...labda na Kikwete atakubali hivi karibuni kwamba Ikulu yake inanuka rushwa na inaongoza kwa kupokea rushwa kuliko taasisi yoyote ile nchini.
Naelewa nachozungumza kwa kuwa tatizo si la TAKUKURU kama TAKUKURU kwani tumeunda taasisi kwa maana ya kupambana na kuzuia rushwa lakini wahusika ambao ni serikali wanachukulia poa tu kuwa support hawa jamaa kiasi kwamba mtu kiongozi kabisa anatamka hadharani 'hawa mafisadi wana nguvu na mtandao mkubwa ni kwenda nao kwa tahadhari', unategemea nini sasa hapa kwa Hosea na timu yake. Wangepewa menu na nguvu na kuweka siasa pembeni wangefanya kazi lakini hawapewi
Frankly speaking, mpaka leo sijajua hiki kitengo kilianzishwa kwa madhumuni gani....... serious!Na Bado yuko OFISINI.. Hii taasisi ni kiini macho tu maana meno yake bado hayajaota.
...labda na Kikwete atakubali hivi karibuni kwamba Ikulu yake inanuka rushwa na inaongoza kwa kupokea rushwa kuliko taasisi yoyote ile nchini.
wekeni ushahidi hapa tuwamalize mafisi hawa. tumewakabidhi bucha wakati meno yao yamechongoka wanakula hadi mifupa.Na mzito mmoja wa PCCB aliyepewa sh millioni 30 na Benki Kuu ya Tanzania wakati wa kashfa ya EPA je? Muda umefika wa kuonyesha alivyopokea na aliyempelekea. Hii ndo itakuwa funga kazi ya rushwa nchini.
Frankly speaking, mpaka leo sijajua hiki kitengo kilianzishwa kwa madhumuni gani....... serious!
Tatizo unasoma kwa jicho la seriousness sana mkuu, nimesema hao polisi wenyewe yao yamewashinda bora waongezewe na hili itaonekana wana mambo mengi kuliko kutengeneza kitu maalumu kwa ajili ya rushwa alafu linapokuja suala la kushitaki kunakuwa na muingiliano kati ya DPP na PCCB na mwisho wa siku watu wanaachiwa, natambua uwepo wao ila concern yangu wapewe meno na waachiwe wafanye kazi vingenevyo hakuna maana ya kuwa nao,Kama Polisi wameshindwa kuwa "imara" sasa hivi kwa hiyo watakuwa "imara" wakipewa kazi ya kupambana na rushwa?
Mkuu BAK na bado jamaa anakula mshahara wa nguvu wakati taasisi ya kupambana na rushwa inapokea rushwa naona tuuiite taasisi ya kupokea na kutakatisha rushwa
Serikali nzima inanuka rushwa. Mfumo mzima JK aliorithi toka kwa Mkapa na kuuendeleza na kuweka wake ndo shida ilipoanzia. Sasa hivi watu wanakimbilia serikalini kwasababu nje ya mapato yao halali kuna rushwa na upigaji kibao.
Takukuru ni sehemu ya serikali ya JK kwahiyo usitegemee miujiza ya wao kufanya vyema. Takukuru na system nzima haisafishiki hadi uingie utawala mwingine mpya na kusafisha uozo wote wa ccm.
Frankly speaking, mpaka leo sijajua hiki kitengo kilianzishwa kwa madhumuni gani....... serious!
Wala haitaji kukiri maana hilo lipo wazi. Haiwezekani kila mahali kukawa na rushwa - polisi, mahakama, serikalini (kwenye wizara mbali mbali), TAKUKURU nk lakini Ikulu ikawa safi.
Siamini kama subordinate anaweza kuwa mla rushwa kama bosi wake si mla rushwa! Huu usemi wa Hosea maana yake nini?
Dk Hoseah alisema ili kupambana na rushwa lazima Serikali iwe na uongozi bora na imara
Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini, Dk Edward Hosea.
Na Anthony Kayanda, Mwananchi
Posted Jumatano,Februari11 2015 saa 17:39 PM
Kwa ufupi
Dk Hoseah alisema wanapokea utafiti huo kama changamoto na watatumia sheria, kanuni na taratibu kuwapa adhabu watumishi watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa.
Kigoma. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imekiri kuwapo kwa baadhi ya watumishi wake wanaojihusisha na vitendo vya kupokea rushwa, hivyo kuchafua sifa ya taasisi hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kigoma jana, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hoseah alisema tuhuma zilizotolewa hivi karibuni na taasisi zilizofanya utafiti juu ya masuala ya rushwa nchini, baadhi yake zina ukweli.
Dk Hoseah alisema wanapokea utafiti huo kama changamoto na watatumia sheria, kanuni na taratibu kuwapa adhabu watumishi watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa.
Takukuru siyo malaika, iwapo nitasema hakuna kabisa rushwa ndani ya taasisi hii nitakuwa ninajidanganya kwani hili tatizo lipo sehemu zote, inawezekana maofisa wasio waadilifu wanapokea rushwa lakini ninawahakikishia kwamba tutachukua hatua kali dhidi ya yeyote atakayebainika, alisema Dk Hoseah na kuongeza:
Serikali imefanya jitihada kubwa kuhakikisha Takukuru inaboreshwa, ndiyo maana bado sielewi kwanini kuna baadhi ya watumishi wanalalamikiwa kujihusisha na ulaji rushwa, wanalipwa vizuri na kuna mazingira mazuri ya kufanya kazi. Nitafanya jitihada kuondoa changamoto hizi.
Pia, alitoa tahadhari kwa wananchi kuwa makini na matapeli wanaojitangaza kwamba wao ni maofisa wa Takukuru, hivyo kuomba rushwa kwa baadhi ya maofisa wa Serikali na watu wengine ambao wanabainika kufanya makosa yanayohusiana na ubadhirifu mbalimbali.
Dk Hoseah alisema ili kupambana na rushwa lazima Serikali iwe na uongozi bora na imara, ambao utasaidia kuweka mipango thabiti kwa maendeleo ya wananchi, kufanya mambo kwa uwazi, kuwajibika kwa umma, kuwashirikisha watu katika mipango mbalimbali na kusimamia utawala wa kisheria.
CC: Tized, Mr Rocky, Fixed Point, lyinga, NATA, Chakaza, Elly B, Ablessed, MziziMkavu, afrodenzi, Heaven on Earth, Power to the People, Jasusi, Eiyer, idawa, nguruvi, Mentor, Sikonge, Dingswayo, MANI, tpaul, Bramo, Bulesi Bulldog, Sangarara, MTAZAMO, Erythrocyte, Mag3, Mimibaba, zumbemkuu, Crashwise, amkawewe, Idimi, Ogah, Chakaza, mshana jr, JokaKuu, MWALLA, genekai, PRINCE CROWN, Tuko, Shark, lynxeffect22, samaki2011, MoudyBoka adolay, Elli, nyabhingi, Janjaweed, S.N.Jilala, MEANDU, Tabby, Candid Scope, Honolulu, August, dyuteromaikota, BONGOLALA, Gefu, Bigirita, Kozo Okamoto, Daudi Mchambuzi Kill 3
frankly speaking, mpaka leo sijajua hiki kitengo kilianzishwa kwa madhumuni gani....... Serious!
Nilitaraji Dr Hosea kujiuzulu Mara moja baada ya ripoti ile inayoonyesha pccb/Takukuru kuwa miongoni mwa taasisi za serikali zinazoongoza kwa rushwa, lakini kwa serikali hii ya chama chawala hiyo ni ndoto isiyo na tija