Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,234
Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dkt. Rugemeleza Nshala, akizungumza kwa niaba ya Jopo la Mawakili wa Chama hicho amesema kuwa Mahakama ya Rufaa imesikiliza na kupokea hoja zote za maombi ya marejeo ya mwenendo wa kesi ya mgawanyo wa mali za chama hicho, kesi iliyofunguliwa na Saidi Issa Mohamed na wenzake dhidi ya Bodi ya Wadhamini wa Chadema na Katibu Mkuu wa chama.
Dkt. Nshala ameyasema hayo leo Machi 24, 2026 jijini Dodoma katika viunga vya Mahakama (Judiciary Square) ambapo amebainisha kuwa Mahakama imesikiliza shauri la mapitio manne, na kwamba waliweza kuwasilisha mbele ya majaji hoja zote walizodai kuwa ni uvunjifu wa taratibu uliofanywa na Jaji Mwanga wakati wa usikilizwaji wa kesi hiyo katika Mahakama Kuu, jambo ambalo kwa mujibu wao lilipelekea chama kutendewa uonevu.
Soma Pia: Pingamizi kesi ya mgawanyo wa mali CHADEMA latupiliwa mbali
Amesema baadhi ya amri za mahakama zilizotolewa awali zilikuwa “zinalenga kuiingiza mahakama katika aibu,” na hivyo kulazimisha Chadema kuomba marejeo ili taratibu za kisheria zipitiwe upya.
Dkt. Nshala ameyasema hayo leo Machi 24, 2026 jijini Dodoma katika viunga vya Mahakama (Judiciary Square) ambapo amebainisha kuwa Mahakama imesikiliza shauri la mapitio manne, na kwamba waliweza kuwasilisha mbele ya majaji hoja zote walizodai kuwa ni uvunjifu wa taratibu uliofanywa na Jaji Mwanga wakati wa usikilizwaji wa kesi hiyo katika Mahakama Kuu, jambo ambalo kwa mujibu wao lilipelekea chama kutendewa uonevu.
Soma Pia: Pingamizi kesi ya mgawanyo wa mali CHADEMA latupiliwa mbali
Amesema baadhi ya amri za mahakama zilizotolewa awali zilikuwa “zinalenga kuiingiza mahakama katika aibu,” na hivyo kulazimisha Chadema kuomba marejeo ili taratibu za kisheria zipitiwe upya.