Earthmover
JF-Expert Member
- Sep 28, 2012
- 25,975
- 25,288
Jamani mtoto mwingine kazaliwa anaitwa Jangili tena kashika HATAMU!!!
Huyu mzee amechuja hata mtoto hawezi akamsikiliza sasa hivi.Hana jipya zaidi ufisadi ndo single yao ambayo raia wameichoka.Chama cha kidini(CDM) lazima kife mikononi mwake
kodi zetu zilifujwa mwaka 2007 kwa ushenzi na leo tena wanaamua kuzifuja,si bora zikanunue ambulance.. mwisho wenu waja.
Kwani mafanikio au maendeleo huwa yananadiwa?Hapo kasema Facts zipi mkuu? au ndo wale wale bendera fuata upepo, madam kasema SLAA basi ni facts.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema mpango wa viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakiwamo mawaziri kuanza ziara mikoani, hauwezi kukisaidia chama hicho kujiimarisha kisiasa wala kuathiri kasi ya Chadema ya kujipanua nchi nzima.
Chama hicho kimesema CCM hawatafanikiwa kwa kuwa zimejitokeza tuhuma nzito ambazo hazijajibiwa na serikali ya CCM kwa Watanzania na hivyo kuwafanya wananchi kukosa imani na serikali ya chama hicho.
Kauli hiyo ya Chadema imekuja siku moja baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, kueleza kuwa Sekretarieti mpya ya Chama hicho inatarajia kuongozana na mawaziri kufanya ziara ya kichama mikoani kuzungumzia masuala mbalimbali ya maendeleo.
Nnauye alisema juzi kuwa katika ziara hiyo ambayo itaanza leo katika mikoa ya Mtwara, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, atakuwa akiambatana na baadhi ya mawaziri kwa ajili ya kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya CCM tangu mwaka 2010.
Hata hivyo, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, alisema ziara hiyo haiwezi kukisaidia CCM kwa sababu hata mwaka 2007 mawaziri walifanya ziara mikoani kuelezea utekelezaji wa bajeti ya kipindi hicho na bado hawakufanikiwa.
CCM leo ndiyo wameamka, sisi Chadema kama ni kufanya ziara kila siku tupo mikoani, tunakumbuka mwaka 2007 mawaziri walifanya ziara kama hiyo wakatumia fedha za walipa kodi Shilingi bilioni 2.5 na bado hawakufanikiwa, hawawezi kujibu hoja, alisema Dk. Slaa.
Dk. Slaa ambaye wakati akizungumza na NIPASHE jana alikuwa njiani akielekea mkoani Kagera kwa ziara ya kichama, alisema CCM hawawezi kuwa na majibu ya kuwatosheleza Watanzania kutokana na kashfa na tuhuma kadhaa ambazo zimejitokeza kipindi hiki ambazo serikali yake imeshindwa kujibu na hivyo kuzua maswali mengi kutoka kwa wananchi.
Alitolea mfano mwaka 2007 wakati Chadema kilipowataja kwa majina baadhi ya viongozi wa serikali na CCM kwa tuhuma za ufisadi, lakini hadi sasa hawajachukuliwa hatua za kisheria licha ya kuwapo kwa ushahidi wa kutosha ambao ungesaidia kuwatia hatiani.
Dk. Slaa alisema kashfa nyingine za hivi karibuni ambazo bado serikali ya CCM haijazijibu ni utoroshwaji wa meno ya tembo yenye thamani ya Sh. bilioni 2.24 ambayo yalikamatwa na maofisa wa bandari ya Hong Kong.
Aliongeza kuwa kashfa nyingine ambazo Watanzania wanataka majibu ni usafirishaji wa wanyama hai akiwamo twiga kwenda nje ya nchi.
Dk. Slaa alisema CCM lazima itambue kuwa kikatiba kazi ya wapinzani ni kusema na serikaki kazi yake kubwa iwe ni kujibu hoja kwa vitendo kwa kutekeleza mambo yanayokuwa yanalalamikiwa.
Wapinzani kazi yao ni kusema au kuisema serikali iliyopo madarakani, na serikali kwa upande wake inatakiwa kutekeleza mambo yanayolalamikiwa na nchi inaendelea kusonga mbele, lakini inashangaza unapoona serikali nayo inafanya propaganda za kisiasa, hii ni hatari, alisema.
Kwa mujibu wa Dk. Slaa, kama serikali itaendelea kuzungumzia propaganda za kisiasa kwa kujibu kwa maneno wapinzani badala ya kutenda kwa vitendo, nchi itaendelea kurudi nyuma kimaendeleo na wananchi wataendelea kukabiliwa na hali ngumu ya maisha.
Watanzania wanataka kujua lini CCM na serikali yake watachukua hatua za dhati kukabiliana na ufisadi, CCM wasifikiri ajenda ya ufisadi itaishia hewani hapana itakuwa ya kudumu hadi tutakapoona hatua zimechukuliwa dhidi ya wahusika, alisema
Source:Nipashe Jumatano
wa ukweli au wa kuvizia kama CHICHARITO? ha haa haaaaa, huyu mzee kweli kaishiwa.
uwiiii E MUNGU NILINI UTAIPUKUTISHA SISIEM
Hapo kasema Facts zipi mkuu? au ndo wale wale bendera fuata upepo, madam kasema SLAA basi ni facts.
Huyu SLAA mbona kazi yake ni kufuatilia tu CCM? CCM wao wamesema KINANA anafuatana na mawaziri kukagua shughuli za maendeleo, yeye anakuja na hoja kuwa CCM haitawaweza, kwani CCM wanakwenda kwenye kampeni au kukagua miradi ya maendeleo? SLAA aache kumuogopa KINANA na kuanza kuomba msaada wa wananchi kwa propaganda zake.
Huyu SLAA mbona kazi yake ni kufuatilia tu CCM? CCM wao wamesema KINANA anafuatana na mawaziri kukagua shughuli za maendeleo, yeye anakuja na hoja kuwa CCM haitawaweza, kwani CCM wanakwenda kwenye kampeni au kukagua miradi ya maendeleo? SLAA aache kumuogopa KINANA na kuanza kuomba msaada wa wananchi kwa propaganda zake.
Huyu mzee amechuja hata mtoto hawezi akamsikiliza sasa hivi.Hana jipya zaidi ufisadi ndo single yao ambayo raia wameichoka.Chama cha kidini(CDM) lazima kife mikononi mwake
Nyie nyote mnaompinga Rais wetu mtarajiawa Dr wa ukweli achana na hao Drs uchwala aka magumashi mbona hata hamzidi watatu? Hamuoni aibu tuuuuu??????Slaa ni mfamaji aishi kutapatapa
Nyie nyote mnaompinga Rais wetu mtarajiawa Dr wa ukweli achana na hao Drs uchwala aka magumashi mbona hata hamzidi watatu? Hamuoni aibu tuuuuu??????
Huyu mzee amechuja hata mtoto hawezi akamsikiliza sasa hivi.Hana jipya zaidi ufisadi ndo single yao ambayo raia wameichoka.Chama cha kidini(CDM) lazima kife mikononi mwake