Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,317
Habari za wakati huu JamiiForums.
Kwanza kabisa ninaomba ieleweke kwa kila mmoja wetu ya kwamba, Tanzania ililazimika kupigana vita ya Kagera mwaka 1978 kwa lengo la kuikomboa ardhi yetu na kumtoa nduli Idd Amin Dada na genge la wahuni wenzie.
Vita ile haikuwa na maana tulikuwa tunawachukia sana raia wa Uganda ama mfumo wao wa maisha, la hasha, Waganda walikuwa ni ndugu na rafiki zetu kwa miaka mingi sana hata kabla Amini na wapuuzi wenzake hawajaingia madarakani.
Uamuzi wa kuivamia ardhi ya mkoa wa ziwa Magharibi (Kagera) haukuwa na ridhaa ya waganda hata kidogo bali ni maamuzi ya kipuuzi na kichokozi yaliyofanywa utawala wa kidhalimu wa dikteta Amini dada.
Nimejaribu kuanza mbali kwa kukumbushia vita ya Kagera na hivyo ndivyo inavyopaswa kueleweka kwa jamii ya watanzania kwamba, yule aliyekamatwa na Polisi ni "Emmaus Mwamakula" na hakukamatwa kwa sababu ya "uaskofu wake" au Jeshi la Polisi linalichukia sana kanisa la "Moravian Uamsho" ila alikamatwa kwa maana kuhamasiaha maandamano na kudai katiba mpya ni uamuzi wake binafsi na sio msimamo wa kanisa kama taasisi inayojitegemea.
Hili la huyu baba askofu limekaa hivi, hizi itikadi za kisiasa za mtu mmoja anayejulikana kama askofu kamwe haziwezi kuwa itikadi za wafuasi wote wa kanisa.
Serikali, kwa umoja wake, ina jukumu la kuunda taratibu za msingi pamoja na sheria zinazohitajika katika jamii ili kuweza kuruhusu watu wote kuishi maisha yao kama watakavyo pasipo kila mmoja kuleta bughudha kwa mwingine.
Ikiwa mtu anataka kuongeza itikadi zake binafsi za kisiasa katika sheria/misingi ya kanisa ambayo kila mtu anapaswa kufuata, swali la kwanza litakaloibuka ni "Je! Ni itikadi ipi/mlengo upi wa kisiasa ni sahihi utakaofaa?"
Itakuwa ni bahati nzuri sana kama kutapatikana kiwango chochote cha makubaliano/ maridhiano juu ya swali hilo muhimu na la msingi sana. Vile vile inaweza ikawa ni bahati mbaya sana, kwa maana vita nyingine ya wenyewe kwa wenyewe (ndani ya kanisa) inaweza kuibuka juu ya suala hilo hilo la kisiasa (katiba mpya kwenye muktadha ya kesi ya baba askofu)
Kama ambavyo mtu huchagua taaluma anayopenda kuisomea ama kiwango cha elimu anachopenda kuishia, ndivyo ilivyo hata katika siasa. Misimamo ya kisiasa ni chaguo.
Hakuna mtu anayepaswa kulazimishwa kufuata itikadi za mtu mwingine eti kwa kuwa ni kiongozi katika ngazi fulani ya kanisa. Hapana. Kanisa halifanyi kazi hivyo hata kidogo ndugu zangu kwa maana hakuna mtu anayeweza kulazimishwa kuamini kwamba katiba ya sasa ni sahihi ama sio sahihi.
Kama hiyo ndio hali halisi, sasa kwa nini umshawishi mtu yeyote afuate kitu ambacho haamini? Dini nyingi hutoa kanuni na miongozo ya kimaadili kwa washiriki wao kufuata.
Watu wengine, kwa makusudi kabisa, wanataka kuchanganya dini na siasa ili kila mtu alazimike kufuata itikadi sawa na zao kwa malengo wayajuayo wao wenyewe jambo ambalo sio sahihi hata kidogo.
Kwa mfano, Mimi binafsi sinywi pombe. Sikuwahi kujifunza kunywa kwa sababu dini yangu inafundisha kujiepusha na pombe. Inawezekana kabisa kwamba mtu mwingine anaweza kuwa alianza kunywa alipotimiza umri wa miaka 21, lakini baadaye aliamua kuacha na hakunywa tena kwa sababu aligundua alikuwa anaenenda kinyume na dini yake. Kwa mfano huo mdogo, je jamii nzima ikatazwe kunywa beer kwa staha eti kwa kuwa imani yangu mimi mtu mmoja inakataza? Jibu ni rahisi tu kuwa "HAPANA".
Je! sehemu iliyobaki ya waumini wote wa Kanisa ilazimishwe kuingia katika makatazo fulani fulani kwa sababu ya misimamo ya kisiasa ya mtu mmoja ama kikundi cha watu wachache wanaotaka kuingiza kanisa katika siasa? La hasha!
Ninaomba kumalizia kwa kusema, hoja za kisiasa zinazolenga kulazimisha itikadi za mtu mmoja au kikundi cha watu wachache ndani ya hizi dini/imani zetu juu ya wengine zinapaswa kukemewa na kuwekwa nje kabisa ya kanisa.
