PreGE2025 Dkt. David Mathayo anayemalizia ubunge wake jimbo la Same Magharibi achukua fomu tena

PreGE2025 Dkt. David Mathayo anayemalizia ubunge wake jimbo la Same Magharibi achukua fomu tena

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
MBUNGE wa Jimbo la Same magharibi mkoani Kilimanjaro, Dkt. David Mathayo amechukua fomu ya kuwania Ubunge katika jimbo hilo kwa awamu nyingine.

Mbunge huyo ambaye ameongoza kwa vipindi 4 mfulizo amedai kuwa anataka kuendeleza alipoishia katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Mathayo alifika katika katika ofisi za ccm wilaya ya same majira ya saa mbili kasoro za asubuhi na kupokelewa na Katibu wa CCM wilaya, Amos Kusakula na kukabidhiwa fomu hiyo.
 
Huyu dingi hazeekagi,, nimeanza msikia nipo primary huko. Mtoto wa Msuya huyu.
 
Hata hoja zake ni nyepesi mno.
Hata apewe miaka 20 mingine bado kuna vitu atakua hajamaliza.
Mbunge atumikie wananchi vipindi viwili mwisho na yeye aende akaanzishe biashara au kufungua kampuni aajiri watu wengine wachukue nafasi yake. Baada ya vipindi viwili asiruhusiwe kugombea.

Hii ya wabunge wanakaa kwenye hiyo nafasi zaidi ya miaka 25 haiko vizuri mtu anaweza geuka mchawi na muuaji
 
Ina maana huko Same hakuna watu wengine wanaoweza kuwa wabunge?
Miaka 20 mfululizo!!!
 
Back
Top Bottom