Diamond Platinumz atoa Tsh. Milioni 37 kwa producer Bakteria kwa ajili ya Matibabu

Diamond Platinumz atoa Tsh. Milioni 37 kwa producer Bakteria kwa ajili ya Matibabu

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Star wa muziki, Diamond Platnumz, ameamua kutumia siku yake ya kuzaliwa kutoa msaada wa kiasi cha TSh 37 milioni kwa Producer Bakteria, ambaye kwa sasa anapitia changamoto za kiafya baada ya kupooza na kulazimika kukaa kitandani kwa zaidi ya miaka miwili.

Soma: Diamond Platinumz ampa milioni 10 Mzee Makosa, aliyekuwa tajiri mkubwa Iringa na kufilisika

Pia, Diamond alimpongeza Producer S2kizzy (Zombie) kwa moyo wa upendo aliouonyesha hivi karibuni alipofunga safari hadi Tanga kwenda kumjulia hali Bakteria na kumsaidia.

Producer Bakteria ni miongoni mwa vijana waliokuwa na mchango mkubwa katika kazi za muziki kupitia productions zake, lakini familia yake imekumbwa na changamoto kubwa kutokana na hali yake ya kiafya, hali iliyomfanya kushindwa kuendelea na kazi.






1759387518318.png
 
Wenye roho mbaya na waumini wa dhambi, ndiyo huonekana wema katika matatizo, kwahiyo hiyo pesa asingetoa kama siku yake ya kuzaliwa ingekuwa bado haijafika, inasikitisha sana hii...
 
Wenye roho mbaya na waumini wa dhambi, ndiyo huonekana wema katika matatizo, kwahiyo hiyo pesa asingetoa kama siku yake ya kuzaliwa ingekuwa bado haijafika, inasikitisha sana hii...
Hilo tukio la huyo producer limetokea before ya hata haijafika siku yake ya kuzaliwa na akaidiwa atasaidia na baadhi ya gharama kashatoa sema siku yake ya kuzaliwa ndio kaongezea dau kutokana na ugonjwa wake unahitajika kwenda India kwa matibabu zaidi
 
Hilo tukio la huyo producer limetokea before ya hata haijafika siku yake ya kuzaliwa na akaidiwa atasaidia na baadhi ya gharama kashatoa sema siku yake ya kuzaliwa ndio kaongezea dau kutokana na ugonjwa wake unahitajika kwenda India kwa matibabu zaidi
Umesahau huyu kiumbe ndiye aliyetuita mbuzi juzi kati kwamba hatufanyi kazi kwa bidii badala yake tunapiga kelele hovyo...
 
Umesahau huyu kiumbe ndiye aliyetuita mbuzi juzi kati kwamba hatufanyi kazi kwa bidii badala yake tunapiga kelele hovyo...
Hoja yake ilikuwa sahihi ila alikosea namna alivyowasilisha na pia alishindwa kusoma mazingira ya wakati anawasilisha hoja je yanaruhusu kuongea vile
 
Inaonekana unamuhusudu sana huyo jamaa, atuvunjie heshima halafu bado unamuelewa.
Mkuu huwa Sina mihemko ndio maana mpaka Leo huwa Sina chama cha siasa ninachoshabikia maana vyama vinataka uwe Team sifia na Mimi sio hulka yangu.sasa tuje kwenye mjadala kwanini nimesema hoja iko sahihi? Mkuu kwenye maisha yetu Kama ufanyi Kazi kwa bidii huwezi kufanikiwa hata kidogo hata yeye mpaka amefikia hapo halipo kwasababu ya kufanya kazi, kwa mujibu wake ameshauza makopo, ameshauza nguo za mitumba, ameshafanya kazi kwa wachina lakini amekuja kujipata kwenye mziki na aliwakuta wasanii wakubwa wengi hatimaye yeye akawa mkubwa zaidi yao Je angekuwa hajitumi unafikiri angekuwa hapo halipo? Ngoja niende kwenye hoja ya pili kwanini nimesema uwasilishwaji wake haukuwa mzuri ni kwasababu aliwasilisha kwa jazba pia kuingiza siasa hapo ndio alipokosea kusema watu hawatakiwi kulalamikia serikali,hoja yangu ya tatu ni alishindwa kusoma mazingira hapa nilikuwa namaanisha kaongea wakati tupo kwenye kipindi cha uchaguzi watu wapo kwenye itikadi Kali za kisiasa sio busara kuongea vile lakini kusema watu wafanye kazi hapa haujakosea kabisa shida tu ni hayo Mambo mawili niliyoeleza
 
jux na domo na wasanii wengine CCM wanawapa pesa sana
 
Una maana gani, funguka ueleweke
Siku ukiumwa ndiyoo utaelewa, watakao kuja kukutembelea ni watu wa aina mbili tu, 1 anaekujali, kukupenda na kuona thamani ya uwepo wako, 2 mnafiki, huyu huwa hakosi katika matukio yote yanayokuhusu wewe, iwe katika shida au raha yeye huwepo, hao wengine wanaobaki huwa wapo katikati hawakuchukii wala kukupenda, hawafurahi kukuona wala hawachukizwi kukuona, kwao kila kitu ni sawa, hawakuoni kuwa ni mtu mwenye faida wala hasara kwao, hivyo hata ukiumwa kwao ni kawaida tu, mara nyingi huwa ni ngumu kuonekana katika matukio hivyo wao ndiyo huonekana hawafai.
 
Ni jambo jema na uungwana kusaidiana kama binadamu, abarikiwe
 
Back
Top Bottom