Dhambi 7 kuu

Dhambi 7 kuu

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
23,625
Reaction score
56,952
leo hebu tujadili hizi dhambi saba ambazo ndio kama mizizi saba ya dhambi zote za ulimwengu huu...kwamba kupitia hizi ndio zao la madhambi yote unayojua na kuyafahamu hapa duniani

Kwa mshangao wa wengi dhambi nyingi unazowaza si kati ya hizo saba.. Hebu tuzipitie moja baada ya nyingine

1. Tamaa(lust) tamaa hii ni ile ya utamanifu wa kimwili, na kutaka kuitosheleza nafsi iwe kingono, na tamaa nyingine zote za nafsini na hisia za kimwili

2. Uroho(gluttony) uroho ni sehemu ya tamaa, lakini hapa ni kwenye kumiliki na kutawala zaidi..dhambi nyingi za uchawi na mauaji zimetokana na uroho

3. Choyo(greed)ukiangalia mfuatano huu utagundua kitu cha kushangaza mno, uchoyo ni tunda la uroho.,MTU mroho daima ni mchoyo .. Uroho na uchoyo haviachani

4.Wivu(envy)mtiririko ni uleule ,MTU mwenye wivu ni mchoyo ni mroho pia ana tamaa

5. Ghadhabu(wrath) hapa tumepoteza watu wengi na hata kugombana kutokana na ghadhabu za mmoja ama wengi..sababu kubwa zikiwa ni wivu choyo tamaa nk..

6. Uvivu(sloth)..kama ulikuwa hujui uvivu pia ni dhambi... Na matokeo ya dhambi hii ni kutaka kupata na kustarehe bila kutoka jasho hapa wizi utapeli udanganyifu vimefanyika sana

7. Kiburi(pride) unaweza pia kuita majivuno..kwamba Mimi ni mimi na hakuna zaidi yangu mimi...matatizo mengi yametokea kwenye jamii kutokana na kiburi na kujiona bora kuliko wengine (hata JF tunao)hii ni dhambi ya kunajisi uumbaji na kumkataa Mungu ama la kumkosoa.nknk

Hizi ndio dhambi saba kuu ...najua hakuna mkamilifu kati yetu na wote tunashiriki dhambi hizi kwa njia moja ama nyingine...na wote tunajijua udhaifu wetu ulipo ila kwa kiburi na unafiki wetu huwa tunajivika koti jeupe kuficha uchafu uliomo ndani yetu

Copy from Mshana Jr
 
Mshana Jr kalala au anapiga cha asubuhi
There is NO MAN Dead or Alive that has not fall short from the Glory of God. For All have sinned. The only perfect being to step on earth IS and Was Our Lord and Saviour Jesus Christ. Unapologetically! This world has so many truths and narratives but there can only be 1 Truth!
 
There is NO MAN Dead or Alive that has not fall short from the Glory of God. For All have sinned. The only perfect being to step on earth IS and Was Our Lord and Saviour Jesus Christ. Unapologetically! This world has so many truths and narratives but there can only be 1 Truth!
And one way to heaven
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom