Dk. Chegeni|Mgeja|Chizi wajitosa CCM

sir.JAPHET

JF-Expert Member
May 18, 2012
699
133
Jumamosi, Agosti 25, 2012 06:43 Na Waandishi Wetu, Dar na Mikoani

HARAKATI za kuwania uongozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), zimeshika kasi baada ya makada wa chama hicho, kuendelea kujitokeza kuchukua fomu.

Uchaguzi wa ndani wa CCM, umewaibua makada wa chama hicho, akiwemo aliyekuwa Mbunge wa zamani wa Misungwi Dalali Shibiriti ambaye amechukua fomu ya kuwania Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa(NEC) kupitia wilaya hiyo.

Akizungumza na MTANZANIA, baada ya kuchukua fomu hiyo Shibiriti, alitamba kuibuka kidedea huku akiahidi kuzaliwa upya kwa CCM Misungwi.

Wakati Shibiriti akichukua fomu, Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM), jimbo la Busega umemshinikiza aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Dk. Raphael Chegeni achukue fomu za kuwania kiti cha Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa(NEC), kupitia wilaya ya Busega.

Vijana hao, ambao waliongozwa na Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Busega, Samwel Ngofilo walimchukulia fomu na kumpelekea Dk. Chegeni nyumbani kwake kwa maandamano.

"Dk. Chegeni ni mwana Busega wa kweli, akiwa mbunge alifanya kazi kubwa katika kulijenga jimbo letu, tuna hakika atatusikiliza kilio chetu na kujaza fomu tuliyomchukulia na kuzirejesha kabla ya muda kuisha kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi,” alisema Ngofilo.

Mgeja aibuka kutetea nafasi yake

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja amewataka wanachama wa CCM, kufanya uchaguzi wa kistarabu, badala ya kupakana matope .

Mgeja aliyasema hayo jana, baada ya kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo kwa mara ya pili.

Aliwataka wagombea wenzake watakao chukua fomu kufanya uchaguzi, bila malumbano na badala yake wajenge hoja ambazo zitakuwa hazina madhara kwa chama hicho.

“Ndugu zangu, chanzo cha makundi ndani ya CCM ni mpasuko unaosababishwa na uchaguzi nawaomba wenzangu tuwe wastarabu.

Matson Chizzi

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) makao makuu, Mattson Chizzi amejitosa kwa kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Uenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar e Salaam.

Katibu Msaidizi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Adam Makulilo aliwaambia waandishi wa habari mjini Dar es Salaam, jana kuwa Chizzi alichukua fomu za kugombea nafasi hiyo na kufanya wagombea wa nafasi hiyo, hadi sasa kuwa sita mpaka kufikia jana mchana.

Wengine waliochukua fomu, ni Mwenyekiti wa sasa John Guninita, Ramadhan Madabida ,Omary Kimbau, Isaya Christabera na Rashidi Kakozi.

Katika hatua nyingine, mgombea wa nafasi ya Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa, Amos Kabis amesema endapo atachaguliwa kushika nyadhifa hiyo atahakikisha anawasimamia viongozi wa serikali katia kutekeleza ilani ya chama hicho.

Katika hatua nyingine,jumla ya wagombea zaidi ya ya 41 wamechukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali katika kinyang’anyiro hicho, huku uchukuaji ukitarajia kufungwa Agosti 29, mwaka huu.

Habari hii imeandaliwa na John Maduhu, Mwanza, Neema sawaka, Shinyanga na Simon Nyalobi, Dar es Salaam

[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]
 
Jumamosi, Agosti 25, 2012 06:43 Na Waandishi Wetu, Dar na Mikoani

HARAKATI za kuwania uongozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), zimeshika kasi baada ya makada wa chama hicho, kuendelea kujitokeza kuchukua fomu.

Uchaguzi wa ndani wa CCM, umewaibua makada wa chama hicho, akiwemo aliyekuwa Mbunge wa zamani wa Misungwi Dalali Shibiriti ambaye amechukua fomu ya kuwania Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa(NEC) kupitia wilaya hiyo.

