Nitacomment kama mtu wa kawaida tu ninaependa muziki. Sina ushabiki wa kuegemea upande fulani kwa sababu kufanya hivyo hakuna tija kwangu. Diamond ni mwanamuziki mzuri na kushirikiana na hili kundi la Mafikizolo katika huo wimbo wa Colors of Africa ni hatua kubwa kwani mbali na kuzidi kujitangangaza kimataifa yeye kama yeye lakini pia ni heshima kubwa kwa taifa letu.
Kwa ujumla wimbo na video mimi nimeona ni ya kawaida sana. Midundo na video ya Make Me Sing aliyoshirikiana na Aka ni nzuri zaidi ya hii. Huo ni mtazamo wangu.