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Kwanza kabisa ninaomba ieleweke kwa kila mmoja wetu ya kwamba, Tanzania ililazimika kupigana vita ya Kagera mwaka 1978 kwa lengo la kuikomboa ardhi yetu na kumtoa nduli Idd Amin Dada na genge la wahuni wenzie.
Vita ile haikuwa na maana tulikuwa tunawachukia sana raia wa Uganda ama mfumo wao wa maisha, la hasha, Waganda walikuwa ni ndugu na rafiki zetu kwa miaka mingi sana hata kabla Amini na wapuuzi wenzake hawajaingia madarakani.
Uamuzi wa kuivamia ardhi ya mkoa wa ziwa Magharibi (Kagera) haukuwa na ridhaa ya waganda hata kidogo bali ni maamuzi ya kipuuzi na kichokozi yaliyofanywa utawala wa kidhalimu wa dikteta Amini dada.
Nimejaribu kuanza mbali kwa kukumbushia vita ya Kagera na hivyo ndivyo inavyopaswa kueleweka kwa jamii ya watanzania kwamba, yule aliyekamatwa na Polisi ni "Emmaus Mwamakula" na hakukamatwa kwa sababu ya "uaskofu wake" au Jeshi la Polisi linalichukia sana kanisa la "Moravian Uamsho" ila alikamatwa kwa maana kuhamasiaha maandamano na kudai katiba mpya ni uamuzi wake binafsi na sio msimamo wa kanisa kama taasisi inayojitegemea.
Hili la huyu baba askofu limekaa hivi, hizi itikadi za kisiasa za mtu mmoja anayejulikana kama askofu kamwe haziwezi kuwa itikadi za wafuasi wote wa kanisa.
Serikali, kwa umoja wake, ina jukumu la kuunda taratibu za msingi pamoja na sheria zinazohitajika katika jamii ili kuweza kuruhusu watu wote kuishi maisha yao kama watakavyo pasipo kila mmoja kuleta bughudha kwa mwingine.
Ikiwa mtu anataka kuongeza itikadi zake binafsi za kisiasa katika sheria/misingi ya kanisa ambayo kila mtu anapaswa kufuata, swali la kwanza litakaloibuka ni "Je! Ni itikadi ipi/mlengo upi wa kisiasa ni sahihi utakaofaa?"
Itakuwa ni bahati nzuri sana kama kutapatikana kiwango chochote cha makubaliano/ maridhiano juu ya swali hilo muhimu na la msingi sana. Vile vile inaweza ikawa ni bahati mbaya sana, kwa maana vita nyingine ya wenyewe kwa wenyewe (ndani ya kanisa) inaweza kuibuka juu ya suala hilo hilo la kisiasa (katiba mpya kwenye muktadha ya kesi ya baba askofu)
Kama ambavyo mtu huchagua taaluma anayopenda kuisomea ama kiwango cha elimu anachopenda kuishia, ndivyo ilivyo hata katika siasa. Misimamo ya kisiasa ni chaguo.
Hakuna mtu anayepaswa kulazimishwa kufuata itikadi za mtu mwingine eti kwa kuwa ni kiongozi katika ngazi fulani ya kanisa. Hapana. Kanisa halifanyi kazi hivyo hata kidogo ndugu zangu kwa maana hakuna mtu anayeweza kulazimishwa kuamini kwamba katiba ya sasa ni sahihi ama sio sahihi.
Kama hiyo ndio hali halisi, sasa kwa nini umshawishi mtu yeyote afuate kitu ambacho haamini? Dini nyingi hutoa kanuni na miongozo ya kimaadili kwa washiriki wao kufuata.
Watu wengine, kwa makusudi kabisa, wanataka kuchanganya dini na siasa ili kila mtu alazimike kufuata itikadi sawa na zao kwa malengo wayajuayo wao wenyewe jambo ambalo sio sahihi hata kidogo.
Kwa mfano, Mimi binafsi sinywi pombe. Sikuwahi kujifunza kunywa kwa sababu dini yangu inafundisha kujiepusha na pombe. Inawezekana kabisa kwamba mtu mwingine anaweza kuwa alianza kunywa alipotimiza umri wa miaka 21, lakini baadaye aliamua kuacha na hakunywa tena kwa sababu aligundua alikuwa anaenenda kinyume na dini yake. Kwa mfano huo mdogo, je jamii nzima ikatazwe kunywa beer kwa staha eti kwa kuwa imani yangu mimi mtu mmoja inakataza? Jibu ni rahisi tu kuwa "HAPANA".
Je! sehemu iliyobaki ya waumini wote wa Kanisa ilazimishwe kuingia katika makatazo fulani fulani kwa sababu ya misimamo ya kisiasa ya mtu mmoja ama kikundi cha watu wachache wanaotaka kuingiza kanisa katika siasa? La hasha!
Ninaomba kumalizia kwa kusema, hoja za kisiasa zinazolenga kulazimisha itikadi za mtu mmoja au kikundi cha watu wachache ndani ya hizi dini/imani zetu juu ya wengine zinapaswa kukemewa na kuwekwa nje kabisa ya kanisa.
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.