Uchaguzi 2020 Dkt. Charles Kimei ndiye habari ya Mjini Vunjo

SautiYaMnyonge

JF-Expert Member
May 13, 2018
439
742
Wanajukwaa salaam,

Kwa muda sasa wa wiki mbili nipo jimbo la Vunjo ambapo nilikuja kuona uzalishaji wa zao la vanila ukanda wa Kirua,Kilema,Marangu,Mamba na Mwika. Hali ya hewa ni baridi sana ukizingatia nimezoea maisha ya jiji la kibiashara au jiji la Kune Boy (Abubakar Kunenge RC Dar)

Katika pitapita zangu stori zinazobamba kila kona ni uchaguzi mkuu hususani nafasi ya ubunge katika jimbo hili ambapo mbunge aliyekuwepo Ndg James Mbatia naye amejitosa kwa mara nyingine kutetea nafasi yake japo hali ya kisiasa sio nzuri hata kidogo.

Yupo mgombea wa chadema Ndugu Grace Kiwelu huyu hapewi nafasi kwani amekuwa mbunge wa viti maalum miaka kumi hajawahi kuwa msaada kwa wana vunjo, wasemavyo wananchi walio wengi.

Habari ya mjini sasa ipo kwa Dkt Charles Stephen Kimei (CSK kama wanavyomuita) ambaye wanasema wakati alipokuwa mkurugenzi mtendaji wa CRDB alisaidia mambo mengi ikiwemo kuanzishwa kwa tawi la benki hiyo jimboni humo, kujenga kituo cha polisi Marangu mtoni, kununua magari mawili mapya aina ya landcruiser kwa ajili ya vituo vya polisi vya Himo na Marangu Mtoni, ukarabati wa Tumaini Saccos iliyopo Mamba Kusini, kuchangia ujenzi wa madarasa Mboni Sekondari,Kuchangia ujenzi wa mabweni ya wasichana Muungano Sekondari, amechangia vigae vya sakafuni (tiles) kukamilisha jengo la ofisi Vicoba Vunjo yenye wanachama 7,000 ambapo walimteua kuwa mkurugenzi wao kwa sasa.

Kwa hayo machache wanasema ni mtu ambaye alionesha mapenzi makubwa kwa wanavunjo muda mrefu sasa ni vizuri wakamtuma kuwa mbunge wao ili akafanye kazi hii kwa uzuri zaidi. Wengine wanasema jimbo hili lina fursa nyingi za kiuchumi ila hazijaibuliwa hivyo Kimei anamudu kuzifungua kwani kama aliweza kuitoa benki ya CRDB kutoka benki iliyokuwa inafilisika mpaka kuwa benki kubwa, mashuhuri, inayotengeneza faida kuliko benki zote nchini na kushinda tuzo mbalimbali za kimataifa za benki bora Afrika!

Hakuna shaka yoyote kuwa Moshi mweupe utaonekana kwa bingwa huyu wa uchumi na masuala ya kifedha, Namtakia kila la heri!

Tukumbuke uchaguzi unapita,nchi inabaki tuitunze amani yetu.

Pichani akiwa na vijana jimboni humo.

NB: Suala la urais huku sio agenda maana wanasema Rais yupo ambaye ni Magufuli anayekataa huyo ni mbishi tu wa asili

IMG-20200822-WA0028.jpg
 
Charles Kimei hajulikani jimbo la vunjo na Kitendo cha halmashauri Kuu ya Kamati kuu ya CCM kukata Jina la inock koola zadock mtoto wa Tajiri wa kimarangu Mzee Koola(Mmiliki wa makampuni ya Zadock A1outdoor Africa), ambaye alishinda kura Za maoni imeigawanyisha CCM jimboni vunjo pande mbili, wanao muunga mkono kimei na wale walichukizwa na kitendo cha koola kukatwa. Palikuwa hakuna shamrashara kimei alivyotangazwa kama mgombea wa ubunge CCM vunjo. Pili, kulazimishwa kustaafu CRDB, wananchi wa vunjo wanajua Magufuli alishauri astaafu kuliko kutumbuliwa kwa kashfa ya kulipwa mil 45 kwa mwezi. Hawa ndio wale waliomchukiza magufuli kwa kulipwa zaidi ya mil 40 kwa mwezi na alisema hadharani.

Nae James Mbatia alivyoshinda ubunge 2015 alilikacha jimbo na hakufanya kitu na alikuwa anaonekana kwa nadra sana jimboni humo. Alichangisha kila kaya 20,000 Za kuchonga barabara Jambo ambalo halikulitekeleza na limewaudhi wananchi jimboni humo. Hawataki kumsikia, Jambo jingine ni kwamba mbatia ushindi wake wa 2015 ulibebwa na ukawa na dhana kwamba lowassa angekuwa Rais na mbatia kuwa waziri wa elimu lakini hicho kitu hakipo kwa sasa kila chama kinajigemea hata Chadema ilimsaidia ashinde 2015, mwaka huu wameweka mgombea grace kiwelo.

