Degree 4 ndio kitu gani?

My Son drink water

JF-Expert Member
Nov 30, 2016
4,932
13,286
Hii tabia ya watu kujiona wao ni classic kuliko wengine eti kwa sababu wana Degree nne inachefua sana.

Kwanza ni nani mvumbuzi wa elimu? na nini maana ya elimu?

Thomas Edison wakati akivumbua balbu alikuwa kasomea wapi na alikuwa na Degree ngapi za balbu?

Wright Brothers wakati anavumbua ndege alikuwa kasomea wapi? Na alikuwa na Degree ngapi za kutengeneza ndege?

Tesla wakati anavumbua engine, alikuwa kasomea wapi? na alikuwa na Degree ngapi za kutengeneza engine?

Hawa ni ma genius, wenye akili za kuzaliwa (talented) ambao leo hii dunia inakula matunda yao.

Mwanamuziki hana tofauti na mwandishi, kuandika habari za siasa huhitaji kuwa mwanasiasa, na kuimba vivyo hivyo.

Bob Marley hakuwa mwanasiasa, Lakini nyimbo zake nyingi zilikuwa za kisiasa.

The absence of wisdom creates disaster.
Wapo watu wenye Degree 4 wameajiriwa na watu wa darasa la saba.

Mfano mdogo, ni tajiri Kishimba, MB wa Kahama mjini.

Degree 4 ndo kitu gani?
 
My Son drink water,

Kuwa na Elimu Kubwa siyo Dhambi au Jambo baya na pia tusitake Kuhalalisha kuwa kutokusoma sana au Kutojiendeleza ni Sifa au Jambo jema bali kama una Fursa ya Kusoma basi itumie Usome kwani kuna Faida Kubwa za Mtu aliyesoma sana kuliko Mangumbaru ( Wajinga ) kama akina GENTAMYCINE ambao hata Diploma tu hawana. Shida yangu Kubwa kwa Waziri Mwakyembe ni namna tu ' alivyojimwambafai ' katika hali ya ' Upopoma ' kabisa juu ya Elimu yake Kubwa. Sidhani kama kwa Usomi wake huo mkubwa wa Degree zake Nne alipaswa kuja na aina hiyo ya Uwasilishaji kwani kwa jinsi alivyouleta Sisi wenye Akili Kubwa kuliko hizo Degree zake Nne na wala hatujasoma kama Yeye tumegundua kuwa Muimbaji ana Uwezo mkubwa wa Akili kuliko Yeye na huenda hivyo Vyuo Vikuu vyote alivyopita Yeye ( Mwakyembe ) wangesikia Nyimbo za Mkatoliki basi wangemnyang'anya Yeye Vyeti vyote alivyotunikiwa na akapewa Roma Mkatoliki kutokana na Meseji Kuntu kabisa zilizomo ndani ya huo Wimbo wake.
 
Field Marshal Dr. I.Dada, PhD, President of ..... mfano kuntu wa ngumbaro jingalao ambalo mnajua lilifikisha wapi ujinga wake. Unaweza kujimwambafai na ELIMU yako kama jingalao hilo lilivyofanya na ambalo ELIMU limejipachikia halafu WOTE mkafanana, ZERO. Pawepo basi na UTOFAUTI, msomi mzima na mambo ya kingumbaro wapi na wapi?

Ujinga kwa maana ya IGNORANCE haumaanishi kutokua na akili bali kutokua nazo yaweza kusababisha UJINGA.
 
Tangu anusurike kifo cha sumu akili yake haipo sawa!anahitaji tiba ya kiakili na saikolojia!!!mnakumbuka sakata la kwenda india?
 
GENTAMYCINE, Ni kweli kuwa na elimu kubwa ni vizuri na ni faida lakini elimu hiyo isipotumika vizuri na kubaki kujimwambafai ni upopoma

FB_IMG_1573890013567.jpeg


FB_IMG_1573956529213.jpeg
 
Huyu mzee mwakimango anapotea sana kwa kutokujua maandiko na kupungukiwa kwake na maarifa
 
Mzee Tarimo anaemiliki EKENFORDE ya Tanga ameajiri mpaka maprofesa na aliwahi kumwajiri aliyekuwa Waziri Dr Siame. Lakini yeye mzee Tarimo Ni darasa la Saba.
 
GENTAMYCINE,
Mojawapo ya digrii yake aliandika kuhusu ..Muungano ,na akatetea Muungano wa Serikali Tatu!na hii digrii ndio iliyompa Shhada ya Uzamivu.....kwa wakati mwingine Digrii nyingi NI upopoma tu...NI mtu aliyekomaa shule!
 
Mzee Tarimo anaemiliki EKENFORDE ya Tanga ameajiri mpaka maprofesa na aliwahi kumwajiri aliyekuwa Waziri Dr Siame. Lakini yeye mzee Tarimo Ni darasa la Saba.
dah... umenikumbusha mbali sana mkuu, but all in all sasa naona anafeli, majengo anayauza,mikopo aliyonayo hailipiki,wanawe vilaza hawawezi kuendesha miradi,mzee ndo kazeeka tena ...yaaaan!
 
Back
Top Bottom