Dk. Slaa Ajibu Mapigo ya CCM

CCM hofu imewajaa tu chadema hawana lengo la kuiondoa serikali madarakani kwa nguvu bali wanatoa elimu ya uraia kitu ambacho ni kazi moja wapo ya chama cha siasa. Kama wangekua na lengo la kuiondoa serikali madarakani maandamano hayo si yangekua endelevu kwa mikoa yote waliyokwisha pita! Wale wanaofananisha maandamano ya chadema na yale ya misri, tunisia, libya na bahrein ndio wachochezi namba moja.
 
Nataka kuongelea hapa kuhusu chama cha Mrema, Tanzania Labour Party, (TLP). Ukitafsiri maana ya Tanzania Labour Party kutoka kiingereza kwnda Kiswahili, maana yake ni chama cha wafanyakazi. Je, hapa nauliza, TLP kweli ni chama cha wafanyakazi? Ni mambo mangapi ambacho chama hicho kimefanya kutetea maslahi ya wafanyakazi wa Tanzania mpaka sasa? Ama kupingana na wapigania haki za Watanzania ndio malengo ya hicho chama?
 
hakili ni nywele kila mtu anazake! kwa kuwa wapambe wapo Dr slaa atavimba kichwa na kujiona shujaa,haya mshangilieni.

Kikwete na serikali yake ni lazima wajue kuwa mahala popote pasipokuwa na haki hapawezi kuwa na AMANI; sio haki hata kidogo kwa wanannchhi kutwishwa mizigo ya kulipa kodi kubwa na nyingi ili kuwanufaisha watawala wachache. Bei ya vyakula imepanda na kufanya wananchi wapate milo yao kwa shida yote hiyo ikiletwa na kodi nyingi kwenye mafuta tunayoagiza; bei ya umeme imepanda hivyo kuzifanya bidhaa zote za viwandani kupanda bei na wananchi kuumia zaidi. CCm na serikali yake wanahusika moja kwa moja na masahibu haya kwani kuwakumbatia mafisadi wanaohujumu nchi ndio kumepelekea matatizo yote haya kuwepo. Yanayofanywa na CHADEMA sio uchochezi bali kuwaumbua ccm na serikali yao juu ya madhambi wanayowafanyia wananchi.!
 

Acha woga ndugu yangu, CCM Ndiyo watakao leta vurugu, watu wanamadai yao ya msingi na wanataka mabadiliko kazi ya vyama vya siasa ni kumobileze watu katika kudai haki zao na wanadai kwa njia ya maandamano na mikutano ambayo ni haki ya kikatiba.

Hayo mambo sijui CDM wanasaidiwa hela na Repubican ya usa sidhani kama nitatizo mbona CCM wanavyama marafiki na vinatoa msaada kwa ccm na hakuna tatizo. Hata kama Dr. Amewin brain cöntrol ya wanachadema ni heri kuliköni kuwa win cöntrol na Mkwere. Kwani ni rais aliyeshindwa kuongoza nchi na na chama chake.
 
Ikiwa Walibya walipata yote hayo toka kwa Gadafi lakini wanataka kumtoa si ndiyo zaidi Sisi watanzania tunapaswa kufukuzia mbali mkwere kwani hakuna ya alichokifanya zaidi ya kuongezeka kwa umaskini ni nchini pia lazima ujue pia kuwapa watu maji, umeme , makazi na kadhalika huku ukibana haki zao na uhuru wao ni sawa na bure.
 
Mbona unalia lia kama Chiligati.
 
Kwa kila CCM itakacho kifanya dhidi ya Chadema au uongozi wake ndivyo watakavyowazidishia umaarufu.
Haki inayodaiwa ni ndogo sana. JK ni rais tena analindwa vibaya sana na katiba iliyopo, hivyo swala hapa ni kuwachukulia hatua tu viongozi wenzake waliotufikisha hapa. Maandamano ya Chadema yanatokana na kundi dogo na wahuni wachache sana ndani ya chama chao.
Swala la Dowans, wananchi wasikilizwe kama alivyowaahidi wananchi mwaka jana akisema ni swala la muda tu watalisahau.
Mafisadi kama RA na EL awaambie jamani eeeh mmeisha chuma vya kutosha nendeni Pemba au Ukerewe mkajipumzishe maanake hapa sii tu mnanivurugia jina langu ila mnakisambaratisha chama pia..
Kwa uchache huu tu, CCM itaweza kurudisha tumaini la wananchi kwao lakini wakiendelea kukumbatia udikteta kama kina Mubarak hauwezi kuwasaidia kwa lolote maanake itafikia hata wanachama wa CCM wenyewe watachoka na ufisadi unaondelea ukilindwa na dola.. Sasa sielewi, hivi kweli makosa yatakuwa ya Chadema au CCM wenyewe..
Mimi nasema hivi ikiwa hofu ya JK ni huko nyuma ktk ushirika wake na RA, na hata kama RA atamhusisha JK na lolote lile ndio kinga ya RA na EL kumfunga kamba ya mbuzi shingoni...mbinu hii haina mvuto kwa wadanganyika kwani sisi wepesi sana wa kusamehe.
JK analindwa na katiba iliyopo na kwa kumtosa RA na EL, bunge haliwezi kumwadhibu kama vile wananchi watakavyo waadhibu wote siku ya siku.. chief in command
 
