Wadau nimepita raiamwema nikakuta hio artcle...na yenye Kuendelea...plz fuatilia...
Swali: NSSF ya sasa, hata kwa jina, ni tofauti sana na ilivyokuwa miaka ile
wakati ulipoingia. Leo mna miradi mikubwa mnayoendesha, kama ya
ujenzi wa majumba, ni ipi ya aina hiyo inayoendelea? Mna mingapi
mingine iliyomo mbioni kuanza. Ni ya gharama gani?
Dk. Ramadhani Dau: Miradi imegawanyika katika makundi matatu; ile iliyokamilika; inayoendelea; na kundi la mwisho ni la miradi ambayo tunatarajia kuianza.
Tuliyokwisha kuimaliza ni jengo la ofisi la Mwanza (Sh. 12 bn), kuna jengo hili la Makao Makuu ya NSSF, lililokuwa Mafuta House, ambalo sasa ni Benjamin Mkapa Pension Towers (Sh. 23 bn); na kuna nyumba za Serikali ambazo zipo Kijitonyama (Sh. 13.8 bn). Kuna nyumba za Jeshi za Arusha na Dar es Salaam (Sh. 21.54 bn); kuna Hosteli ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Sh. 16.4 bn) na nyumba za kupangisha za daraja la juu za Mikocheni, Dar es Salaam (Sh. 2.6) na jengo lililokuwa la Nasaco, sasa Waterfront; jengo la ofisi Mtwara; nyumba za bei nafuu za Kinyerezi, Dar es Salaam, Hospitali ya Mkuranga na majengo ya ofisi Nzega na Mafinga.
Ukiacha hayo kuna jengo la Ubungo Plaza ambalo tumejenga kwa pamoja na Shirika la Nyumba (NHC) kwa kushirikiana na Mfuko wa Pensheni wa Serikali na pia kuna ukumbi wa Bunge, Dodoma ambao tumeshirikiana na mifuko yote ya Pensheni nchini.
Miradi inayoendelea ni ofisi za Bukoba zilizogharimu shilingi bilioni 2.88; jengo la ofisi Mbozi lililogharimu shilingi milioni 450; kuna jengo maarufu la Machinga la Dar es Salaam la gharama ya shilingi bilioni 12.41 litakalokwisha Desemba hii na jengo la Makao Makuu ya TAKUKURU la gharama ya shilingi bilioni 3.84.
Kuna pia hosteli tano za Chuo Kikuu Kishiriki cha Sanaa na Sayansi ya Jamii cha Chuo Kikuu cha Dodoma za gharama ya bilioni 32; kuna nyumba za Jeshi la Polisi za Pemba, Unguja na Dar es Salaam na hosteli, madarasa, kumbi za mihadhara na majengo ya huduma nyingine za Chuo Kikuu Kishiriki cha Sanaa na Sayansi ya Jamii cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam vya gharama ya shilingi bilioni 56.
Hivi karibuni tutakuwa na majengo ya ofisi na vitega uchumi katika Mikoa ya Kigoma na Arusha na katika Wilaya za Kahama na Njombe; jengo la kitega uchumi la iliyokuwa AISCO Dar es Salaam, nyumba za kuuza za Mtoni Kijichi na Kigamboni na vilevile daraja la Kigamboni.
Tuna mipango pia ya kuanzisha mradi wa ujenzi wa Business Industrial Park, ambayo uwezekano mkubwa ni kwamba tutajenga pale Kunduchi, Dar es Salaam kwenye eneo la machimbo ya kokoto. Wazo kuu la kuanzisha eneo hilo ni kwamba pale katika Jengo la Machinga, Karume, mtu ananunua viatu au soksi anakwenda pale anauza, ni shughuli za kununua na kuuza.
Pale Kunduchi tunataka kiwango kipande, badala ya kununua na kuuza, wawe na uwezo wa kuunda vitu. Kwa mfano, ananunua soli na ngozi anaunda kiatu. Ananunua mbao anapiga randa anaunganusha meza, anauza, na kwa maana hiyo, anaweza kuwa na watu wengine wawili au watatu. Sisi tutatoa huduma za maji, na miundombinu nyingine pamoja na majengo yenyewe.
Endelea mwenyewe.....
Raia Mwema - Dk. Dau: NSSF inastawisha maendeleo
Maoni yangu...kwa Haya machache waliyoyafanya NSSF ni mambo mazuri na ni ya kupongezwa na kutiwa nguvu ili waweze endelea na kuwekeza ktk Vitega uchumi vya mda mrefu.
Binafsi yangu, ujenzi wa Nyumba TZ umekuwa Hovyo MNO, kwa style ya NSSF ya kujenga nyumba za bei nafuu ni jambo ambalo lingekuwa vyema likawa so tu NSSF, bali unakuwa mpango wa serikali nzima. Hili lingepunguza Ujenzi wa Mabondeni, na Ujenzi wa kiholela usio ktk Master Plan ya Miji.
Last natoa Pongezi kwa Dr. Dau na wengine wote wanaosimamia maendeleo huko NSSF... Usikate tamaa wala usikatishwe tamaa...Kama mie ningekuwa mshauri wako, basi Uwekezaji wote ungekuwa ktk REAL Estate... nchi nzima...Nchi ingependeza. na Inalipa sio SIRI..!!!
