"Duh!hii kali sasa.na baada ya hapo atatoka kwa msamaha wa rais."
MTU KWAO: Ndiyo msamaha wa Rais lazima. Yaani huyu kijana asiyejua kuendesha gari kama alivyokiri hapo awali, ameshawishiwa/amelazimishwa kukubali kwamba aliendesha?
Kuna kitu kinafichwa! Utata mtupu hasa tangu kifo cha ghafla cha yule mendesha mashitaka wa awali -- kifo kilichoelezwa kuwa na utata mkubwa.
Kesi hii imeendeshwa kama vile ya wauwaji wa Amran Kombe mwaka 1996 -- kuna baadhi yao walifia jela na wengine kupatikana na hatia -- lakini hatukuelezwa undani wa sababu ya kuuawa pamoja na kwamba Kombe aliinua mikono kujisalimisha. Hata hivyo hapo awali, mke wa Kombe hakuwa amepangwa kuwa shahidi, ingawa alikuwa eye-witness akiangalia tukio huku akijificha katika shamba la mahindi..
Tunakwenda kubaya sana.