Vianelly Vian
JF-Expert Member
- Jul 26, 2011
- 337
- 100
Nimekuwa nikifuatilia bunge la katiba na nimeona mapungufu mengi sana kubwa zaidi ni la wajumbe wengi kuto kujua maana ya democrasia.Tunapozungumzia democrasia huru ni kila kitu kuamuliwa kwa kupiga kura na mwenye kura nyingi ndiye anakuwa mshindi ukiangalia bunge unaona vyama vya upinzani havitaki kukubaliana na ukweli kuwa chama tawala kina wabunge wengi zaidi hivyo kila watakachokitaka lazima watakifanikisha kwasababu kura ndiye mwamuzi wa mwisho na mwenye kura nyingi ndiye mshindi.Kitendo cha wabunge wa upinzani Leo kutoka nje wakishinikiza matakwa yao yafanikiwe hiyo siyo democrasia na wala si uungwana,Kumekuwa na maoni kuwa kuutishwe mkutano wahadhara kukishitaki chama tawala kwa wananchi nimekuwa nikijiuliza wananchi hao ni wepi?maana kila mbunge anawananchi wake ambao wanamwamini na ndio waliompa kura,
Mwisho ushauri wangu ni kwamba mara nyingi nimeona vyama vya upinzani vinataka kuiona pepo bila kufa cha msingi kwanza wahakikishe wananchi tumewaamini kwenye majimbo na kuwapa kura nyingi ambazo zitawafanya wawe na wabunge wengi bungeni hivyo kufanikisha malengo yao pia Maana kwenye democrasia ya kweli maamuzi yote yanafanywa kwa kura na siyo kutoka nje ya bunge wala kuandamana
Mwisho ushauri wangu ni kwamba mara nyingi nimeona vyama vya upinzani vinataka kuiona pepo bila kufa cha msingi kwanza wahakikishe wananchi tumewaamini kwenye majimbo na kuwapa kura nyingi ambazo zitawafanya wawe na wabunge wengi bungeni hivyo kufanikisha malengo yao pia Maana kwenye democrasia ya kweli maamuzi yote yanafanywa kwa kura na siyo kutoka nje ya bunge wala kuandamana