini kusikia atakuwa na ujumbe gani kwa watanzania hiyo kesho.

Nawasilisha. Peoples Power!

hapo penye bold unatengeneza mgogoro kati yake na mbowe
 
ina maana dr slaa amefilisika sana kisiasa kiasi cha kuongoza kampeni za udiwani?
 
Rais ambaye hukutangazwa kutokana na tume chafu ya uchaguzi pole nakazi za chama karibu mianzini kuimarisha chama 2015 utatangazwa iam sure!!

atatangazwa na nani na nani atamlinda wakati amewatukana vyombo vyote vya dola
 
ina maana dr slaa amefilisika sana kisiasa kiasi cha kuongoza kampeni za udiwani?

hapana ni kwamba tunajenga kuanzia mizizi nyie mnayoyadharau hamjui huku ndo kufilisika kwenu kisiasa? mmezoea kujikweza sana ndo maan unashangaa hii hatua.
 
ina maana dr slaa amefilisika sana kisiasa kiasi cha kuongoza kampeni za udiwani?

Kweli wewe gamba la kobe.
Sasahivi Makamu mwenyekiti wa ccm Philip Mangula amepiga kambi kata ya Iyela jijini Mbeya kumuuza mgombea wenu.
Katibu mkuu wenu ze dentist Kinana akishirikiana na Katibu mwenezi Nape kwa pamoja wamepiga kambi Mikoa ya Iringa na Njombe wakiwanadi wagombea wenu wa udiwani.

Kama ungekuwa unatumia vizuri akili yako usingekurupuka na kuropoka vitu vilivyokuwa dhahiri kiasi hiki.

Hata kama unafukuzia buku saba kwa post lakini uwe unajitahidi kujua kinachoendelea duniani ili usionekane kituko mbele ya jamii.
 
Kiongozi aliyeko kwenye mioyo ya watu Dr Slaa.Hakika Jiji la Dar kesho litatikisika.

Kamanda molemo, ubarikiwe sana.popote kamanda molemo anapokuwa hapaharibiki kitu.tuko nyuma yako mkuu molemo.shukrani sana.
 
salam wana jf.

Baada ya kukamilisha ziara ndefu na iliyojaa mafanikio katika mkoa wa manyara, katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) ambaye pia ni kiongozi mkuu wa upinzani nchini, kesho anatarajiwa kuzungumza na watanzania kupitia mkutano wa hadhara utakaofanyika katika viwanja vya mbagala zakhem jijini dar es salaam.

Kabla ya mkutano huo wa hadhara dkt. Slaa atapata fursa ya kukutana na timu inayoratibu kampeni za mgombea wetu wa udiwani katika kata ya mianzini kamanda cuthbert saulo ngwatta (almaarufu mdudu) ambaye ndiye chaguo la wana mianzini.

Katika ziara hiyo katibu mkuu katika kata ya mianzini, ataambatana na viongozi wa kanda ya pwani iliyo chini ya uenyekiti wa msomi na nguli profesa abdallah safari.

Makamanda pamoja na wananchi waishio wilaya ya temeke hasa maeneo ya jirani na mbagala mnakaribishwa kumlaki na kumsikiliza kiongozi mahiri wa upinzani nchini kusikia atakuwa na ujumbe gani kwa watanzania hiyo kesho.

Nawasilisha. Peoples power!
ahsante kwa taarifa kamanda,ila usisahau live updates na mapicha kama kawa
 
Kweli wewe gamba la kobe.
Sasahivi Makamu mwenyekiti wa ccm Philip Mangula amepiga kambi kata ya Iyela jijini Mbeya kumuuza mgombea wenu.
Katibu mkuu wenu ze dentist Kinana akishirikiana na Katibu mwenezi Nape kwa pamoja wamepiga kambi Mikoa ya Iringa na Njombe wakiwanadi wagombea wenu wa udiwani.

Kama ungekuwa unatumia vizuri akili yako usingekurupuka na kuropoka vitu vilivyokuwa dhahiri kiasi hiki.

Hata kama unafukuzia buku saba kwa post lakini uwe unajitahidi kujua kinachoendelea duniani ili usionekane kituko mbele ya jamii.

Kamanda mwita maranya imemjibu kisomi, safi sana!
 
Najivunia kujitambua na kujiunga CDM,sichoki kuwaombea waliojivua ufahamu kwa sababu ya buku 7 nao wapate ukombozi wa fikra
 
Back
Top Bottom