george ndamanya
Member
- Jul 10, 2017
- 22
- 33
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuimarisha miradi ya maendeleo sambamba na kukuza uhusiano uliopo.
Dk. Shein amesema hayo alipokuwa na mazungumzo na Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Watu wa China Cai Defeng, aliopo nchini Tanzania kwa ziara ya siku sita kufuatia mwaliko wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai.
Katika mazungumzo hayo, Rais Dk. Shein alitoa shukurani kwa Serikali ya Watu wa China kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzbar katika kuendeleza miradi mbali mbali ya maendeleo ambayo imekuwa chachu katika kukuza uchumi wa Zanzibar. Rais Dk. Shein alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inathamini uhusiano na ushirikiano wa kihistoria uliopo kati yake na Jamhuri ya Watu wa China ambapo ujio wa kiongozi huyo unathibitisha ukweli huo.
Sambamba na hayo, Rais Dk. Shein ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar alipongeza uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati ya (CCM) na chama cha Kikomunisti cha China (CPC) chini ya uongozi wa Rais Xi Jinping wanchi hiyo.
Dk. Shein alizipongeza hatua za Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kuunga mkono jitihada za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo afya, elimu, kilimo, maji safi na salama, miundombinu, viwanda na mengineyo Dk. Shein alipongeza juhudi kubwa zinazochukuliwa na nchi hiyo katika kutoa nafasi za masomo kwa wanafunzi kutoka Zanzibar sambamba na mashirikiano yaliopo kutoka Jimbo la Jangsu katika kuimarisha sekta ya afya.
Dk. Shein amesema hayo alipokuwa na mazungumzo na Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Watu wa China Cai Defeng, aliopo nchini Tanzania kwa ziara ya siku sita kufuatia mwaliko wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai.
Katika mazungumzo hayo, Rais Dk. Shein alitoa shukurani kwa Serikali ya Watu wa China kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzbar katika kuendeleza miradi mbali mbali ya maendeleo ambayo imekuwa chachu katika kukuza uchumi wa Zanzibar. Rais Dk. Shein alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inathamini uhusiano na ushirikiano wa kihistoria uliopo kati yake na Jamhuri ya Watu wa China ambapo ujio wa kiongozi huyo unathibitisha ukweli huo.
Sambamba na hayo, Rais Dk. Shein ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar alipongeza uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati ya (CCM) na chama cha Kikomunisti cha China (CPC) chini ya uongozi wa Rais Xi Jinping wanchi hiyo.
Dk. Shein alizipongeza hatua za Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kuunga mkono jitihada za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo afya, elimu, kilimo, maji safi na salama, miundombinu, viwanda na mengineyo Dk. Shein alipongeza juhudi kubwa zinazochukuliwa na nchi hiyo katika kutoa nafasi za masomo kwa wanafunzi kutoka Zanzibar sambamba na mashirikiano yaliopo kutoka Jimbo la Jangsu katika kuimarisha sekta ya afya.