Hakuna machiko ya kuwakamata na CCM na Jk wanajua walichofanya kwenye uchaguzi hivyo zote ni Kelele ila ukweli ni Kwamba CHADEMA wapo sahihi sana kwa hili
 
Sasa mimi nashindwa kuelewa, Azimio la Arusha tuliandamana sana tu. Halafu CCM ni chama chama cha kudumu, inakuwaje sasa tuaogopa CDM. Maadui wa CCM wamo ndani, wafukuzeni muone kama watu hawakuandamana nchi nzima kuwaunga mkono. Ngoja niwape kidogo List.
RS
EL
AK
MK
AC
SS

sasa kuangaika na chadema, mnapoteza muda, hatutaki watu watakaotokea nsituni, heri hawa wanaosema tu. Chonde chonde safisheni nyumba ndani. Wakafanye biashara hawa.:hand:
 
Dr Slaa

Safi sana hii, Majambazi yaliyovaa ngozi ya kondoo yakiogozwa na JK na anayejidai mtoto wa mkulima ambaye hana huruma na mpunga wa walipa kodi wanafikiri sisi watanzania hatufahamu jinsi wanavyojinufaisha. Kamwe hawawezi tena kutumia njia ile ile ya danganya toto. Lazima pachimbike na wawashughulikie Mafisadi kama kweli wanataka kuendelea kula kodi zetu. RA, EL, Chenge, BWM et al hata mtoto wa darasa la kwanza anafahamu ni wezi ndio waliotufikisha hapa bila kuwasahau Manji na makuwadi wao wa NSSF wakamatwe na kuwekwa ndani kwa kutumia sheria ya uhujumu wa uchumi.
 

Sielewi ni kwanini Dr. Slaa ana hofu ya Chadema kuadhibiwa, sielewi hii hofu yake inatoka wapi?

Na ni kwanini anadhani ni yeye na Mbowe tu ndio wanaopaswa kuchukuliwa hatua? ina maana maandamano yalikuwa ni ya Dr. Slaa na Mbowe na sio ya Chadema? ina maana ndani ya Chadema ni Dr. Slaa na Mbowe tu wenye uchungu wa kutetea umma? ina maana wale viongozi wengine wa Chadema walikuwa ni wafuata mkumbo tu kwenye hili? huku ni kuutafuta umaarufu binafsi badala ya umaarufu wa Chama na hili sio jambo zuri katika kujenga chama!!

Katibu Mkuu wa Chadema hapaswi kuridhia kwa namna yeyote kitendo chochote cha serikali kuwachukulia hatua viongozi wa Chadema kwani kama ni sahihi kuwachukuliwa hatua viongozi wa Chadema kwa viwango vyovyote ni sahihi pia kuichukulia hatua Chadema, he should know this!!
 
Nice thread,ila kuna mtu kanichekesha sana eti Makamba nae shujaa!for sure yeye mwenyewe atakushangaa ukimwita shujaa
 
hapa sasa Mh.dr Slaa kasema ukweli......

ccm wababaishaji sana
 

Rudia kusoma kwa utulivu utaelewa kaka
 
Rudia kusoma kwa utulivu utaelewa kaka
Mkuu chama ni cha wananchi, yaani watanzania wote wanaokubaliana na sera zake.. Kukifungia chama ni sawa na kukataa kuwepo kwa mrengo wa kati kushoto hivyo maadam tatizo ni maandamano ambayo yaliandaliwa na uongozi wa Chame basi wao ndio wakamatwe kama vile ukipinga CCM kwa utawala wake na ufisadi haina maana tukifungie chama madarakani CCM haina maana tukifungie chama kwa makosa ya JK na viongozi wenzake..
 

This also is supposed to be great thinking! Bwa ha ha haaa! CCM haiishiwi watetezi uchwara.
 
Kuna post nilindika baada ya bunge kuahirishwa yenye heading
Bunge la 10 na ukuta wa spika kwa serikali.

Kitendo cha kufinyanga haki za msingi za wananchi haya ndio matokeo,inatupasa wote tunaohudumia watanzania kuacha kufinyanga haki mambo yote yatakwenda sawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…