Dkt. Slaa Kutua Mbagala (Mianzini) Kesho...

Dkt. Slaa Kutua Mbagala (Mianzini) Kesho...

Salam wana JF.

Baada ya kukamilisha ziara ndefu na iliyojaa mafanikio katika mkoa wa Manyara, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni Kiongozi Mkuu wa upinzani nchini, kesho anatarajiwa kuzungumza na watanzania kupitia mkutano wa hadhara utakaofanyika katika viwanja vya Mbagala Zakhem jijini Dar es salaam.

Kabla ya mkutano huo wa hadhara Dkt. Slaa atapata fursa ya kukutana na timu inayoratibu kampeni za mgombea wetu wa udiwani katika kata ya Mianzini kamanda Cuthbert Saulo Ngwatta (almaarufu Mdudu) ambaye ndiye chaguo la wana mianzini.

Katika ziara hiyo Katibu mkuu katika kata ya Mianzini, ataambatana na viongozi wa kanda ya Pwani iliyo chini ya uenyekiti wa msomi na nguli Profesa Abdallah Safari.

Makamanda pamoja na wananchi waishio wilaya ya Temeke hasa maeneo ya jirani na Mbagala mnakaribishwa kumlaki na kumsikiliza kiongozi mahiri wa upinzani nchini kusikia atakuwa na ujumbe gani kwa watanzania hiyo kesho.

Nawasilisha. Peoples Power!

uwepo wa molemo na maranya kwenye huo mkutano sina shaka na covarage ya kutosha.katika ujenzi wa nyumba tunathamini kila mtu.ur mark clear kamanda
 
Mia mkuu najua dr. Atakuja na mambo mapya ni mchaka mchaka mpaka kieleweke.
 
ina maana dr slaa amefilisika sana kisiasa kiasi cha kuongoza kampeni za udiwani?

Kwa hiyo Lowassa amefilisika sana kuongoza kampeni za udiwani Makuyuni? Ama hujamuona Wassira akimnadi mgombea Arusha? Na je Kinana alivyomnadi mgombea kule Njombe nayo hukuona? Na Mangula kule Mbeya nayo umejitia upofu?

Unafiki ni dhambi mbaya sana!
 
Nitakosa kuwapo huko kimwili ila kiroho nitakuwa na wanambagala wote, nawaomba jitokezeni mapema ili tusikilize sera ambazo ccmafisadi hujaribu kiziiba.
Kila la kheri wanamianzini msifanye makosa kwenye uchaguzi huo tuiweke ccm pembeni ili wajue tunauchungu na nchi yetu.
 
ina maana dr slaa amefilisika sana kisiasa kiasi cha kuongoza kampeni za udiwani?

Haya ya udiwani tuyaache , anataka kutumia jukwaa hilo kuongea na wananchi , yaani unataka Slaa awe Jangwani wakati kuna kampeni Mianzini ? Hebu Mswalie Mtume bhana !
 
Asante kamanda , ntahakikisha uwepo wangu ili kuhakikisha mambo yanaenda sawa .
 
Tuko wote wakuu.
Tafadhali mkuu Mwita na Molemo itabidi tujitahidi kuto update za kutosha,maana hata mimi huwa nachukia pale ambapo watu wanachelewa kuleta up dates.ningependa mjipange sawasawa,nitaangalia majukumu yatakavyokuwa,nisipobanwa na jukumu langu kwenye mkutano huo,basi sitoacha kitu kuwaletea,na ndio maana nawaomba Mwita na Molemo wajiandae.
nawasilisha!
 
Mkuu Mwita Maranya,
Asante sana kwa taarifa kamanda. Panapo majaliwa ya Mwenyezi Mungu mie ntakuwepo kwenye eneo la tukio.
 
Dr. wa ukweli kawapatie wana mbagala elimu ya uraia wajitambue
 
atatangazwa na nani na nani atamlinda wakati amewatukana vyombo vyote vya dola

Mtu akikuambia hajavaa nguo na ikiwa ni kweli hajakutukana bali kasema lilo sawia lakini kama umevaa atakuwa kakunenea sivyo.Ukweli unabaki kuwa hivyo japo waumiza.
 
Rais ambaye hukutangazwa kutokana na tume chafu ya uchaguzi pole nakazi za chama karibu mianzini kuimarisha chama 2015 utatangazwa iam sure!!

Hakika Watz tulidhulumiwa na mafisadi. hii haipaswi kujirudia. Pia tuwe tayari kupambana na mafisadi wa ccm wakati wa kura ya maoni dhidi ya rasimu ya katiba mpya.

Watarazimisha wananchi waikubali na kuipitisha kulinda wizi wao 2015. Hio tuwe tayari kutumia nguvu ya umma. Watz inaumma kununua sim ya Million (1000000/-) ila unapewa mche wa Sabuni. Sitasahau historia ya wizi wa kura 2010. Mungu atusaodie
 
Haya ya udiwani tuyaache , anataka kutumia jukwaa hilo kuongea na wananchi , yaani unataka Slaa awe Jangwani wakati kuna kampeni Mianzini ? Hebu Mswalie Mtume bhana !

Tuwe na busara! Dr.Slaa ni mtumishi wa Watz anawaelimisha watu kwa njia tofauti. Nakushangaa Nampangalala unapohoji kwa mtazamo wa kinafiki. unadhani atakuwa anaongea udiwani tu? Badilika plze.
 
Back
Top Bottom