napata shida sana kuelewa hilo tukio la kumpiga risasi huyo binti! Kwani huyo binti alikuwa akiandamana akidai haki au alikuwa anapita na risasi ikampiga kwa bahati mbaya hasa kutokana na uzembe wa polisi? Kama hivyo ndivyo, iweje kilaumiwe chama fulani kwasababu ya ushindi wake badala ya kulaumu huyo mfyatuaji wa risasi? Kama ni uzembe wa polisi kwanini upinzani ushikilie bango kuwa ilikuwa ni makusudi wakati binti alikuwa mpita nja tu? Je ni dalili ya upinzani kukosa uwezo wa kuchambua masuala na kutambua kuwa ilikuwa bahati mbaya? Hali hiyo ni inaweza kuwa inaashiria mwanzo wa mwisho wa upinzani tukielekea uchaguzi mkuu wa 2020?
..labda kwasababu viongozi wa CCM husema jeshi la Polisi ni la kwao.
..kauli hizo zinaweza kupelekea CCM kulaumiwa kwa UNYAMA na UKATILI unaofanywa na Polisi.