Akizungumza na MTANZANIA, baada ya kuchukua fomu hiyo Shibiriti, alitamba kuibuka kidedea huku akiahidi kuzaliwa upya kwa CCM Misungwi.

Wakati Shibiriti akichukua fomu, Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM), jimbo la Busega umemshinikiza aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Dk. Raphael Chegeni achukue fomu za kuwania kiti cha Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa(NEC), kupitia wilaya ya Busega.

Vijana hao, ambao waliongozwa na Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Busega, Samwel Ngofilo walimchukulia fomu na kumpelekea Dk. Chegeni nyumbani kwake kwa maandamano.

"Dk. Chegeni ni mwana Busega wa kweli, akiwa mbunge alifanya kazi kubwa katika kulijenga jimbo letu, tuna hakika atatusikiliza kilio chetu na kujaza fomu tuliyomchukulia na kuzirejesha kabla ya muda kuisha kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi,” alisema Ngofilo.

Mgeja aibuka kutetea nafasi yake

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja amewataka wanachama wa CCM, kufanya uchaguzi wa kistarabu, badala ya kupakana matope .

Mgeja aliyasema hayo jana, baada ya kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo kwa mara ya pili.

Aliwataka wagombea wenzake watakao chukua fomu kufanya uchaguzi, bila malumbano na badala yake wajenge hoja ambazo zitakuwa hazina madhara kwa chama hicho.

“Ndugu zangu, chanzo cha makundi ndani ya CCM ni mpasuko unaosababishwa na uchaguzi nawaomba wenzangu tuwe wastarabu.

Matson Chizzi

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) makao makuu, Mattson Chizzi amejitosa kwa kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Uenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar e Salaam.

Katibu Msaidizi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Adam Makulilo aliwaambia waandishi wa habari mjini Dar es Salaam, jana kuwa Chizzi alichukua fomu za kugombea nafasi hiyo na kufanya wagombea wa nafasi hiyo, hadi sasa kuwa sita mpaka kufikia jana mchana.

Wengine waliochukua fomu, ni Mwenyekiti wa sasa John Guninita, Ramadhan Madabida ,Omary Kimbau, Isaya Christabera na Rashidi Kakozi.

Katika hatua nyingine, mgombea wa nafasi ya Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa, Amos Kabis amesema endapo atachaguliwa kushika nyadhifa hiyo atahakikisha anawasimamia viongozi wa serikali katia kutekeleza ilani ya chama hicho.

Katika hatua nyingine,jumla ya wagombea zaidi ya ya 41 wamechukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali katika kinyang’anyiro hicho, huku uchukuaji ukitarajia kufungwa Agosti 29, mwaka huu.

Habari hii imeandaliwa na John Maduhu, Mwanza, Neema sawaka, Shinyanga na Simon Nyalobi, Dar es Salaam

[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]

Hivi kumbe nafasi ya ukatibu itikadi,siasa na uenezi ni ya kugombea?au ni ngazi ya mkoa na taifa ni mteule?
 
kitendo cha waislamu kugomea sensa ni rais wa tz ndiye wa kulaumiwa sababu sheikh ponda ni muumini mwenzake rais na anashindwa kuwachukulia hatua kama alivyofanya kwa mgomo wa madaktari na walimu huu ni uzembe na udhaifu wa kikkwete kama rais anaweka dini mbele kuliko taifa anaamini katika hilo ushahidi upo mwingi.na kama taifa hili litaingia kwenye vita ya kidini kiongozi atakayebeba mzogo huu ni jakaya kikwete.kama angelikuwa ni mchungaji mtikila kasema wakristo wasusie sensa basi manyang'au wa usalama wa taifa na polisi wangeshamuweka ndani mtikila sasa kikwete acha udini na ongoza taifa kwa misingi ya uongozi na si vinginevyo ubaguzi wa kidini utazikwa nao hata ukienda kaburini maan wewe ndie muanzilishi n​a unaendekeza.
 
Back
Top Bottom