Vunjo wanachagua mtu na sio chama, ambaye ana historia nzuri vunjo ni Augustine Mrema na akicheza karata zake vizuri anachukua jimbo.
 
SautiYaMnyonge,

Kwenye level ya social ties, huyu mtu simjui sana ila huwa nakuwa prompted kumfananisha fananisha na Mh. Dr Reginald Mengi (RIP). Nashauri Mh. Mbatia ajiandae kwa ajili ya kazi nyingine safari hii, uwezekano wa kurudi bungeni HAUPO. Bora ungekuwepo, ila ukawa ni mgumu,..., HAUPO! Kitu kigumu ambacho kipo ni tafauti sana, na kwa mbali sana na kile ambacho hakipo. Ni kwa sababu kile ambacho hakipo, HAKIPO!
 
Charles Kimei hajulikani jimbo la vunjo na Kitendo cha halmashauri Kuu ya Kamati kuu ya CCM kukata Jina la inock koola zadock mtoto wa Tajiri wa kimarangu Mzee Koola(Mmiliki wa makampuni ya Zadock A1outdoor Africa), ambaye alishinda kura Za maoni imeigawanyisha CCM jimboni vunjo pande mbili, wanao muunga mkono kimei na wale walichukizwa na kitendo cha koola kukatwa. Palikuwa hakuna shamrashara kimei alivyotangazwa kama mgombea wa ubunge CCM vunjo. Pili, kulazimishwa kustaafu CRDB, wananchi wa vunjo wanajua Magufuli alishauri astaafu kuliko kutumbuliwa kwa kashfa ya kulipwa mil 45 kwa mwezi. Hawa ndio wale waliomchukiza magufuli kwa kulipwa zaidi ya mil 40 kwa mwezi na alisema hadharani.


Nae James Mbatia alivyoshinda ubunge 2015 alilikacha jimbo na hakufanya kitu na alikuwa anaonekana kwa nadra sana jimboni humo. Alichangisha kila kaya 20,000 Za kuchonga barabara Jambo ambalo halikulitekeleza na limewaudhi wananchi jimboni humo. Hawataki kumsikia, Jambo jingine ni kwamba mbatia ushindi wake wa 2015 ulibebwa na ukawa na dhana kwamba lowassa angekuwa Rais na mbatia kuwa waziri wa elimu lakini hicho kitu hakipo kwa sasa kila chama kinajigemea hata Chadema ilimsaidia ashinde 2015, mwaka huu wameweka mgombea grace kiwelo.

Vunjo wanachagua mtu na sio chama, ambaye ana historia nzuri vunjo ni Augustine Mrema na akicheza karata zake vizuri anachukua jimbo
Nimependa uchambuzi wako.

Ila hapo mwisho, Ndugu Mrema bado ana nafasi huko Vunjo?
 
Nahuko Kilimanjaro/Moshi kwa wasomi bado wanaichaguaga ccm?.
Ndiyo hivyo watu wa vunjo ni wa tofauti sana yaani huwa hawaangalii chama
Yaani unaweza kuta Mbunge in wa CCM alafu madiwani wote ni TLP + Chadema.

Au mbunge. TLP madiwani wote CCM

Ni miongoni mwa majimbo machache nchini ambayo tangu uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi CCM waliwahi kushinda Mara Moja Tu 2005-2010 (kile kisulisuli cha JK) tokea hapo mpaka leo wanalitafuta na hawajalipata.

Pamoja na kuwa upinzani unaongoza vunjo tangu 1995 isipokuwa 2005-2010
Chadema haijawahi kushinda ubunge vunjo hata namba mbili haijawahi kushika inaambulia namba 3,4 na kuendelea
 
Kuna watu wanaamini kwamba Charles Kimei ataibadilisha Vunjo, sasa imani yao inaegemea kwamba jamaa alikuwa CRDB, na wanaamini pesa alizovuna CRDB zitaenda kuibadilisha Vunjo.

Haya ni mawazo si sahihi kabisa, MO alikuwa na pesa mbona singida bado ni masikini? Rostam alifanya nini Igunga si alikuwa na pesa?

wananchi wa vunjo ni werevu, Charles Kimei hatachukua pesa zake za mafao CRDB akawaletee watu maendeleo, hizi ni ndoto Za mchana, wananchi wa vunjo Wanajua mtu bora anayefaa ni Nani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom