Yote haya mimi nimeshayasema mara nyingi tu humu likiwemo la IDs ambazo watu tunatumia humu.
Wangapi humu wamo kwenye ndoa na wenza wao wa hizo ndoa hawazijui ID(s) zao za humu, achilia mbali kujua hata kama wamo humu? Kuna uwezekano kabisa wa mume na mke wote wakawemo humu lakini kila mmoja wao anadhani mwenzake hayumo humu na/au hata haijui kabisa JF!!!!
Au hata kama wanazijua, wanazijua ngapi (ukiingiza katika mlinganyo uwezo wa kuwa nazo zaidi ya moja)?
Wangapi humu wanachiti kihisia na watu wa humu humu?
Ndiyo maana mimi naamini kabisa kuwa, kwanza, binadamu kwa asili tu, ana kiwango kikubwa tu cha kutokuwa mwaminifu (katika suala au jambo lolote lile). Pili, mtu anapohakikishiwa au anapojihakikishia kuwa kuna faragha, ana uwezo wa kufanya lolote lile pasipo kuathiriwa na hali yake ya kimahusiano ya kimapenzi.
Pia, hii makala inaipa nguvu ile hoja ya 'kama huna la kuficha, kwa ufanye yote hayo ikiwemo kutokumruhusu mwenza wako ashike au atumie hiyo simu yako'?
Poleni mlioko kwenye ndoa!