Swali: NSSF ya sasa, hata kwa jina, ni tofauti sana na ilivyokuwa miaka ile
wakati ulipoingia. Leo mna miradi mikubwa mnayoendesha, kama ya
ujenzi wa majumba, ni ipi ya aina hiyo inayoendelea? Mna mingapi
mingine iliyomo mbioni kuanza. Ni ya gharama gani?
Dk. Ramadhani Dau: Miradi imegawanyika katika makundi matatu; ile iliyokamilika; inayoendelea; na kundi la mwisho ni la miradi ambayo tunatarajia kuianza.
Tuliyokwisha kuimaliza ni jengo la ofisi la Mwanza (Sh. 12 bn), kuna jengo hili la Makao Makuu ya NSSF, lililokuwa Mafuta House, ambalo sasa ni Benjamin Mkapa Pension Towers (Sh. 23 bn); na kuna nyumba za Serikali ambazo zipo Kijitonyama (Sh. 13.8 bn). Kuna nyumba za Jeshi za Arusha na Dar es Salaam (Sh. 21.54 bn); kuna Hosteli ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Sh. 16.4 bn) na nyumba za kupangisha za daraja la juu za Mikocheni, Dar es Salaam (Sh. 2.6) na jengo lililokuwa la Nasaco, sasa Waterfront; jengo la ofisi Mtwara; nyumba za bei nafuu za Kinyerezi, Dar es Salaam, Hospitali ya Mkuranga na majengo ya ofisi Nzega na Mafinga.
Ukiacha hayo kuna jengo la Ubungo Plaza ambalo tumejenga kwa pamoja na Shirika la Nyumba (NHC) kwa kushirikiana na Mfuko wa Pensheni wa Serikali na pia kuna ukumbi wa Bunge, Dodoma ambao tumeshirikiana na mifuko yote ya Pensheni nchini.
Miradi inayoendelea ni ofisi za Bukoba zilizogharimu shilingi bilioni 2.88; jengo la ofisi Mbozi lililogharimu shilingi milioni 450; kuna jengo maarufu la Machinga la Dar es Salaam la gharama ya shilingi bilioni 12.41 litakalokwisha Desemba hii na jengo la Makao Makuu ya TAKUKURU la gharama ya shilingi bilioni 3.84.
Kuna pia hosteli tano za Chuo Kikuu Kishiriki cha Sanaa na Sayansi ya Jamii cha Chuo Kikuu cha Dodoma za gharama ya bilioni 32; kuna nyumba za Jeshi la Polisi za Pemba, Unguja na Dar es Salaam na hosteli, madarasa, kumbi za mihadhara na majengo ya huduma nyingine za Chuo Kikuu Kishiriki cha Sanaa na Sayansi ya Jamii cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam vya gharama ya shilingi bilioni 56.
Hivi karibuni tutakuwa na majengo ya ofisi na vitega uchumi katika Mikoa ya Kigoma na Arusha na katika Wilaya za Kahama na Njombe; jengo la kitega uchumi la iliyokuwa AISCO Dar es Salaam, nyumba za kuuza za Mtoni Kijichi na Kigamboni na vilevile daraja la Kigamboni.
Tuna mipango pia ya kuanzisha mradi wa ujenzi wa Business Industrial Park, ambayo uwezekano mkubwa ni kwamba tutajenga pale Kunduchi, Dar es Salaam kwenye eneo la machimbo ya kokoto. Wazo kuu la kuanzisha eneo hilo ni kwamba pale katika Jengo la Machinga, Karume, mtu ananunua viatu au soksi anakwenda pale anauza, ni shughuli za kununua na kuuza.
Pale Kunduchi tunataka kiwango kipande, badala ya kununua na kuuza, wawe na uwezo wa kuunda vitu. Kwa mfano, ananunua soli na ngozi anaunda kiatu. Ananunua mbao anapiga randa anaunganusha meza, anauza, na kwa maana hiyo, anaweza kuwa na watu wengine wawili au watatu. Sisi tutatoa huduma za maji, na miundombinu nyingine pamoja na majengo yenyewe.
Endelea mwenyewe.....
Raia Mwema - Dk. Dau: NSSF inastawisha maendeleo
Maoni yangu...kwa Haya machache waliyoyafanya NSSF ni mambo mazuri na ni ya kupongezwa na kutiwa nguvu ili waweze endelea na kuwekeza ktk Vitega uchumi vya mda mrefu.
Binafsi yangu, ujenzi wa Nyumba TZ umekuwa Hovyo MNO, kwa style ya NSSF ya kujenga nyumba za bei nafuu ni jambo ambalo lingekuwa vyema likawa so tu NSSF, bali unakuwa mpango wa serikali nzima. Hili lingepunguza Ujenzi wa Mabondeni, na Ujenzi wa kiholela usio ktk Master Plan ya Miji.
Last natoa Pongezi kwa Dr. Dau na wengine wote wanaosimamia maendeleo huko NSSF... Usikate tamaa wala usikatishwe tamaa...Kama mie ningekuwa mshauri wako, basi Uwekezaji wote ungekuwa ktk REAL Estate... nchi nzima...Nchi ingependeza. na Inalipa sio SIRI..!!!