wewe Mwenyekiti wako hajachanganyikiwa baada ya kuvuta kivyake na kumsahau katibu Mkuu?Yaani Mwenyekiti amechanganyikiwa baada ya deal kutofanikiwa kaishia kusema ....Wapinzani Mtakiona cha Mtema kuni.........'Itabidi atuambie alikuwa anamaana gani kabla ya uchaguzi kuanza..............
Inasikitisha sana badala ya pesa kupelekwa sehemu muhimu wanatumia ili wabaki madarakani. Mungu ni mwema atatuepusha na hili zimwi!
wewe Mwenyekiti wako hajachanganyikiwa baada ya kuvuta kivyake na kumsahau katibu Mkuu?
tumia Lugha nzuri usi - panic hizi ni Siasa
mpaka usiku huu bado mnamsubiri tu aingie ofisini?
jaribuni asubuhi tena kwani yeye ni muungwana kakaa na ninyi miaka 20 leo Mwenyekiti wako anampa likizo
Kwanza Dr Slaa kesharudi ofisini?Ndiyo hapo tunapotakiwa kutumiaakili zaidi.Hakuna njia zaidi ya kuendelea kupigania HAKI zetu za msingi....Ukiwa na USHAHIDI wa Mwenyekiti wetu kupokea pesa tupatie tukamuulize!Kama huna basi huna hata rights za kuongea hayo.Ila wenzako tunaushahidi wa Mke wa Mwenyekiti wako kutoa RUSHWA ili wale waliogombana nao wakati wa UTEUZI wa mgombea URAIS kukatwa kwenye kinyang'anyiro cha Ubunge......
Kwanza Dr Slaa kesharudi ofisini?
unapigania Haki gani wewe ambayo huipati mpaka uitoe CCM?
mwanzo ulidai Mwenyekiti sasa unasema ni Mke wa Mwenyekiti
Mara nyingi unapochangia uwe mpole CCM haitaondolewa na jazba wala LOWASSA, Lipumba Dr au Mbowe ni Balot Box tu
- Hivi ni kwanini unawahusisha viongozi wangu kwenye fikra zako za kuwalaani?
- Tii Mamlaka uliyopewa na MUNGU muda wao ukipita tutakuja kwa Dr naye
- Lakini na mm nikianza kumwaga habari za Josephine Mshumbusi anavyomfungia au kutoa rushwa hapa usije juu, maana vituko vyake vyote vipo na tunamuheshimu km Mke wa Padre mfuasi wa Kristo
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, anatarajiwa kuwasili ofisini kwake leo, baada ya kutoweka tangu Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, alipojiunga na chama hicho hivi karibuni.
Hatua hiyo inakuja siku chache baada ya Baraza Kuu la chama hicho kuridhia apumzike kwa muda, baada ya kutofautiana na Kamati Kuu kwa kile kilichoelezwa kumkaribisha Lowassa.
Vyanzo vya uhakika ndani ya Chadema vilivyozungumza na MTANZANIA juzi na jana, vilisema Dk. Slaa huenda akarejea ofisini leo kutokana na mazungumzo yaliyofanyika kwa nyakati tofauti na viongozi waandamizi wa chama hicho.
Jana (juzi) mzee Philemon Ndesamburo na makada wengine wa chama walikwenda nyumbani kwa Dk. Slaa kwa ajili ya mazungumzo, na kwamba amekubali, amesema atarejea ofisini kesho (leo), alisema mtoa habari huyo.
Vyanzo hivyo vilisema Dk. Slaa amekubali kurudi ofisini na kuendelea na shughuli za chama baada ya Ndesamburo na makada wengine wanaoheshimika ndani ya chama hicho kuzungumza naye.
Mazungumzo hayo yanadhihirishwa pasipo shaka na picha zilizosambaa mitandaoni juzi, zilizomwonyesha Ndesamburo akiwa na Dk. Slaa na makada wengine wa chama hicho.
Mmoja wa makada wa chama hicho aliyeshiriki mazungumzo hayo juzi, ambaye hakutaka jina lake litajwe, alilidokeza gazeti hili kuwa walielewana na Dk. Slaa na akaahidi kuwa atarejea ofisini muda wowote.
Ni kweli tumezungumza na Dk. Slaa, na amekubali atarejea ofisini muda wowote, mengine tuliyozungumza siwezi kukwambia, alisema kada huyo.
Akihutubia wajumbe wa Baraza Kuu wiki iliyopita, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema amekutana na Dk. Slaa kwa mazungumzo na kwamba wameelewana apumzike.
Nilichukua uamuzi wa kukutana na Dk. Slaa kwa sababu ni kiongozi anayeheshimika na kupendwa, na ameshiriki katika hatua zote na vikao vya ujio wa Lowassa kikiwamo cha Kamati Kuu.
Tulikubaliana kwa pamoja baada ya kupitia mawasiliano ya kitakwimu, kisayansi na tafiti mbalimbali, kwamba kiongozi huyo (Lowassa) ni mpango wa Mungu, na atatusaidia kuwaunganisha wenzetu wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Wakati nimezungumza naye aliomba muda wa kupumzika huku akitoa ruhusa ya chama kuendelea na mipango yake ya kuelekea uchaguzi mkuu, tukatumia usemi unaosema maji yakikupwa na kujaa hayamsubiri mtu, hivyo hatuwezi kumsubiri mtu ili tuendelee.
Tumekubaliana na Katibu Mkuu, apumzike kwa muda na sisi tuendelee, na pindi atakapokuwa tayari ataungana nasi mbele ya safari. Sisi hatuwezi kuzuia mabadiliko kwa sababu ya Mbowe au Slaa, alisema Mbowe
CHANZO;MTANZANIA
Dr Slaa keshaingia ofisini au ni kesho tena maana mkimsingizia Mke ni chuki zenuMamlaka inayotoa RUSHWA na kuikabidhi nchi kwa wachina?Mamlaka ilikwisha laaniwa na Mungu kwa kuuza ardhi ya Tanzania?Mamlaka inayoendekeza ubadhirfu wa mali za umma,rushwa,ufisadi,ujangili,madawa ya kulevya nk nk?
Mamlaka inaua wananchi wake?Mamlaka inayoabudu CHUKI kuliko UPENDO?Sina sababu ya kutii mamlaka hii pole...
Dr Slaa keshaingia ofisini au ni kesho tena maana mkimsingizia Mke ni chuki zenu
soma Warumi 13:1-2
Mstari wa 6 unazungumzila 'walipeni Kodi, walipeni ushuru,astahiliye Hofu, hofu, astahiliye heshima, heshima
- Kila mtu na atii Mamlaka iliyo kuu, kwa maana hakuna mamlaka isiyo toka Mungu, na ile iliyopo omeamriwa na Mungu.
- Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu nao washindanao watajipatia hukumu.