Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt Doto Biteko amesema Rais Samia Suluhu Hassan anasikitishwa anapoona haki za kidini zinapuuzwa na anapenda kufanya kazi na viongozi wa dini na akiwaalika ili kuzungumza masuala mbalimbali ya kitaifa.
"Mheshimiwa Rais Samia anapenda kufanya kazi na viongozi wa dini na ninyi ni mashahidi amekuwa akiwaalika ili tuzungumze masuala mbalimbali ya kitaifa ingekuwa ni mtu anayejifungia ndani na akasema analo jeshi, sheria, katiba na vyombo vya ulinzi basi nitafanya kazi nadhani hivi ingekuwa ngumu sana lakini yeye amesema milango yetu iwe wazi tuzungumze na viongozi wa dini kwa ajili ya kutafuta mustakabali wa nchi yetu pale ambapo tunadhani hatuendi sawasawa,"
Dkt. Biteko amesema hayo Julai 3, 2025 jijini Dodoma wakati akimwakilisha Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano Mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT).
"Mheshimiwa Rais Samia anapenda kufanya kazi na viongozi wa dini na ninyi ni mashahidi amekuwa akiwaalika ili tuzungumze masuala mbalimbali ya kitaifa ingekuwa ni mtu anayejifungia ndani na akasema analo jeshi, sheria, katiba na vyombo vya ulinzi basi nitafanya kazi nadhani hivi ingekuwa ngumu sana lakini yeye amesema milango yetu iwe wazi tuzungumze na viongozi wa dini kwa ajili ya kutafuta mustakabali wa nchi yetu pale ambapo tunadhani hatuendi sawasawa,"
Dkt. Biteko amesema hayo Julai 3, 2025 jijini Dodoma wakati akimwakilisha Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano Mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT).