James Martin
JF-Expert Member
- Apr 2, 2016
- 1,205
- 1,509
Inasikitisha kuona baadhi ya watu wakitumia jina la Marekani kueneza propaganda za kisiasa. Nimewasikia baadhi ya wajinga wakijigamba kuwa nchi fulani ina demokrasia ya juu kuliko Marekani!
Sasa ili kuweka mambo sawa inabidi kuwajibu hawa wapuuzi ili wasiendelee kuwajaza watu ujinga.
Kwanza, kuhusu ulalamikaji wa Donald Trump kuhusu upigaji wa kura kwa njia ya posta ni maoni yake binafsi. Utaratibu huo umekuwepo kwa miaka mingi bila ya kulalamikiwa.
Pili, kuhusu Trump kwamba anaweza kukataa kuachia ofisi ni jambo la kupuuza. Ki historia jambo hilo halijawahi kutokea kwenye taifa hilo. Halafu hata ikitokea kwamba atakataa kuachia ofisi bado taifa hilo lina vyombo huru vya kumshughulikia mgombea huyo.
Napenda kumalizia kwa kusema kwamba hata kama kukitokea kasoro za hapa na pale kwenye uchaguzi wa Marekani lakini bado wataweza kuzitatua kwasababu wana vyombo madhubuti na huru. Vyombo madhubuti na huru vya kutatua mambo yao ndio tofauti kubwa kati yao na nchi isiyo ya kidemokrasia.
Sasa ili kuweka mambo sawa inabidi kuwajibu hawa wapuuzi ili wasiendelee kuwajaza watu ujinga.
Kwanza, kuhusu ulalamikaji wa Donald Trump kuhusu upigaji wa kura kwa njia ya posta ni maoni yake binafsi. Utaratibu huo umekuwepo kwa miaka mingi bila ya kulalamikiwa.
Pili, kuhusu Trump kwamba anaweza kukataa kuachia ofisi ni jambo la kupuuza. Ki historia jambo hilo halijawahi kutokea kwenye taifa hilo. Halafu hata ikitokea kwamba atakataa kuachia ofisi bado taifa hilo lina vyombo huru vya kumshughulikia mgombea huyo.
Napenda kumalizia kwa kusema kwamba hata kama kukitokea kasoro za hapa na pale kwenye uchaguzi wa Marekani lakini bado wataweza kuzitatua kwasababu wana vyombo madhubuti na huru. Vyombo madhubuti na huru vya kutatua mambo yao ndio tofauti kubwa kati yao na nchi isiyo ya kidemokrasia.