Mwanamwana
Platinum Member
- Aug 1, 2011
- 9,604
- 22,714
Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Devotha Minja, amesema wanawake wengi nchini wanaishi maisha ya huzuni kutokana na mikopo inayowadhoofisha kiuchumi na kihisia.
Akizungumza mbele ya wakazi wa Kigoma Mjini katika mwendelezo wa mikutano ya hadhara ya chama hicho, Minja ameeleza kuwa endapo CHAUMMA kitaingia madarakani, kitaweka mikakati ya kuwawezesha wanawake kujishughulisha na shughuli za kiuchumi zisizowaumiza.
“Wanawake wengi hawana furaha kwa sababu ya mikopo ya kausha damu. Wanalazimika kuchukua mikopo hiyo ili kuendesha maisha ya familia zao, lakini mwisho wa siku inawaumiza,
Nataka CHAUMMA ikiingia madarakani, iwasaidie wanawake kuwa na furaha kwa kufanya shughuli ambazo hazitawaumiza,” amesema Devotha