Diwani wa CCM Arusha aongoza maandamano kupinga posho za wabunge huku wamevaa magunia

EasyFit

JF-Expert Member
Jul 4, 2011
1,269
1,082
WANANCHI wa Manispaa ya Arusha, bila kujali itikadi zao za kisiasa, jana waliandamana kwa amani wakiwa peku huku wamevaa magunia kupinga ongezeko la posho za wabunge na kutishia kuandamana hadi mjini Dodoma iwapo Rais Jakaya Kikwete ataidhinisha ongezeko hilo.

Wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali, wananchi hao walisema ni udhaifu wa Rais kukubali posho hizo zianzwe kulipwa kwa wabunge kabla hajasaini kama sheria inavyoelekeza na kumtaka kuchukua hatua kali dhidi ya wote waliohusika na ukiukwaji huo wa sheria za nchi alizoahidi kuzilinda katika kiapo chake.

“Iwapo kweli tayari wabunge wamejilipa posho hizo bila Rais kuidhinisha na hadi sasa hakuna mtu amewajibishwa, basi atakuwa ameonyesha udhaifu mkubwa kiuongozi, tutaandamana nchi nzima kupinga posho hizi bila kujali itikadi zetu kisiasa,” alisema Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya maandamano hayo, Mawazo Alphonce

Wakizungumza na waandishi wa habari mara baada ya maandamano hayo ya kilomita Saba, Mawazo ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Wazalendo Associate ya mjini Arusha, na Katibu wake, John Mchasu walisema kitendo cha Spika wa Bunge, Anne Makinda kutetea posho hizo ni kielelezo cha ubinafsi unaoonyeshwa na viongozi nchini.
“Spika kutetea posho hizo kuwa zitasaidia wabunge wake kuacha kuwa omba omba imetia doa nishani aliyotunikiwa na ni kielelezo cha ubinafsi na matumizi mabaya ya rasilimali za taifa kwa kundi moja dogo kujihalalishia mgawo mkubwa wa keki ya Taifa huku kundi kubwa likibaki bila matumaini,” alisema Mawazo.

Mawazo ambaye ni diwani wa Kata ya Sombetini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisema Spika alipaswa kuwakumbuka na kuwazungumzia makundi mengine yanayotaabika kwa kipato kidogo na ugumu wa maisha kama walimu, wauguzi, madaktari na omba omba waliozagaa kila sehemu nchini, badala ya kutetea posho za wabunge wenye kipato kinachokadiriwa kufikia milioni 12 kwa mwezi.

Alisema ubunge sasa siyo wito wala uwakilishi wa umma bali ni fursa ya kujitajirisha ndiyo maana siku hizi watu wanauza rasilimali zao kufanikisha kushinda ubunge na ndiyo maana wakishaingia bungeni wanaanza kutetea ongezeko la posho kama inavyoshuhudiwa hivi sasa.Alihoji uhalali wa wabunge kudai nyongeza ya posho wakati malipo yao kwa siku mbili ni zaidi ya mshahara wa mwezi mzima wa mwalimu na watumishi wengine wa kada ya chini serikalini.

Alitaja baadhi ya ishara za ubinafsi na matumizi mabaya ya madaraka kuwa ni kitendo cha viongozi wengi, watoto wao, ndugu, jamaa na marafiki kuishi maisha ya anasa na ufahari mara tu baada ya kuingia madarakani akitoa mfano wa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alivyoongoza kwa uadilifu kiasi cha kushindwa hata kujenga nyumba hadi alipojengewa na serikali baada ya kustaafu.

Kuhusu kuvaa magunia na kutembea peku kwenye lami lenye joto kali mchana Saa 7:00, Mawazo alisema ni ujumbe unaowakumbusha jamii kusimama imara kupinga na kuzuia malipo ya kufuru na posho zisizo na maelezo ya kutosha na kuongeza kuwa katika siku zijazo hali hii ikiendelea maisha ya watanzania yatakuwa magumu na hawatamudu kununua hata nguo wala malapa kutokana na viongozi kujigawia keki yote ya taifa.

Moja ya mabango yaliyobebwa na watoto walioshiriki maandamano hayo lilisomeka “Wakati wabunge wanadai posho zaidi, watoto hatuna madawati, tunakaa chini kwenye mavumbi hivyo tunalaani nyongeza hizo,”

Diwani huyo ambaye kabla ya kuhamia CCM alikuwa katika Chama cha Tanzania Labour alikoshinda udiwani wa Sombetini alisema wako tayari kuandamana hadi Dodoma hata ikibidi kuuawa kwa kupigwa risasi kwani hata wakifa watafia ukombozi wa jamii iliyochoka kimaisha kutokana na viongozi wengi kujali maslahi binafsi badala ya umma wanaouongoza.
 
Hivi maziko ya CCM ni lini jamani maana naona kihi chama kimesha kufa......
 
kuomboleza kwa kuvaa magunia ni ishara kubwa sana kwa kati ya mungu na mwanadamu, taifa limepelekwa kusiko ee MOLA sikia kilio cha waja wako utawala huu uwe na hofu ya MUNGU.
 
Kuvaa magunia inamaanisha nini ?
Ogopa sana kitu kiitwacho kuvaa magunia, maana kinaashiria maombolezo
mbele za MUNGU ya hali ya juu sana. CCM wangekuwa wakijua maana yake
wangeyapiga marufuku kabisa. Nilipoona jana ktk TV nikaona safari kubwa
imeaanza, TANGU TUPATE UHURU SIJAWAHI ona waTZ wakilia kilio hiki.
TAFAKARI: K
UVAA MAGUNIA NA KULIA MBELE ZA MUNGU SIO KITU CHA KAWAIDA
kuna kitu kikubwa kinakuja. TAFAKARI
 
Mimi naona taabu sana pale ambapo mtaalamu aliyeteseka kwa miaka mingi kusomea kazi yake, na baada ya kupata ajira anaendelea kufanya kazi ngumu ktk mazingira magumu na analipwa kidogo na baada ya kustaafu analipwa mafao yasiyofaa kwa mda usiofaa baada ya kusota sana. Lakini mwanasiasa analipwa babu kubwa na mafao yake anapata kabla hajatoka kwa ofisi. Je tutafika? Ona sasa watoto wengi wanakosa motisha wa kusoma masomo ya SCIENCE! Je tutafika?
 
WANANCHI wa Manispaa ya Arusha, bila kujali itikadi zao za kisiasa, jana waliandamana kwa amani wakiwa peku huku wamevaa magunia kupinga ongezeko la posho za wabunge na kutishia kuandamana hadi mjini Dodoma iwapo Rais Jakaya Kikwete ataidhinisha ongezeko hilo.

Wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali, wananchi hao walisema ni udhaifu wa Rais kukubali posho hizo zianzwe kulipwa kwa wabunge kabla hajasaini kama sheria inavyoelekeza na kumtaka kuchukua hatua kali dhidi ya wote waliohusika na ukiukwaji huo wa sheria za nchi alizoahidi kuzilinda katika kiapo chake.

"Iwapo kweli tayari wabunge wamejilipa posho hizo bila Rais kuidhinisha na hadi sasa hakuna mtu amewajibishwa, basi atakuwa ameonyesha udhaifu mkubwa kiuongozi, tutaandamana nchi nzima kupinga posho hizi bila kujali itikadi zetu kisiasa," alisema Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya maandamano hayo, Mawazo Alphonce

Wakizungumza na waandishi wa habari mara baada ya maandamano hayo ya kilomita Saba, Mawazo ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Wazalendo Associate ya mjini Arusha, na Katibu wake, John Mchasu walisema kitendo cha Spika wa Bunge, Anne Makinda kutetea posho hizo ni kielelezo cha ubinafsi unaoonyeshwa na viongozi nchini.
"Spika kutetea posho hizo kuwa zitasaidia wabunge wake kuacha kuwa omba omba imetia doa nishani aliyotunikiwa na ni kielelezo cha ubinafsi na matumizi mabaya ya rasilimali za taifa kwa kundi moja dogo kujihalalishia mgawo mkubwa wa keki ya Taifa huku kundi kubwa likibaki bila matumaini," alisema Mawazo.

Mawazo ambaye ni diwani wa Kata ya Sombetini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisema Spika alipaswa kuwakumbuka na kuwazungumzia makundi mengine yanayotaabika kwa kipato kidogo na ugumu wa maisha kama walimu, wauguzi, madaktari na omba omba waliozagaa kila sehemu nchini, badala ya kutetea posho za wabunge wenye kipato kinachokadiriwa kufikia milioni 12 kwa mwezi.

Alisema ubunge sasa siyo wito wala uwakilishi wa umma bali ni fursa ya kujitajirisha ndiyo maana siku hizi watu wanauza rasilimali zao kufanikisha kushinda ubunge na ndiyo maana wakishaingia bungeni wanaanza kutetea ongezeko la posho kama inavyoshuhudiwa hivi sasa.Alihoji uhalali wa wabunge kudai nyongeza ya posho wakati malipo yao kwa siku mbili ni zaidi ya mshahara wa mwezi mzima wa mwalimu na watumishi wengine wa kada ya chini serikalini.

Alitaja baadhi ya ishara za ubinafsi na matumizi mabaya ya madaraka kuwa ni kitendo cha viongozi wengi, watoto wao, ndugu, jamaa na marafiki kuishi maisha ya anasa na ufahari mara tu baada ya kuingia madarakani akitoa mfano wa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alivyoongoza kwa uadilifu kiasi cha kushindwa hata kujenga nyumba hadi alipojengewa na serikali baada ya kustaafu.

Kuhusu kuvaa magunia na kutembea peku kwenye lami lenye joto kali mchana Saa 7:00, Mawazo alisema ni ujumbe unaowakumbusha jamii kusimama imara kupinga na kuzuia malipo ya kufuru na posho zisizo na maelezo ya kutosha na kuongeza kuwa katika siku zijazo hali hii ikiendelea maisha ya watanzania yatakuwa magumu na hawatamudu kununua hata nguo wala malapa kutokana na viongozi kujigawia keki yote ya taifa.

Moja ya mabango yaliyobebwa na watoto walioshiriki maandamano hayo lilisomeka "Wakati wabunge wanadai posho zaidi, watoto hatuna madawati, tunakaa chini kwenye mavumbi hivyo tunalaani nyongeza hizo,"

Diwani huyo ambaye kabla ya kuhamia CCM alikuwa katika Chama cha Tanzania Labour alikoshinda udiwani wa Sombetini alisema wako tayari kuandamana hadi Dodoma hata ikibidi kuuawa kwa kupigwa risasi kwani hata wakifa watafia ukombozi wa jamii iliyochoka kimaisha kutokana na viongozi wengi kujali maslahi binafsi badala ya umma wanaouongoza.
kwa nini awe diwani sasa hivi nasi lema (mbuge)? au amewageuka? nyie machalii wa arusha imekula kwenu. pole.
 
kwa nini awe diwani sasa hivi nasi lema (mbuge)? au amewageuka? nyie machalii wa arusha imekula kwenu. pole.

huwaambii kitu na Lema wao! Pata historia ya Lema kabla ya kuwa mbunge kwa mkazi yeyote wa Arusha...
 
Kuvaa magunia inamaanisha nini ?

Well, a good question!
Kuvaa gunia inamaanisha kwamba, Wananchi wamekata tamaa, na hawana matarajio na wamekosa imani na uhakika wa kesho yao. Inaashiria hawana uhakika kama kesho wataweza kupata kipaato na kununua nguo ya kuvaa na hivyo watavaa magunia, wanaonyesha namna ya nchi ilivyoshindwa kusimama na hivyo kuwa kama gunia, bila kulishikilia haliwezi simama. Gunia halina mawazo wala fikra, gunia ni tupu, gunia halifikiri na gunia halina maamuzi, kwahiyo waandamanaji wanawakilisha gunia na viongozi wa Tz, gunia halifuliwi, kwa hiyo gunia ni chavu na limechoka, hiyo ndiyo tanzania yetu. Tanzania ni gunia
 
Nasikia hii mbinu ya kuvaa magunia ibuniwa na Nape baada ya CCM kupoteza umaarufu Arusha, hivi washona suti au makombati.
 
Back
Top Bottom