Dk. Ndungulile atetea kiti IAS

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797




na Abdallah Khamis

MBUNGE wa Kigamboni, Dk Faustine Ndungulile (CCM) amechaguliwa kuwa mwakilishi wa Bara la Afrika kwenye Taasisi ya Kimataifa ya Masuala ya Ukimwi (IAS) ambapo atashikilia nafasi hiyo kwa muda wa miaka minne.


Hiyo ni mara ya pili kwa Dk. Ndungulile kushika nafasi hiyo baada ya kipindi cha mwaka 2008 - 2012 kumalizika.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Dk. Ndungulile, ilieleza alichuana na wagombea wengine 13 kutoka nchi mbalimbali za Afrika ambazo ni Ethiopia, Nigeria, Afrika Kusini, Rwanda, Kenya, Morocco, Sudan na Misri.


Alisema majukumu ya taasisi hiyo yenye makao makuu yake Geneva, Uswisi ni pamoja na kuhamasisha njia bora na ya kisasa katika mapambano dhidi ya ukimwi, kutoa elimu na kujenga uwezo wa wataalamu wa ukimwi katika vita dhidi ya ugonjwa huo

 


Mbunge Kijana, anayetufaa na mwenye Msimamo CCM ingetakiwa Kumkumbatia na kuleta Mabadiliko ndani through yeye

Na wengine wasafi; lakini la itamkandamiza akimbie... wabaki na wale wale wabovu... WANANCHI hawasikii na kuona?

HII ILIKUWA KAZI YA NYERERE KUKIFANYA CCM KUWA NA MHURI HUU; SIDHANI HAWA WENGINE WANAJUA HAYA

WANAFURAHIYA KAZI YA JK NYERERE; NA WANASHIBA...

* Rais wetu Kikwete alikuwa Katibu wa CCM - LINDI ukimwuliza ni wanachama wangapi aliwawezesha kujiunga CCM; Hatakumbuka

Na enzi hizo ni wakati wa CHAMA KIMOJA
 
Back
Top Bottom