Dk. Slaa kuhutubia Korogwe leo

Dk. Slaa kuhutubia Korogwe leo

luhui

Member
Joined
Dec 24, 2011
Posts
22
Reaction score
1
Katika suala la kutoa elimu na kukusanya maoni ya katiba leo katika viwanja vya Sokoni Dk. Slaa na Mabere Marando watahutubia saa tano asubuhi.

Picha zitafuata,naona watu wameanza kumiminika.
 
watu wengi sana wamehudhuria,ameanza waitara halafu marando wa mwisho ni katibu mkuu mwenyewe
 
Anaongea kuhusu uhuru wa kuabudu, anasema yeye kwake huwa akitaka kuchinja anamtafuta muislamu anachinja. Mzee anaongea vizuri. Nitaendelea kuandika anayozungumza ila picha sitaweza kuleta natumain Xp music. Ila mzee ni mkali sana. Anaongea kwahasira.
 
Kama rasimu isipopita je tutaendelea na ile ya zamani?.
Swali hili kalijibu kwajazba kiasia hata sijaelewa. Kutokana na muulizaji kuliuliza kimlengo wa kisiasa.
 
Ninaomba rais asiwe na mamlaka ya kumteua jaji mkuu. Na kama akifanya makosa aburuzwe mahakamani. Hoja imepita kwa wananchi kunyoosha mikono mingi.
 
Wananchi wanaonekana kutoelema maana ya rasimu na pia maoni yao ni ya ajabu mno. Eti mmoja anazungumzia hoja za maisha binafsi badala ya mambo ya kitaifa.
Hata ivo umeme umekatika hapa uwanjani pametukia na wananchi wengine wanaondoka.
 
Safiiii! Mwenyenzi MUNGU mwingi wa Rehema awape nguvu kila kukicha hawa makamanda waendelee kuibomoa chama cha mafisadi a.k.a ccm.
 
Umeme umerudi. Kipengele cha uwazi wananchi wamekubaliana mikataba kuwa wazi. Na pia maadili ya taifa yaingie kwenye katiba mfano kutangaza mali zake.
 
Wananchi wanaonekana kutoelema maana ya rasimu na pia maoni yao ni ya ajabu mno. Eti mmoja anazungumzia hoja za maisha binafsi badala ya mambo ya kitaifa.
Hata ivo umeme umekatika hapa uwanjani pametukia na wananchi wengine wanaondoka.

Akili yako haina akili
 
Uraia wa nchi mbili uwe haki ya mtanzania.
Mahakama iendelee kuwa na nguvu ya kusitisha matokeo ya uchaguzi mahakamani.
Ardhi iwe chini ya wananchi na sio raisi kama ilivyo kwasasa.
 
Raisi asiwe na mamlaka ya kuvunja bunge kama alivyofanya nyerere kipindi chake cha uongozi. Sababu ya kupingana na matakwa yake.
Cheo cha mkuu wa mkoa kifutwe na wilaya pia na mbadala yake iwe uongozi wa majimbo.
 
Serikali tatu ndio msimamo wa chadema ila zanzibar wakisema serikali moja chadema wapo tayari.
 
Kiongozi akistaafu asipewe uongozi tena na kwakuwa ajira ni tatizo tanzania. Limepita.
 
Huduma ya elimu iwe bora na itakuwa ya bure kutoka msingi hadi chuo kikuu. Huyo ndio slaa na cdm bwana.
 
Back
Top Bottom